Jamani hatuna Serikali tena!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
How in the shag can a minister who is responsible for good governance and indirectly supervision of TISS utter such childish, nusery school responses?

How can our government be sound asleep when sensitive matters are at stake?

Inashangaza sana majibu ya Sophia Simba na Manumba kushangaa matokeo ya kuchunguzwa Chenge na SFO!

Inatia aibu kuwa wakati SFO walipokuja na kutoa rasmi tamko kuwa tunamchunguza Chenge, si Rais, Mawaziri, Polisi au Usalama walioshtuka na kuanza kazi kupeleleza inakuwaje aliyekuwa Mwanasheria Mkuu ambay ni Waziri katika Serikali na mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu za CCM anachunguzwa kwa tuhuma za Rushwa na Serikali ya Uingereza?

Can anyone with right mind respond to that?

This is what Simba stated as qouted by Tanzania Daima

Akizungumza na Tanzania Daima mjini Dodoma jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Sophia Simba, alisema serikali ilikuwa bado haijaanza kumfanyia uchunguzi Chenge na kwamba suala hilo lilikuwa likishughulikiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini Uingereza ya SFO.
Waziri Simba alisema maofisa wa SFO walifika hapa nchini na kuomba nyaraka na taarifa zote zinazomhusu Chenge na wakazichukua na kurudi kwao ambako wanaendelea na uchunguzi wao.
Aidha, waziri huyo alishindwa kueleza kama serikali ilikuwa imechukua hatua zozote kuchunguza iwapo waziri huyo aliyerejesha nchini juzi akitokea China alikuwa amewasilisha taarifa za kuwa na akaunti ya fedha katika Kisiwa cha Jersey katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi..
Waziri Simba, alieleza kuwa, kwa sasa serikali inajikita katika kuandaa utaratibu ambao utaiwezesha kupata fedha ambazo zilitozwa zaidi kuliko gharama halisi ya rada hiyo, iliyonunuliwa mwaka 2002.
“Wale (SFO) ndio wamekuja kutaka mafaili na taarifa kuhusu Chenge na wakapewa halafu wameondoka kwenda kufanya uchunguzi wao, sasa sisi hatuna cha kufanya zaidi ya kusubiri matokeo,” alisema Simba.
Alisema serikali haimtuhumu Chenge kwa kumiliki akaunti yenye fedha nyingi kiasi hicho, bali wale wenye kujua mambo hayo ndio watakaokuwa na jukumu la kufanya uchunguzi husika.
Alisema kifungu cha 6(i) cha Sheria namba 13 ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, kinabainisha wazi kuwa Kamishna wa Sekretariati ya Maadili ya Viongozi anayo mamlaka ya kuruhusu kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya kiongozi wa umma.
Alisema kutokana na sheria hiyo, kamishna aliwaruhusu wataalamu wa SFO kuchukua taarifa kuhusu Waziri Chenge, jambo ambalo mtu yeyote anaweza kulifanya kama kamishna atakubaliana na sababu alizozitoa.
Waziri huyo ambaye hivi karibuni alikaririwa na gazeti moja akionyesha mshtuko wa wazi dhidi ya tuhuma hizo za Chenge hata kufikia hatua ya kuhoji pengine alizipata kwa kuuza ng’ombe wake, alisema taarifa za Chenge kumiliki kiasi kikubwa cha fedha wamezipata kupitia vyombo vya habari.
“Sisi tuna taratibu za kufanya kazi na kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili watumishi wa umma. Hatuwezi kufanya uchunguzi wa kila taarifa inayotolewa na vyombo vya habari,” alisema Simba.
Alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete alishaweka bayana msimamo wa Tanzania kuhusu suala la ununuzi wa rada ya kijeshi iliyonunuliwa kwa paundi za Uingereza milioni 28.
Alisema kama kuna tatizo lolote kwa mtumishi wa umma kuhusishwa katika tuhuma za rushwa, serikali itaangalia cha kufanya baada ya kupata taarifa za uhakika, baada ya uchunguzi kufanyika. “Kama kuna ulazima wa kufanya uchunguzi kuhusu kiongozi wetu, tutaufanya, lakini si kwa shinikizo kutoka sehemu fulani au kwa sababu ya maneno ya watu,” alisema Simba.

Naye Manumba anatoa hoja kama hii, eti anasubiri amri kuzima moto..

Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alisema ofisi yake haijapokea taarifa yoyote rasmi ya maandishi kutoka ngazi za juu kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi Waziri Chenge.
“Kwa kweli suala hili nimelisoma kwenye magazeti tu… naomba tuwe na subira,” alisema DCI Manumba katika mahojiano na gazeti hili jana.
Alisema kama ofisi yake ikipokea taarifa ya kumfanyia uchunguzi Chenge, haitasita kufanya hivyo kwa vile kazi yake kubwa ni kushughulikia matatizo kama hayo.
“Tutafika hata huko anakodaiwa kuweka fedha hizo kuchunguza, kwa vile hivi sasa kuna njia nyingi za mawasiliano,” alisema Manumba.
Hata hivyo, alisema kulingana na aina ya suala lenyewe, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndiyo yenye dhamana kubwa ya kuendesha uchunguzi.
DCI, ambaye hakutaka kuingia kiundani juu ya suala hilo, alisema taasisi nyingi za serikali zimegawana majukumu kwa mujibu wa sheria. “Wenzetu wa TAKUKURU naamini hivi sasa wako katika nafasi nzuri zaidi ya kulizungumzia hili, mimi hapa nakupa tu hali ilivyo ya mgawanyiko wa majukumu yetu,” alisema

This is crap, and Watanzania tumetukanwa na viongozi wetu!
 
"Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Sophia Simba, alisema serikali ilikuwa bado haijaanza kumfanyia uchunguzi Chenge na kwamba suala hilo lilikuwa likishughulikiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini Uingereza ya SFO."

Mwongo. PCCB na SFO wanafanya kazi hii kwa pamoja.

"Wale (SFO) ndio wamekuja kutaka mafaili na taarifa kuhusu Chenge na wakapewa halafu wameondoka kwenda kufanya uchunguzi wao, sasa sisi hatuna cha kufanya zaidi ya kusubiri matokeo,"

This is rubbish, yeye ana dhmana ya kujua, ila hakutaka kujua ndo maana hajui. Ni mvivu.



"Alisema serikali haimtuhumu Chenge kwa kumiliki akaunti yenye fedha nyingi kiasi hicho, bali wale wenye kujua mambo hayo ndio watakaokuwa na jukumu la kufanya uchunguzi husika."

Na wasipofanya uchunguzi? Huyu mama anatia aibu,

"alisema taarifa za Chenge kumiliki kiasi kikubwa cha fedha wamezipata kupitia vyombo vya habari."

Rev, huyu mama ni timamu kweli? si kasema: "suala hilo lilikuwa likishughulikiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini Uingereza ya SFO.

"Sisi tuna taratibu za kufanya kazi na kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili watumishi wa umma. Hatuwezi kufanya uchunguzi wa kila taarifa inayotolewa na vyombo vya habari,"

kwa hiyo SFO na PCCB waliwaomba kupitia vyombo vya habari?

Kwa kifupi nafasi hii haiwezi. Na pengine hafai hata kupewa standard seven afundishe.

Kifupi, yeye akiwa waziri hana coordination na vyombo husika, ama hajui asemeje, hata kama anataka hatiua za kiuchunguzi zisifahamike zimefikia wapi asingeokea pumba namna hii!
 
Duuh, threads za wiki hii zinaweza kukufanya mtu uukane Utanzania..... anyways, tufurumuane humu humu mpaka kieleweke. Truth always prevail.
 
Huo ndio ukweli wa mambo. Hatuna serikali mambo yanaenda shakalabaghala tu, ufisadi kila kona na mafisadi hata woga hawana maana wanajua hakuna atakayethubutu kuwagusa. Shilingi Bilioni 155 zilizochotwa na Meremeta pale BoT hadi hii leo hakuna uchunguzi wowote!

Shilingi 133 zilichotwa bilioni 133 hadi hii leo wahusika hawajatajwa hadharani wala kukamatwa. Kama alivyosema Mkuu wa polisi kwamba wakikamatwa nchi inaweza kuwaka moto. Pinda naye akasema kwamba ni matajiri wakubwa hawa hivyo kuna ugumu wa kushughulikia mafisadi hao.

Inadaiwa kati ya bilioni 133 zilizokupuliwa, bilioni 60 zimesharudishwa ukiwauliza wahusika wanaotangaza hivyo kama zimerudishwa kwa cash, cheques or money order wanang'aa macho. Ukiwaomba majina ya waliorudisha na kiasi walichorudisha wanang'aa macho. Ukiwauliza pesa hizo zimewekwa katika bank ipi na kama wanafahamu account number, wanang'aa macho.

Kama unavyosema Rev hatuna serikali bali tuna mafisadi na wasanii wanaoendeleza ufisadi dhidi ya Watanzania
 
Duuh, threads za wiki hii zinaweza kukufanya mtu uukane Utanzania..... anyways, tufurumuane humu humu mpaka kieleweke. Truth always prevail.

Mkuu

Katika kusoma thread za wiki hii nimegundua Mkuu Rev alicho-conclude kinatosha hatuna serikali kabisa.

Walioko OFISINI hakuna anayejua haswa anafanya kazi gani. nasikia hata kuwa na account nje ya nchi wakati unahishi Tanzania bila Gavana kuwa na taarifa kitaratibu zetu ni uvunjaji wa sheria.

Kimsingi Chenge Tayari ameisha kubali kuwa ana vijisenti UK, lakini vile vile inaonekana hajatoa taarifa kwa Gavana, ina maana amevunja sheria za nchi na anatakiwa mara moja awe ameisha funguliwa mashitaka.

Lakini unaona kote hakuna mwenye kuwajiba.

Kwa maana nyingine kumbe huwa hatuna serikali
 
Are these really prudent Tanzanian leaders?
Kwa nini waseme hizi ni habari walizosikia kwenye magazeti na kunyamaza kimya wala wasiwapatie wananchi majibu yanayohusu pesa yao??.

Basi upo mfumo mbovu sana wa utendaji ktk serikali,tena wa kuogopana na kulindana katika maovu,hatima yake ni kufuga bomu ambalo itafikia mda litalipuka.

Namuuliza mheshimiwa Waziri na mkurugenzi wa makosa ya jinai,ina maana hayo magazeti yamezusha??Basi yafungieni,yasitolewe tena maana yanapotosha umma wa Watanzania kwa habari ambazo ni uzushi na zinazoweza kuhatarisha amani na usalama wa Taifa hili.

Na hizi habari kama ni kweli basi hamjui mlitendalo ni vema mkae kimya kama kawaida yenu na kutumia ile falsafa ya mimi si msemaji wa hili na lile,kuliko kujichafua kwa kitu ambacho ni dhahiri.

Naililia Tanzania yangu maana hatima yake siijui.
 
kuililia tu tanzania haitasaidia, cha msingi ambacho kitatubeba ni kuyafikisha maovu yooote kwa wale ambao wanawakata kodi watu wao kwa nia ya kutusaidia sisi, ile hali wakituma pesa serikali yetu wanagawana na mtanzania anaishia kuugulia ugumu wa maisha tu.
 
Rev Huhitaji kuongeza neno. Yaani ni AIBU AIBU AIBU TUPU. Natamani ningekuwa na uwezo nikimbilie hata Rwanda. Viongozi kazi hawajui hata kuongea!!! Jamani hivi tunaenda wapi. Hata mtoto mdogo angeulizwa maswali hayo angekuja na jibu.
 
kuililia tu tanzania haitasaidia, cha msingi ambacho kitatubeba ni kuyafikisha maovu yooote kwa wale ambao wanawakata kodi watu wao kwa nia ya kutusaidia sisi, ile hali wakituma pesa serikali yetu wanagawana na mtanzania anaishia kuugulia ugumu wa maisha tu.

Gang chomba, nimekupata sana!
Unajua kuna wakati unashikwa najazba lakini wa kumalizia hiyo hasira haupaoni.

Ni kweli lazima walipa kodi wajue wanaibiwa pesa yao
 
Naturaly speaking... Kuna kiwango cha kufanya upuuzi kwenye maisha ya kila siku, hasa kwnye nagazi ya uongozi! What always seem as "majanga ya kiasili" ni mambo yanayoepukika kabisa.

Nature ya Mtu ni Utu!

Utu ni pamoja na maadili yake. Na hasa maadili ya Uongozi. Hakuna mtu hakuzaliwa na utu..lakini kwenye process ya kuishi maisha ya kila siku..wengine Utu unajengeka na kuimarika..na wengine UTU unafifia na kuporomoka hata kuuvaa unyama wazi hadharani. Mtamshi gani viongozi wetu wanatoa?? Nini kinawafanya wasione kinachotakiwa kuonwa? Kwanini wasiwe straight? Giza gani limewakumba?

Kwa sababu hakuna bingwa wa kupinga nature yake na akabaki salama...Hawa viongozi wetu waamke na waone mchezo wanaoucheza hapa...kwa kufanya mzaha na mambo ya msingi ya kitaifa na wananchi waliowachagua ni hatari kubwa.

Tume ya maadili na viogozi iko wapi? wanajaribu kufanya mazingaubwe gani? Ni tume ya Kuwaamsha viongozi warudi kwenye ASILI yao, maadili ya utu, utu katika uongozi! Ni tume ya kuwakumbusha kila mara viongozi wapi wameukana utu ndani ya uogozi wao! Viogozi wetu wanahitaji kukarabatiwa upya kabisa. Lakini sasa hawa wa utawala bora nao ndio hawa ...what a bad news? Tunakwenda wapi? Basi hawa wa "maadili ya uongozi" wako wapi?

Kama hilo hawalifanyi...Wanategemea nini? Kama sio janga la kitaifa?

Janga la Viongozi wote kuukana utu na kuuvaa unyama ambao unajulika kama UFISADI au jina lolote la kuwakilisha Usaliti wa utu!

Naturaly mechanisim ya ku_recover asili na heshima ya mtu na hasa mtanzania, itatokea na kushika hatamu...Lakini nani anaweza kuitabiri itakuja kwa sura gani?

Kwa taarifa...Mara nyingi kwa nyakati kama hizo recovery process inakuja kama JANGA ...tunaadika hapa kukemea, kuonya na kuonyesha kuwa janga kama hili linaweza kuepukika...!! Ni juu yenu nyie VIONGOZI mlio na wajibu kuogoza kwa busara na kwa madili ya kiutu, Kusikiliza na kutekeleza lile lililo sahihi!! vinginevyo you will have to do this in hard way!! Is that what you want?
 

Kama unavyosema Rev hatuna serikali bali tuna mafisadi na wasanii wanaoendeleza ufisadi dhidi ya Watanzania

TANZANIA, TANZANIA NCHI YANGU, NAKULILIA. NIKUONAPO TANZANIA WEE UNAVYOSULUBIWA NA MANYANG'AU NAKULILIA, TANZANIA TANZANIA NCHI YANGU, HALI HII MPAKA LINI, ......nashindwa kuendelea ......
 
Kweli kabisa, serikali ipo kama haipo vile, yaani kama waziri wa utawala bora alivyojiropokea ameondoa mashaka yoyote yaliyokuwepo kuhusu uwezo wake kiutendaji na kuzua swali, je aliyempa huo wadhifa alikuwa anafikiria nini?
 
How in the shag can a minister who is responsible for good governance and indirectly supervision of TISS utter such childish, nusery school responses?

How can our government be sound asleep when sensitive matters are at stake?

Inashangaza sana majibu ya Sophia Simba na Manumba kushangaa matokeo ya kuchunguzwa Chenge na SFO!

Inatia aibu kuwa wakati SFO walipokuja na kutoa rasmi tamko kuwa tunamchunguza Chenge, si Rais, Mawaziri, Polisi au Usalama walioshtuka na kuanza kazi kupeleleza inakuwaje aliyekuwa Mwanasheria Mkuu ambay ni Waziri katika Serikali na mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu za CCM anachunguzwa kwa tuhuma za Rushwa na Serikali ya Uingereza?

Can anyone with right mind respond to that?

This is what Simba stated as qouted by Tanzania Daima



Naye Manumba anatoa hoja kama hii, eti anasubiri amri kuzima moto..



This is crap, and Watanzania tumetukanwa na viongozi wetu!

Jamani nisaidieni nasikia kutapika. natamani nitukane lakini katika matusi yote ninayojua hakuna linalofaa!!!!!!!!!!
 
Leaders` Ethics watchdog mum on minister Chenge

2008-04-18 09:30:50
By Angel Navuri

The Public Leaders` Ethics Secretariat has remained tight-lipped on whether the Infrastructure Development minister Andrew Chenge has ever declared the 1.2bn/- he is reported to have deposited in an overseas bank account.

The law governing the public leadership code of ethics requires ministers and Members of Parliament to declare their wealth upon assuming office.

Judge Stephen Ihema, the secretariat`s commissioner, has for three days running been reluctant to respond to questions from journalists on the matter.

When approached for comment yesterday, he told this reporter through his public relations officer to draft her questions and bring them to his office.

According to sources, many questions have been forwarded to the office from different media houses since last week but no response had been forthcoming.

Judge Ihema is the secretariat`s spokesperson and effectively the only person who could answer the questions.

The Minister of State in the Presidents Office (Good Governance), Sofia Simba, meanwhile told The Guardian yesterday that the secretariat was the relevant institution to explain whether Chenge had declared the money as part of his wealth.

The secretariat``s key functions include monitoring public leaders� abuses of power, accountability and transparency.

The allegations against Chenge were first reported by the Guardian newspaper of the UK, which revealed that British investigators involved in a three-year inquiry over the controversial sale of a military radar to Tanzania had located more than $1m in his account in Jersey.

Chenge, Tanzania`s Attorney General for ten years until his ministerial appointment, told journalists on his return from China on Wednesday that the allegations were ``too serious`` and that he needed time to respond to them.

The embattled minister was in China as part of President Jakaya Kikwete�s entourage on an official visit there when details of his foreign offshore bank account made newspaper headlines in Tanzania.

In his remarks on Wednesday he said he believed ``these baseless and malicious`` allegations related to the purchase of the radar from UK`s leading arms manufacturers, BAE Systems. He swore to fight back.

As AG, Chenge was the government`s chief legal advisor when the 28 million pounds sterling (approx. 70bn/-) radar was purchased at what is alleged to be a massively inflated price.

SOURCE: Guardian
 
"Viongozi" wa bongo walivyo wapuuzi hata hawajui ku cover their own asses.Hawa nao hata baada ya kuona Chenge is a sinking ship bado wanasuasua kumbabua!
 
Kweli kabisa, serikali ipo kama haipo vile, yaani kama waziri wa utawala bora alivyojiropokea ameondoa mashaka yoyote yaliyokuwepo kuhusu uwezo wake kiutendaji na kuzua swali, je aliyempa huo wadhifa alikuwa anafikiria nini?

..alikuwa hafikiriii.

..alikuwa anampa wadhifa!
 
Wabongo walivyo wapuuzi hata hawajui ku cover their own asses.Hawa nao hata baada ya kuona Chenge is a sinking ship bado wanasuasua kumbabua!

..when a ship is sinking,there is chaos!

..you just can't think straight!
 
..natoka nyumbani asubuhi,nayaona mawingu mazito meusi yametanda angani.

..najiuliza,"itanyesha kubwa au ndogo?. na ikiisha,kutakuwa na madimbwi au mafuriko?"

..najishauri nichukue mwamvuli,lakini nabaini sitouhitaji sana,kwani nitajibanza pembeni kama itanikuta njiani. mvua za namna hii huwa kubwa na si busara kuamini mwamvuli utakufaa. ni bora ukajibanza mapema sehemu,ipite.

..mvua inakuja waungwana!tujiandae kuloa! na ikishakauka ardhini,majani na mimea mipya itaota!
 
How in the shag can a minister who is responsible for good governance and indirectly supervision of TISS utter such childish, nusery school responses?

How can our government be sound asleep when sensitive matters are at stake?

Inashangaza sana majibu ya Sophia Simba na Manumba kushangaa matokeo ya kuchunguzwa Chenge na SFO!

Inatia aibu kuwa wakati SFO walipokuja na kutoa rasmi tamko kuwa tunamchunguza Chenge, si Rais, Mawaziri, Polisi au Usalama walioshtuka na kuanza kazi kupeleleza inakuwaje aliyekuwa Mwanasheria Mkuu ambay ni Waziri katika Serikali na mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu za CCM anachunguzwa kwa tuhuma za Rushwa na Serikali ya Uingereza?

Can anyone with right mind respond to that?

This is what Simba stated as qouted by Tanzania Daima



Naye Manumba anatoa hoja kama hii, eti anasubiri amri kuzima moto..



This is crap, and Watanzania tumetukanwa na viongozi wetu!

Ingawa si utaratibu unaotumika kokote ulimwenguni, I think kuna haja kubwa ya kuwapima IQ viongozi wetu. This is too much. Under normal circumstances, mtu mwenye IQ ya kutosha hawezi toa maneno in the way huyu waziri anavyojikanyaga. Hii ni aibu.

Hivi mda ukapita na wakaacha nafasi zao wanazozishika kwa sasa, je wataweza ku-substantiate semi zao wanazozitueleza siku hizi? I wonder!!!!

Can you imagine, mtu dizaini hizi ndio wanao-determine mustakabali wa Taifa.... Inawezekanaje minds za dizaini hii kutoa ideas za maana za kuendeleza taifa? NEVER!!!! Tanzania itaendelea kuwa masikini milele kama tukiacha mtu za dizaini hii kuendelea kuwa decision makers.

We deserve better......
 
Back
Top Bottom