Jamani embu nisaidieni ktk hili suala la sheria za hapa bongo na mwenendo wa maisha yetu wabongo!

Makelelejr

New Member
Sep 7, 2011
3
0
Kuna sheria nyingi sana mfano, sheria za ndoa, ardhi, kazi, n.k. Mimi binafsi kwa kifupi ndiyo kwanza nimeanza kujitegemea ktk hili nimeanza kukutana na mambo mengi nahisi yanakanganya sana na hii ni kuokana na mifumo ya utawala ya nchi yetu.

Sisi tumetoka ktk mfumo wa kijamaa ambapo kuna mambo yalihitajika kuamriwa kijamaa, vilevile kuna mambo kutokana na jinsi tulivyokua tumejengwa kiupendo kati yetu tuliweza jua sote ni wa tanzania twapaswa kujaliana kwani tunajenga nchi yetu.

Mabadiliko hayakwepeki, yamekuja tumeyapokea, kutoka kule kwenye ujamaa wetu na kujaliana kama wa Tanzania na kuingia kwenye ubepari. Tupo humo sasa. Ni mazingira tofauti sana lakini hatuna budi kuyakubali kwani ndiyo hivyo mwenye nacho huongezewa na wewe ambaye huna ni ngazi zuri kwa huyu mwenye nacho.

Sote tunajua maisha bora ni NYUMBA, sekta hii asilimia 90% ni binafsi toka ile sera ya hawa tunaoamini watatufikisha tunakotaka kwenda ya kuuza nyumba za serikali na sekta hiyo kufikia kiasi hicho.

Ktk Hili la nyumba tunazopanga hivi kuna SHERIA YOYOTE INAYOMDHIBITI HUYU MWENYE NYUMBA BINAFSI KTK KUMSIMAMIA HUYU ASIYEKUWA NA UWEZO WA KUJENGA SASA HIVI, HUSUSANI KTK UPANGAJI KODI ZA HIZI NYUMBA TUNAZOPANGA SASA HIVI. KWANI KODI HUPANGWA KIHOLELA NA MWENYE NYUMBA PASI NA KIFUNGU CHOCHOTE KINACHOONYESHA KUMSIMAMIA HUYU MPANGAJI.

Naomba mnisaidie hili kama kuna anayejua kuna sheria ya upangaji nyumba usimamizi wa mkataba kati ya mwenye nyumba na mpangaji, vilevile kama kuna mamlaka au wakala ya kiserikali inayoshulikia hili hususani kwenye upangaji bei za hizi nyumba tunazopanga kwa maendeleo yetu na umoja wa taifa letu. Naomba msaada wako ewe mwanajamii.
 
Kuna sheria nyingi sana mfano, sheria za ndoa, ardhi, kazi, n.k. Mimi binafsi kwa kifupi ndiyo kwanza nimeanza kujitegemea ktk hili nimeanza kukutana na mambo mengi nahisi yanakanganya sana na hii ni kuokana na mifumo ya utawala ya nchi yetu.

Sisi tumetoka ktk mfumo wa kijamaa ambapo kuna mambo yalihitajika kuamriwa kijamaa, vilevile kuna mambo kutokana na jinsi tulivyokua tumejengwa kiupendo kati yetu tuliweza jua sote ni wa tanzania twapaswa kujaliana kwani tunajenga nchi yetu.

Mabadiliko hayakwepeki, yamekuja tumeyapokea, kutoka kule kwenye ujamaa wetu na kujaliana kama wa Tanzania na kuingia kwenye ubepari. Tupo humo sasa. Ni mazingira tofauti sana lakini hatuna budi kuyakubali kwani ndiyo hivyo mwenye nacho huongezewa na wewe ambaye huna ni ngazi zuri kwa huyu mwenye nacho.

Sote tunajua maisha bora ni NYUMBA, sekta hii asilimia 90% ni binafsi toka ile sera ya hawa tunaoamini watatufikisha tunakotaka kwenda ya kuuza nyumba za serikali na sekta hiyo kufikia kiasi hicho.

Ktk Hili la nyumba tunazopanga hivi kuna SHERIA YOYOTE INAYOMDHIBITI HUYU MWENYE NYUMBA BINAFSI KTK KUMSIMAMIA HUYU ASIYEKUWA NA UWEZO WA KUJENGA SASA HIVI, HUSUSANI KTK UPANGAJI KODI ZA HIZI NYUMBA TUNAZOPANGA SASA HIVI. KWANI KODI HUPANGWA KIHOLELA NA MWENYE NYUMBA PASI NA KIFUNGU CHOCHOTE KINACHOONYESHA KUMSIMAMIA HUYU MPANGAJI.

Naomba mnisaidie hili kama kuna anayejua kuna sheria ya upangaji nyumba usimamizi wa mkataba kati ya mwenye nyumba na mpangaji, vilevile kama kuna mamlaka au wakala ya kiserikali inayoshulikia hili hususani kwenye upangaji bei za hizi nyumba tunazopanga kwa maendeleo yetu na umoja wa taifa letu. Naomba msaada wako ewe mwanajamii.

Nakumbuka zamani kulikuwa na Rent restriction Act iliyokuwa inasimamia masuala ya pango za nyumba na proceeds therefrom. Kwa soko huria sasa, nadhani hakuna sheria inayosimamia kodi za pango za nyumba hususan za binafsi. Give time will let you know
 
Back
Top Bottom