Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,329
- 6,447
Makamu wa Rais, Dr. Ghalib Bilal
Wakati akiongea kwenye maazimisho/ sherehe/ sala ya Idd El Hajj ya kitaifa kwenye Msikiti wa Simbambali uliopo wilaya ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam tarehe 17/11/2010, alitoa ahadi kwa umma wa waislamu ya kushughulikia kwa kuanzishwa kwa mahama ya kadhi Tanzania Bara (Mwananchi/ Majira/Mtanzania, 18/11/2010)
Katiba inasema:
Ibara ya 3
(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa
Ibara ya 6
...neno ‘serikali' maana yake ni ... na pia mtu anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya serikali yoyote
Ibara ya 19
(2) kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi
(4) kila palipotajwa neon ‘dini' katika ibara hii ifahamike kwamba maana yake in pamoja na madhehebu ya dini, na maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neon hilo nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo
Ibara ya 20
(2) ...haitakuwa halali kwa chama chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na katiba au sera yake:
(a) Kukusudia kukuza au kupigania maslahi ya:
(i) Imani au kundi lolote la dini
Ibara ya 26
(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii katiba hii na sheria za Jamhuri ya Muungano
[Maswali ya Msingi: Katiba kama isemavyo na ahadi ya Makamu wa Rais kwa Umma wa Waislamu kwa niaba ya serikali ya CCM na Chama cha Mapinduzi sio kuvunja katiba huko? Huyu Kiongozi si amevunja katiba ndani ya kama wiki mbili baada ya kushika madaraka na kuapa kuilinda, kuitetea na kuhifadhi katiba hii, je baada ya miaka miwili itakuaje? Je, serikali ya CCM na Chama Cha Mapinduzi au mamlaka ya nchi ina dini?]
Wakati akiongea kwenye maazimisho/ sherehe/ sala ya Idd El Hajj ya kitaifa kwenye Msikiti wa Simbambali uliopo wilaya ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam tarehe 17/11/2010, alitoa ahadi kwa umma wa waislamu ya kushughulikia kwa kuanzishwa kwa mahama ya kadhi Tanzania Bara (Mwananchi/ Majira/Mtanzania, 18/11/2010)
Katiba inasema:
Ibara ya 3
(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa
Ibara ya 6
...neno ‘serikali' maana yake ni ... na pia mtu anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya serikali yoyote
Ibara ya 19
(2) kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi
(4) kila palipotajwa neon ‘dini' katika ibara hii ifahamike kwamba maana yake in pamoja na madhehebu ya dini, na maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neon hilo nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo
Ibara ya 20
(2) ...haitakuwa halali kwa chama chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na katiba au sera yake:
(a) Kukusudia kukuza au kupigania maslahi ya:
(i) Imani au kundi lolote la dini
Ibara ya 26
(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii katiba hii na sheria za Jamhuri ya Muungano
[Maswali ya Msingi: Katiba kama isemavyo na ahadi ya Makamu wa Rais kwa Umma wa Waislamu kwa niaba ya serikali ya CCM na Chama cha Mapinduzi sio kuvunja katiba huko? Huyu Kiongozi si amevunja katiba ndani ya kama wiki mbili baada ya kushika madaraka na kuapa kuilinda, kuitetea na kuhifadhi katiba hii, je baada ya miaka miwili itakuaje? Je, serikali ya CCM na Chama Cha Mapinduzi au mamlaka ya nchi ina dini?]