WanaJF leo saa 2 usiku kwenye taarifa ya habari TBC1 nimeshangazwa na Mbunge mmoja viti maalum alipokua shuhuda wa tukio la Mbunge wa viti maalum aliyeugua ghafla bungeni mapema leo asbh!!! Shuhuda huyo alipoulizwa akadai walikua wamekaa karibu mule bungeni wakawa wanaongea mambo yao ya nyumbani ghafla mwenzie akaishiwa nguvu na kuanguka!! Wakati tukio hili linatokea ilikua ndani ya bunge na kikao kinaendelea lkn waheshimiwa hawa walikua wanaendelea na mambo yao tena ya nyumbani kwao mpaka ugonjwa ulivyowaumbua!!! Swali langu ni kwamba ina maana wabunge viti maalum hasa wa Chama Cha Magamba (CCM) hawana mchango wowote bungeni!?