Jamani bongo ulaya! mpo?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Watu wamiminika Shoprite kununua mkate Sh 340
Mwandishi Wetu
Daily News; Monday,May 19, 2008 @00:03


WATU wengi wamekuwa wakimiminika katika maduka makubwa ya Shoprite Dar es Salaam kununua mikate inayouzwa kwa bei nafuu ya Sh 340 wakati sehemu nyingine inauzwa hadi Sh 900.

Katika kipindi cha wiki moja iliyopita, HabariLeo imekuwa ikishuhudia wateja wengi wakimiminika kwenye maduka hayo na kupanga foleni kwenye kaunta ya mikate kujipatia mikate hiyo.

Baadhi ya wateja waliohojiwa katika maduka hayo, walisema wanakimbilia kununua mikate kwenye maduka hayo kwa sababu ni bei nafuu na inakuwa bado ya moto. Maduka hayo hutengeneza mikate yake papo hapo.

“Naipenda mikate hii kwa sababu ni bei nafuu, lakini pia tunaipata ikiwa ya moto, mtaani wakati mwingine wanatuuzia mikate ya juzi,” alisema Juma Kisoki ambaye alikuwa katika duka la eneo la Kamata. Kisoki ni Meneja Masoko wa kampuni ya DCD Dar es Salaam.

Hassan Said ambaye alisema ni mteja wa muda mrefu wa mikate hiyo, alisema kinachomfanya anunue ni ubora wa mikate hiyo kwa sababu inapikwa vizuri na inaweza kukaa muda mrefu bila kuharibika.

Wakati bei ya mikate katika maduka ya Shoprite ni nafuu, bei katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam ni kubwa maradufu ya ile inayouzwa na maduka ya Shoprite.

Katika maeneo mengi ya jiji mkate unauzwa kati ya Sh 600 na Sh 900 kitu ambacho kimesababisha wengine kuacha kuitumia na badala yake wanatumia maandazi na vitafunwa vingine kwa ajili ya kifungua kinywa.

Katika duka la City Supermarket lililopo Mtaa wa Samora, bei ya mkate ambao ni wa ukubwa sawa na ule wa Shoprite ni Sh 700 na mikate mikubwa Sh 900. Nao wanatengeneza wenyewe papo hapo dukani.

Katika duka la Pamba House Supermarket ambalo lipo Mtaa wa Garden ni Sh 800 kwa mkate mmoja wa ujazo wa kawaida na mikate mikubwa ni Sh 1,100 wakati Shoprite mkate mkubwa ni Sh 550 tu.

Hata hivyo, unafuu wa bei ya mikate kwenye maduka ya Shoprite umezua maswali mengi kutokana na bei ya mikate katika maduka mengine ni zaidi ya mara mbili ya hiyo.

Maswali hayo yanatokana na hisia kwamba huenda wauzaji wengine wa mikate wanawaibia wananchi au kuna tatizo la biashara ambalo linasababisha wauze bei juu.

Juhudi za kumpata Meneja Mkuu, Fredrick Skein wa Shoprite kueleza unafuu wa bei hiyo hazikuzaa matunda, lakini HabariLeo ilizungumza na Meneja Masoko Mathew Kaubo ambaye alisema yeye hana ruhusa ya kuzungumza na waandishi hadi apewe kibali cha kuzungumza.
 
Mwanakijiji nadhani hili ni tangazo la biashara, tufanye utaratibu wa malipo kidogo kwa matangazo kama haya! Au?
 
loh dis technique is quite impressive esp if forum hii yatembelewa na wa tz wengi walioko bongo..as ni tangazo la biashara toshaaa!

on the other hand nimepata mshtuko kidooogo as wakati naondoka bongo kama sikosei mwaka unusu nyuma mkate was just 250 tshs now mwaniambia mingini ni hadi 700 kwa mia 9??
 
ni kweli kabisa, nilishaque hapo madakika kadhaa kisa mkate! na utaona watu wengi wanamiminika shoprite mida ya jioni ukadhani kuwa duka hilo lina wateja wengi sana lkn majority hufuata mikate! kazi kwao bakery zingine.

Lakini 'heading' ya kuwa bongo ni ulaya haiendani na haya maelezo!
 
Je Ubora Wa Mikate Hiyo Ipo Sawa Manake Isije Ikawa Bei Poa Na Kiwango Chake Powa Tena


sijui viwango vya mikate lakini nikilinganisha na mikate mingine niliyonunua hapo dar, ambayo mingine inakuwa imeshaanza kuota fungi, ninaopt kwa mikate fresh from the oven hapo shoprite
 
sijui viwango vya mikate lakini nikilinganisha na mikate mingine niliyonunua hapo dar, ambayo mingine inakuwa imeshaanza kuota fungi, ninaopt kwa mikate fresh from the oven hapo shoprite
GOOD MANAKE HAWA JAMAA KUKU WAKISHINDIKANA SOUTH WANAWALETA BONGO NA KUPGA SALE BASI WATU WANAMIMINIKA MADUKANI.WATU HAWA ISHI KUHALISHA.
 
Watu wamiminika Shoprite kununua mkate Sh 340
Mwandishi Wetu
Daily News; Monday,May 19, 2008 @00:03


WATU wengi wamekuwa wakimiminika katika maduka makubwa ya Shoprite Dar es Salaam kununua mikate inayouzwa kwa bei nafuu ya Sh 340 wakati sehemu nyingine inauzwa hadi Sh 900.

Katika kipindi cha wiki moja iliyopita, HabariLeo imekuwa ikishuhudia wateja wengi wakimiminika kwenye maduka hayo na kupanga foleni kwenye kaunta ya mikate kujipatia mikate hiyo.

Baadhi ya wateja waliohojiwa katika maduka hayo, walisema wanakimbilia kununua mikate kwenye maduka hayo kwa sababu ni bei nafuu na inakuwa bado ya moto. Maduka hayo hutengeneza mikate yake papo hapo.

"Naipenda mikate hii kwa sababu ni bei nafuu, lakini pia tunaipata ikiwa ya moto, mtaani wakati mwingine wanatuuzia mikate ya juzi," alisema Juma Kisoki ambaye alikuwa katika duka la eneo la Kamata. Kisoki ni Meneja Masoko wa kampuni ya DCD Dar es Salaam.

Hassan Said ambaye alisema ni mteja wa muda mrefu wa mikate hiyo, alisema kinachomfanya anunue ni ubora wa mikate hiyo kwa sababu inapikwa vizuri na inaweza kukaa muda mrefu bila kuharibika.

Wakati bei ya mikate katika maduka ya Shoprite ni nafuu, bei katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam ni kubwa maradufu ya ile inayouzwa na maduka ya Shoprite.

Katika maeneo mengi ya jiji mkate unauzwa kati ya Sh 600 na Sh 900 kitu ambacho kimesababisha wengine kuacha kuitumia na badala yake wanatumia maandazi na vitafunwa vingine kwa ajili ya kifungua kinywa.

Katika duka la City Supermarket lililopo Mtaa wa Samora, bei ya mkate ambao ni wa ukubwa sawa na ule wa Shoprite ni Sh 700 na mikate mikubwa Sh 900. Nao wanatengeneza wenyewe papo hapo dukani.

Katika duka la Pamba House Supermarket ambalo lipo Mtaa wa Garden ni Sh 800 kwa mkate mmoja wa ujazo wa kawaida na mikate mikubwa ni Sh 1,100 wakati Shoprite mkate mkubwa ni Sh 550 tu.

Hata hivyo, unafuu wa bei ya mikate kwenye maduka ya Shoprite umezua maswali mengi kutokana na bei ya mikate katika maduka mengine ni zaidi ya mara mbili ya hiyo.

Maswali hayo yanatokana na hisia kwamba huenda wauzaji wengine wa mikate wanawaibia wananchi au kuna tatizo la biashara ambalo linasababisha wauze bei juu.

Juhudi za kumpata Meneja Mkuu, Fredrick Skein wa Shoprite kueleza unafuu wa bei hiyo hazikuzaa matunda, lakini HabariLeo ilizungumza na Meneja Masoko Mathew Kaubo ambaye alisema yeye hana ruhusa ya kuzungumza na waandishi hadi apewe kibali cha kuzungumza.

VYA BEI POA NI GHARI SANA SANA
HIYO NGANO YA KUTENGENEZA MIKATE NI YA MWAKA 1955 KWA HIYO UTAONA WATU WATAKAVYOKUWA NA UTINDIO WA UBONGO, KISA MIKATE BEI POA. JIULIZE KWANZA KABLA YA KUNUNUA. KAMA NI BREAKFAST TUMIA MIHOGO, NDIZI, VIAZI NA NGANO YA HAPO NYUMBANI. HIYO NGANO YA KUTOKA INDIA NA SOUTH AFRICA ILIYOKWISHA MUDA WAKE, MTAKUWA VICHAA, NA CCM HAPO NDO WANAPENDA MAANA WENGI WATAKUWA MAZEZETA. UNAJUA JINSI MOHAMED ENTERPRISES ALIVYOUA MKEMIA MKUU WA TANZANIA NA BAADHI YA WAKEMIA, KISA MREMA KACHOMA NGANO ILIYOKUWA IUZWE KWA WATU. KWA HIYO MIKATE JARIBU KUULIZA UNGA WA NGANO NI WA MWAKA GANI? LA SIVYO WENGI WATAENDELEA KUWA MAZEZETA, NDIYO NDIYO NDIYO CCM MPAKA UNAKUFA MAANA UBONGO UMESHAOZA KWA HIYO MIKATE YA BEI NAFUU.
 
WANANDUGU HAWA JAMAA WA SUPERMARKET NI WA KUANGALIA SASA KWA INFO TU NA ZA UHAKIKA NAWAPA HII.......ILA NAPENDA KUELEZA HAP[A TATIZO NI KWA WATANZANIA TUNAUANA WENYE KWA WENYEWE.........

SUPERMARKET NYINGI HIVI SASA ZINACHUKUA MATUNDA TOKA NJE MENGI NI KUTOKA KWA NDUGU ZETU WA SOUTH....KUNA MATUNDA YANAFUNGWA MAENEO YA BARABARA YA KUTOKA MJINI KWENDA UBUNGO NA UKITOKA UBUNGO KWQENDA BUGURUNI
VIJANA WAMEKUUWA WAKIUZA MIKONONI MFUKO YAKO MATANO MATANO
WANANDUGU YALE YAMETUPWA NA HAWA NDUGU ZETU SUPERMARKET NA WATANZANIA KUAMUA KUWFUNGIA WENZAO KUONYESHA KWAMBA SISI HAKUNA KITU KINACHO EXPIRE HUKU BONGO KWA HIYO HIYO MIKATE NAYO MMHhhhhhhhhhhhh???????????!!!!1111111 kunani tuwaulize wanatumia nini tofauti..maana ukija angalia utaona hii sehemu serikali waanze kuwafawatilia viwanda vya mikate wanapata faida sana kama ni kweli hatulishwi vilivyo expire...kama wanavyosema wanaunda tume kwa ajili ya mafuta kuchunguza uletaji wake na faida yake waangali na hivi viwanda ...nahisi huu ndio wakati wa TBS kwenda pale supermarket kucheck ubora wa hiyo mikate waje JF KUTUJULISHA nasi tuunde tume yetu ya kupunguza umasikini tanzania.....
 
Watu wamiminika Shoprite kununua mkate Sh 340
Mwandishi Wetu
Daily News; Monday,May 19, 2008 @00:03


WATU wengi wamekuwa wakimiminika katika maduka makubwa ya Shoprite Dar es Salaam kununua mikate inayouzwa kwa bei nafuu ya Sh 340 wakati sehemu nyingine inauzwa hadi Sh 900.



Bei sasa ni Tsh 500 badala ya 340
This could just be a marketing strategy


.
 
Back
Top Bottom