Jamaa yangu anatakiwa kuondolewa jicho kesho. Jicho mpaka litolewa linatakiwa liwe katika hali gani?

Ziroseventytwo

JF-Expert Member
Mar 27, 2011
7,971
13,605
Kuna jamaa ya yangu anatarajiwa kuingi theater kesho kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji utakao ondoa jicho lake 1. Nimeumia sana. Atafanyiwa upasuaji kesho kwenye hospitali ya mt Fransis hapa ifakara. Madaktari wamemweleza kuwa jicho lake limekufa.

Jamaa aliumia kama siku 10 zilizopita baada ya kukwaruzwa na kijiti kwenye shughuli zake za kivuvi. Kilichonifanya niilete hii thread hapa ni muda na aina ya tiba aliyopewa. Kwa maelezo ya mgonjwa alipewa dawa ya kuweka kwenye jicho ya matone. Na dawa ya kupunguza maumivu. Jana hali yake ikabadilika akidai kuwa anasikia maumivu makali. Leo hii kaja haspitalini hapa na madoctor wamemwambia kuwa jicho limekufa na linatakiwa litolewe.

Sina uhakika kama hii hospitali ina vipimo vizuri kwa ajili ya macho.

Jicho mpaka litolewa linatakiwa liwe katika hali gani.? Nina mpango wa kwenda kumshauri akatae maana muda na aina ya tiba alizopata kwa maana ya dawa si nzuri.
 
Pole sana.

Kuna ulazima gani wa kuharakisha? Anaweza kupimwa na wataalamu zaidi kuangalia kama anaweza kusaidiwa asitoe jicho?
Huo uharaka ndio siuelewi kabisa. Hata kama mgonjwa ana maumivu makali si wampe madawa ya usingizi na ya maumivu? Mimi nina wasiwasi jamaa anaweza kupoteza jicho wakati kulikuwa na otanative nyingine.

Naumia roho sana.
 
Huo uharaka ndio siuelewi kabisa. Hata kama mgonjwa ana maumivu makali si wampe madawa ya usingizi na ya maumivu? Mimi nina wasiwasi jamaa anaweza kupoteza jicho wakati kulikuwa na otanative nyingine.

Naumia roho sana.
Kamaunawezakushauri waahirishe wakati anatafuta ushauri zaidi fanya hivyo.

Anaweza kutolewa jichokesho, halafu baada ya wiki mkagundua jicho lingeweza kutibiwa vizuri tu.
 
Haoo jamaa walikosea toka mwanzooo... itakuwa jamaa jicho liloharibika sanaa afuu waoo wakachukulia kirahisi tuu so now limeharibika kabisa... Lakini aende hospital nyingne kama bado anaona hata kwa mbalii...
 
Haoo jamaa walikosea toka mwanzooo... itakuwa jamaa jicho liloharibika sanaa afuu waoo wakachukulia kirahisi tuu so now limeharibika kabisa... Lakini aende hospital nyingne kama bado anaona hata kwa mbalii...
Nimetoka kumwona muda c mrefu. Jicho limevimba sana na kwa maelezo ya mgonjwa jicho limepoteza uwezo wa kuona. Nimeangalia vyeti madaktari wameandika jicho limepoteza uwezo wa kuona. So kesho saa 3 asubuhi anaingia chumba cha upasuaji kwa ajili ya upasuaji.
 
Nimetoka kumwona muda c mrefu. Jicho limevimba sana na kwa maelezo ya mgonjwa jicho limepoteza uwezo wa kuona. Nimeangalia vyeti madaktari wameandika jicho limepoteza uwezo wa kuona. So kesho saa 3 asubuhi anaingia chumba cha upasuaji kwa ajili ya upasuaji.

Poleni sana..so sad
 
jicho likiwa katika hali ambayo uwepo wake utazidi kusababisha madhara kwa sehemu nyingine za mwili ni kuliondoa tu, , unakuta jicho kadri siku zinavyozidi kwenda linazidi kuharibika mwisho wa siku litaambukiza hata maeneo mengine, hivyo ni kuliwahi.
pole sana.
 
Angeanzia hospitali baada ya kupata hiyo shida labda hata asingefikia huko..ni jambo la kushangaza kuumia jicho(physical injury) alaf ukaweka matone..anywy..kamajicho limepata maambukizi lazima litolewe..pole sn mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom