mnyongeni
Senior Member
- Dec 6, 2011
- 141
- 24
Hili swala la jk kukumbatia mawaziri mafisadi, ana upendo na wananchi kweli? pinda si ameshindwa kuwawajibisha, eti kisa hana mamlaka(amezibwa mdomo), sasa wabunge hongereni kwa kazi nzuri, ila hatutaki mje muwashitaki kwetu, kwani hili limeshatendeka, si mlishawashitaki mlipokuwa bungeni? tumechoka tumechoka tumechoookaaa..wito wangu kwako jakaya mrisho kikwete, sasa yatosha, we siunatuona sie mambumbumbu wa kusukumwa na upepo, ndomana unasema "HUU NI UPEPO TU UTAPITA" sasa fahamu ni upepo ndiyo; ila UTAPITA NA WEWE. WITO WANGU KWA WANANCHI:Naomba tulishikilie hili swala kama hatowawajibisha mawaziri wake tumshinikize mpaka ajiuzulu. tangazeni, hamasisheni tumieni mitandao ya kijamii ili swala hili lifanikiwe, siye si ndo tulimweka madarakani sasa tunauwezo wa kumwondoa. na ataondoka. nategemea ushirikiano wako.