Shujaa Mwendazake
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 3,735
- 6,291
Hapo awali nilishuhudia mkutano kati ya Bwana huyu na Balozi wa Marekani, ukiachilia mambo mengi anayoalikwa huko nje. Nachelea kusema kuwa sehemu kubwa ya Diplomasia ya nchi yetu inamuweka JK kama alama muhimu ya taifa letu huko Duniani. Bwana fulani alitaka kumzima huyu lakini inaonekana ana nyota kali ama anakubalika sana na mataifa mengine huko nje.
Inaonekana Madam President ni kama vile anamtumia JK katika kufungua mpaka iliyokwishafungwa na Hayati kaka. Hii ni kwa sababu Mama naye alikuwa namba 2 kwenye utawala wa Kaka ndo maana bado mataifa mengi yana mashaka naye.
Ni Mkwere pekee anayeweza kuifanya kazi ya kuwaaminisha kuwa mambo yamebadilika, na anaiifanya kwelikweli. Hapo Zambia hajaenda bure, you can imagine atakutana na viongozi na wafanyabiashara wangapi atakaowakaribisha kujenga uhusiano na nchi yetu.