Mbogela
JF-Expert Member
- Jan 28, 2008
- 1,384
- 257
Mh. JK amekuwa na bahati ya kutunikiwa shahada za juu za PhD kuwazidi maraisi wengine wa JMT waliomtangulia. Mwl. JK alipewa shahada kama hiyo na chuo kikuu cha kilimo Sokoine kwa mchango wake katika Rural development.
Akipokea hiyo shahada mwalimu alisema ameipokea kwasababu 2. Moja kutambua umuhimu wa mkakati maendeleo vijijini na pia kwa sababu ya heshima ya Edward Sokoine ambaye chuo hicho kimepewa jina kwa heshima yake.
Mpaka sasa Jakaya Kikwete ameshawazidi Ben na Ali katika kujinyakulia hizo shahada. Sijajua vigezo vinavyotumika kumtunuku shahada zote hizo. Lakini nadhani kama wasomi wote hao wametambua mchango wa Jakaya katika ustawi wa nchi hii na Afrika kwa ujumla.
Mwaka 2009 na 2010 nishani ya Mo ilikosa mshindi, kama kweli wakuu wa vyuo vyetu wametoa hizo shahada kwa vigezo stahiki, je, tutegemee JK kuwa mshindi wa nishani ya Mo mwaka 2016?
Akipokea hiyo shahada mwalimu alisema ameipokea kwasababu 2. Moja kutambua umuhimu wa mkakati maendeleo vijijini na pia kwa sababu ya heshima ya Edward Sokoine ambaye chuo hicho kimepewa jina kwa heshima yake.
Mpaka sasa Jakaya Kikwete ameshawazidi Ben na Ali katika kujinyakulia hizo shahada. Sijajua vigezo vinavyotumika kumtunuku shahada zote hizo. Lakini nadhani kama wasomi wote hao wametambua mchango wa Jakaya katika ustawi wa nchi hii na Afrika kwa ujumla.
Mwaka 2009 na 2010 nishani ya Mo ilikosa mshindi, kama kweli wakuu wa vyuo vyetu wametoa hizo shahada kwa vigezo stahiki, je, tutegemee JK kuwa mshindi wa nishani ya Mo mwaka 2016?