JOESKY
JF-Expert Member
- Mar 25, 2015
- 816
- 2,032
Wasaalam ndugu wana jamvi!!
Nimefikiri kwa marefu na mapana bila kupata majibu ya baadhi ya maswali yahusuyo utawala wa Dr Jakaya Kikwete enzi za utawala wake. Ni miaka kadhaa imepita sasa toka mzee wetu arudi kijijini kwao Msoga kuendelea na maisha yake ya kawaida baada ya kumaliza muda wake wa kuongoza.
Kuna vitu vingi na vikubwa mno vilifanyika enzi za Jakaya Kikwete lakini havikuzuia mambo mengine kwenda sawa bin sawia.
Kuna nyakati mambo yalikuwa yanakwama lakini yanatatulika ndani ya muda mfupi mambo yalikuwa yanakaa sawa.
Mfano wa vitu ambavyo alivimudu Jk pasi na kuteteleka ni pamoja na:
- Nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma kila ufikapo mwaka mpya wa bajeti
- Ajira za uhakika pasi na urasimu
- Miundo mbinu ya barabara
- Ujenzi wa madarasa na shule za kata
- Ujenzi wa zahanati na hospitali
- Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
- Uwekezaji wa pesa kwenye tafiti mbali mbali zihusuzo mambo ya Uchumi kwa ujumla
- Vikao na semanars kwa maafisa wa idara mbalimbali(hawa wote walipata posho zao bila bughuza?)
*NA MENGINE MENGI.
Lakini nchi ilienda na Mzunguko wa pesa mtaani ulikuwa mkubwa biashara zilikuwa zinakua kila uchao kukaongeza wimbi la wafanyabiashara na wawekezaji wa nje na ndani ya mipaka ya nchi yetu. Mashirika na makampuni yalinawiri kwa utajiri na yalitoa ajira kwa ukubwa usio kifani.
Sasa swali langu kwa awamu hii pamoja na kubana matumizi na uzibaji wa mianya ya Rushwa kwa ukali wa hali ya juu ni nini kinachofanya tusione matunda ya huo mfumo? kama mishahara ya watumishi imebaki constant bila kuongezwa tokea JK aondoke???_Suala la ajira lipo wazi sitaki hata kuligusia kwa kifupi hakuna ajira za uhakika awamu hii lakini bado kunaonekana kuna uhaba na umasikini mkubwa kwa taifa na mtu mmoja mmoja??
Nawakaribisha mezani tutete!!
Nimefikiri kwa marefu na mapana bila kupata majibu ya baadhi ya maswali yahusuyo utawala wa Dr Jakaya Kikwete enzi za utawala wake. Ni miaka kadhaa imepita sasa toka mzee wetu arudi kijijini kwao Msoga kuendelea na maisha yake ya kawaida baada ya kumaliza muda wake wa kuongoza.
Kuna vitu vingi na vikubwa mno vilifanyika enzi za Jakaya Kikwete lakini havikuzuia mambo mengine kwenda sawa bin sawia.
Kuna nyakati mambo yalikuwa yanakwama lakini yanatatulika ndani ya muda mfupi mambo yalikuwa yanakaa sawa.
Mfano wa vitu ambavyo alivimudu Jk pasi na kuteteleka ni pamoja na:
- Nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma kila ufikapo mwaka mpya wa bajeti
- Ajira za uhakika pasi na urasimu
- Miundo mbinu ya barabara
- Ujenzi wa madarasa na shule za kata
- Ujenzi wa zahanati na hospitali
- Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
- Uwekezaji wa pesa kwenye tafiti mbali mbali zihusuzo mambo ya Uchumi kwa ujumla
- Vikao na semanars kwa maafisa wa idara mbalimbali(hawa wote walipata posho zao bila bughuza?)
*NA MENGINE MENGI.
Lakini nchi ilienda na Mzunguko wa pesa mtaani ulikuwa mkubwa biashara zilikuwa zinakua kila uchao kukaongeza wimbi la wafanyabiashara na wawekezaji wa nje na ndani ya mipaka ya nchi yetu. Mashirika na makampuni yalinawiri kwa utajiri na yalitoa ajira kwa ukubwa usio kifani.
Sasa swali langu kwa awamu hii pamoja na kubana matumizi na uzibaji wa mianya ya Rushwa kwa ukali wa hali ya juu ni nini kinachofanya tusione matunda ya huo mfumo? kama mishahara ya watumishi imebaki constant bila kuongezwa tokea JK aondoke???_Suala la ajira lipo wazi sitaki hata kuligusia kwa kifupi hakuna ajira za uhakika awamu hii lakini bado kunaonekana kuna uhaba na umasikini mkubwa kwa taifa na mtu mmoja mmoja??
Nawakaribisha mezani tutete!!