Jaji Warioba: Tanzania imepiga hatua, lakini bado tuna matatizo makubwa

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema tangu Uhuru, Tanzania imepiga hatua kubwa mpaka kuingia Uchumi wa Kati lakini bado yapo matatizo hasa katika eneo la umasikini.

Akizungumza katika Mdahalo wa Kumbukizi ya Kitaifa ya Hayati Edward Sokoine uliofanyika Viwanja vya SUA Morogoro, Jaji Warioba amesema Watanzania walio wengi bado ni masikini.

Aidha, amesema Rais Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango wamefanya Watanzania waamini Taifa lipo salama

 
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema tangu Uhuru, Tanzania imepiga hatua kubwa mpaka kuingia Uchumi wa Kati lakini bado yapo matatizo hasa katika eneo la umasikini
Aidha, amesema Rais Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango wamefanya Watanzania waamini Taifa lipo salama
1622113350002.png
 
Midahalo imerudi kwa kasi sana nchini

Kweli kama asemavyo Mhenga Mstaafu

'Heri hupatikana ndani ya tumbo la shari'

Pamoja athari kadhaa mbaya za Corona. Demokrasia na uhuru wa kujieleza umerejea
 
Huu uchumi Wa kati tumesukumiziwa tu ila kiuhalisia si kweli bali ulikua no mtego tu!
 
Huu uchumi Wa kati tumesukumiziwa tu ila kiuhalisia si kweli bali ulikua no mtego tu!
Watu mntaka tuendelee kuwa tegemezi, mnataka tuendelee kubaki kwenye rika la umasikini ipi tuonewe huruma. Simama, TUJITEGEMEE ki kweli kweli kama nchi.
 
Back
Top Bottom