Jaji Warioba na Pro.Shivji wabishana kuhusu Bunge la Katiba

Mtambue kuwa Warioba ni kada wa ccm. Sidhani kama anaweza kuwa fair kama baadhi ya watu wanavyofikiri. Cheo alichopewa na rais wa chama chake lazima kiambatane na yeye kulipa fadhila (kufuata matakwa ya waliompa hayo madaraka).
 
Ukweli husemwa:

Sija bahatika kuyasoma hayo majibizano na tofauti ya mitizamo yao kwenye gazeti, lakini kwa yale uliyoyaandika na maoni yako, inaonekana hujamtendea haki Jaji Warioba.

Tatizo letu Watanzania, pale tunapomuona mtu anasema mambo mengi tunayoafikiana nayo kimaslahi au kiitikadi, basi hata yale mengine atakayoyasema ambayo ni pumba tunayaona ni mchele. Tumejengeka tabia ambayo pale tunapomwamini mtu fulani, basi tunakuwa kama vipofu wa fikra kwa kile akifanyacho.


Tunatakiwa tujenge tabia ya kujongea kila jambo kwa walakini ili tuweze kubainisha kwa undani sababu zilizoko nyuma ya kila jambo kabla ya kulikubali.


Kama Jaji Warioba alivyosema, 'Utawapata wapi watu ( wajumbe wa Bunge la Katiba) ambao hawana maslahi na suala zito kama katiba ya nchi'.

Pro Shivji anasema haya kwa vile labda ana motive behind lakini vilevile kauli zake nyingi zinaonyesha kama anajaribu kuidhalau tume ya katiba.



Kumbuka wabunge ni wawakilishi wa wananchi ambao wanachaguliwa na wavua samaki, wakulima na wafanyakazi. Kwa mantiki na mchanganuo huo, lazima tu watakuwa ni wengi.


Tatizo kubwa ambalo Watanzania linatusumbua katika mchakato mzima wa katiba ni kutanguliza maslahi ya kiitikadi kwanza badala ya uzalendo.


Hatutaki kujifunza kutokana na makosa mengi ambayo tumechangia kuifikisha nchi hapa ilipo.


Hebu tujaribu kuwa wazalendo kwa hili.

Mkuu mbona tuko pamoja ila unapindisha kidogo hapo kwenye red.
Mosi, Wewe Hujamtendea haki prof Shivji kwa kusema tu ana motive behind bila kuitaja. Itaje. La sivyo, tunabaki kuwa ktk hili Prof Issa Shivji alikuwa sahihi.
Pili, mimi nimemtendea haki kwa sababu yote niliyoyaeleza ndo aliyoyasema yeye. Labda kama gazeti limemnukuu vibaya - raia mwema wako makini.
Tatu, kwa hiyo, kwa kuwa wabunge ni wawakilishi wa wakulima, wavua samaki na wafanyakazi wanapaswa wawe wengi? kwa maoni yangu Hapana. Kama jibu ndiyo, basi tungewaachia jukumu lote wenyewe kama tulivyowaachia jukumu la kutunga sheria. Kwenye katiba hata wabunge kundi maslahi kwa sababu nao zao (product) yakatiba. Kwa hiyo, ni kosa kubwa wabunge kuwa wengi kuliko wafanyakazi na wakulima ndani ya Bunge la katiba.
 
Sioni ubaya wa scholars kutofautiana, na mijadala kama hii ndio inayojenga. Scholars differ and that's healthy as long as there is no abuse and it's for the better of the country.
 
Tunapozungumzia system ni chama tawala hata tufanyeje katiba itakayotoka itakuwa na muegemeo wa serikali sio wa wananchi. Ningetamani mkiti wa tume ya katiba atoke un hapo ndio tungepata maoni ambayo ni balanced. Sijui wamarekani walifanyaje lakini walito kitu kinachokubalika daima nchini kwao. Ni jambo gumu sana kuoanisha maoni yote utoke na kitu balanced kama wewe si mzalendo wa kweli. Kwa wanaofaidi nchi hii maoni yao yatakuwa tofauti na walalahoi na mkiti na tume yake wanatakiwa wa -balance ndio wapeleke bunge la katiba.
 
Topic kama hizi zina mitazamo tofauti sana kwa kila mtu na jinsi anavyoona mambo kwa uelewa wake. Kila mtu hapa, either Jaji Warioba au Prof. Shivji wako sahihi kabisa kwa mitizamo yao juu ya jambo hili la bunge la katiba.

Hakika nakuambia Mikael P Aweda, Warioba ana amini kabisa, hakuna tatizo lolote kwa bunge la sasa kuwa bunge la katiba kwa sababu anaamini (sijui kwa makusudi au ni kweli ana amini hivyo) kuwa wabunge wote, wakiwemo wa CCM wamechaguliwa kwa uhalali sana. Ingawaje nayeye pia, baada a uchaguzi wa 2010 alikuja na makala nyiingi za kukosoa mfumo wa uchaguzi Tanzania.

Prof. Shivji amekuwa msitari wa mbele sana kutetea hili suala la bunge la katiba kwa kuhakikisha tunapata katiba inayotokana na matakwa ya wananchi. Kwa mtazamo wake, na kwa mtazamo wa anti-CCM wengi, bunge la katiba lazima litokanane na kuchaguliwa kwa wananchi wenyewe!. Sasa hapa ndipo akina Warioba wanaona ugumu, ni nani atasimamia kuwachagua hao wabunge wa bunge la katiba kama Tume ya Uchanguzi iliyopo sasa siyo huru. Ni nani huyo, ni kundi gani hilio ambalo litasimamisa uchaguzi wa hawa wabunge? Je yeye hatakuwa biased, is not easy to be in a win win situation katika jambi hili.

Pia, mimi nina amini kuwa, Jaji Warioba, ana amini kabisa kuwa wabunge watakuwa wazalendo sana katika hili na kuweka u-chama pembeni, haki ya nani hapa ndipo pana kuwa pagumu, kwani LILA NA FILA HAWATANGAMANI!

Cha muhimu, ni kuwekwa makundi ya kutosha (kutoka katika nyanja zote) katika bunge la katiba, na ki ukweli hata kama CDM ndo ingekuwa imeshika dola, siyo rahisi hivo Mikael P Aweda kuacha mambo yande yenyewe kama unavofikiri, utashi wa kisiasa unatawala hata kwenye hiyo katiba, Katiba siyo Quran au Biblia, hata CDM ikishika dola inaweza kuja na move ya kuibadilisha, hili limetokea nchi nyingi tu.
 
Wakuu,
Nimesoma mabishano au tofauti ya mtizamo kati ya prof Issa Shivji na Jaji warioba ktk gazeti la Raia mwema la leo. Nimeshangazwa na msimamo wa Jaji Warioba ninayemheshimu sana, nitaeleza.

Kwa mujibu gazeti la Raia mwema la Leo wasomi hawa wawili wetofautiana juu ya wajumbe wa Bunge la Katiba.

Msimamo Shivji;
Akiwa katka Kongamano la Katiba Prof Shivji alisema;
Kuna kasoro kubwa ktk sheria ya kuendesha mchakato wa katiba mpya, hasa kuhusu uundaji muundo wa Bunge la katiba. Chombo muhimu sana kuliko hata Refrendum ( kura ya maoni) ni Bunge la katiba. Linapaswa kuwa Bunge la wananchi, vinginevyo uhalali wa hiyo Bunge utakuwa na Shaka. Ni Busara kwa wajumbe wa Bunge la Katiba kuchaguliwa moja kwa moja wa Wananchi kwa ajili ya kazi hiyo maalum tu.

Msimamo wa Jaji Warioba.
Hata hivyo, akizungumzia hilo Mkiti wa Tume ya Mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba alimweleza mwandishi wetu akihoji; Utawapata wapi watu ( wajumbe wa Bunge la Katiba) ambao hawana maslahi na suala zito kama katiba ya nchi? Aliendelea ingawa jambo hilo siyo sehemu ya hadidu rejea kwa tume hiyo lakini ni suala la kidemokrasia pia kuwaingiza wabunge na wawakilishi kuwa sehemu ya Bunge la Katiba. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi ni watu waliokabidhiwa pia jukumu la kutunga sheria.
Alipoulizwa kuhusu wingi wa wabunge wa ccm ktk bunge hilo na kwamba watalinda maslahi ya chama chao alijibu, wabunge hao wametokana na mfumo wa demokrasia yetu na ndio mtazamo wa wananchi.

My take;
Hivi jaji Warioba hajui kuwa tunacholalamikia ni wingi wa kundi moja - wabunge, ambao nao wana maslahi lakini hatutaki wao wawe wengi huku makundi mengine ya wavua samaki, wakulima na wafanya kazi wakikosa fursa hiyo?

2. Anaposema uwepo wabunge wengi wa ccm ni mtazamo wa wananchi, hajui kuwa moja ya sababu za kutungwa katiba mpya ni udhaifu wa Tume ya uchaguzi kutuletea viongozi wasiochaguliwa wakiwepo hao wa ccm wanaotuhumiwa kuchakachua kura wakisaidiwa na Tume.

NB, Nadhani jaji wangu ninayemheshimu ameteleza ktk hili kama hajavutwa na ushabiki wa kichama zaidi
.
ni vizuri pia prof shivji angeainisha hizo hela za kufanya uchaguzi wa nchi nzima zingetoka wapi. sio kuongea tu.let we be realistic
 
Sidhani kama ni sahihi sana kwa Jaji Warioba kudai kwamba composition ya bunge tulilo nalo sasa ambalo wabunge wengi ni wa ccm ndio mtazamo ama matakwa ya wananchi kwa sasa.

Sababu mojawapo ya kushinikiza uwepo wa katiba mpya ni pamoja na mapungufu makubwa yaliyopo katika katiba ya sasa ambayo kwa namna moja ama nyingine imepelekea wakati mwingine tume ya taifa ya uchaguzi kumtangaza mshindi ambaye si chaguo la wananchi. Tunayo mifano ya baadhi ya wabunge ambao hadi leo hii hawathubutu kukanyaga majimboni mwao, na kama wakienda wanafanya hivyo wakiwa na escort ya polisi, wengine wanakwenda kwa kificho na hawajawahi kufanya japo mkutano wa hadhara mmoja tangu watangazwe kuwa washindi.

Na kwa vyovyote vile uwingi wa wabunge wa ccm katika bunge la katiba ni wazi kwamba tutakwenda kuletewa katiba ya ccm na si katiba ya wananchi kama tulivyotarajia. Kwahiyo ni muhimu katika hali hiyo wananchi wenyewe tupewe nafasi/mamlaka ya kuchagua wabunge/wawakilishi wetu katika bunge la katiba. Inawezekana kabisa kumpigia kura (kumchagua) mbunge mwaka 201o lakini miaka miwili baadae yaani 2012 tunagundua kwamba hajakidhi matarajio yetu, hawakilishi matakwa yetu na tungekuwa na nafasi bila shaka tungeweza kumuweka pembeni kwahiyo hoja ya Jaji Warioba inakuwa haina mashiko sana.

Nakubaliana na hoja ya Jaji Warioba kwamba mojawapo ya kazi ya wabunge ni kutunga sheria lakini ni muhimu azingatie kwamba hii ni sheria ya kipekee, hii ni sheria mama, hii ndio nguzo/ mhimili wa sheria nyingine, na ndio maana haitungwi hovyo hovyo, ina utaratibu wake maalum na tofauti, na ndio sababu ikaundiwa tume maalum anayoingoza yeye kwa ajili ya kukusanya maoni ya wananchi kitu ambacho ni tofauti na utaratibu wa utungaji wa sheria nyingine.

Katika hili ninakubaliana moja kwa moja na mawazo ya Prof.Shivji kwamba wananchi wenyewe ndio wanatakiwa kuchagua wawkilishi wao kwa ajili ya bunge hili maalum la katiba. Jaji Warioba katika hili inabidi aachane kabisa na mambo ya kuweka uccm katika jambo hili muhimu kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu kwani katiba nzuri na inayotokana na matakwa ya wananchi wenyewe ndiyo itakayotuletea demokrasia pana na ya ukweli, lakini pia ndiyo itachagiza maendeleo ya nchi yetu kwa miaka mingine 100 au hata 200 ijayo.

Kimsingi warioba kajiweka ktk safe side,ni watu wanaoangalia haraka haraka ndio hawataangalia vyema sentense yake.Warrioba kasema kuwa hao wabunge ni matokea ya DEMOCRASIA ILOYOPO NCHINI, hajasema kuwa ni democrasia yetu ina viwango,ila pia ilipaswa iwe hivyo.Na wabunge waliopo hata kama wakiwa wengi ni wa CCM bado hadi sasa kuna ambao ubunge wao haujapingwa popote na hivyo kuwa wabunge halali kisheria.Sasa kuna vitu havipimwi kwa vigezo vya wazi kama uzalendo,na uelewa etc.Warioba hakuona sababu ya kupoteza muda vielezea.Kwa vyovyote hata waichaguliwa wawakilishi wengine kwa kura za wananchi bado zoezi linaweza lisilete matokeo tofauti au yakawa mabaya zaidi.Kwani makundi ya kimikakakti yatajituma sana tumia watu kufikisha malengo yao.Na mara hii panaweza kuwa na wawakilishi waliopikwa kuliko.

Nadhani tunahitaji jadili njia zote kwa uwazi na ukweli, na unyenyekevu, uzalendo na kutokuwa na ushabiki.
 
Mkuu,
Hujawa wazi, kwa kifupi kati ya hao wawili kwenye hoja hii wewe unakubaliana na nani na kwanini? Baada ya hapo mimi nitakuwa kwenye nafasi nzuri kujibu hoja yako. Na tubase kwenye hoja hii tu
.

Kwangu mimi naona wote wanabishana vitu pungufu ya tuvitakavyo.Ni kama watu wanabishana issue ya usafiri halafu wanapoteza muda kubishana kuhusu vyombo vya usafiri halafu wao wanabishana kuhsu malori na mabasi,wakati kuna vingi zaidi ila kinachomata ni lengo na aina ya usafiri.Tunahitaji Ethics,nia njema ,watu wanaoweza kwenda extra mile bila kutegemea posho na mengine ya kiadilifu. Sasa kinachotokea hapa ni Shivji kujiona superstar na kutaka nyamazisha watu wote ,ili aendelee linda himaya yake.Watu wanahitaji zaidi ya huo ujuaji wao.Hawa jamaa tunaweza share vipengele fulani ambavyo nia yao ni njema kwa taifa na tukawa wamoja,ila kuna mengi au amachache ambayo yana maslahi yao yaliyofichika ambayo ni mabaya sana kwetu.

Off course warioba ana malengo ya CCM na ya taasisi za kiusalama , wendawazimu wake pia na mengine ni ndoto binafsi ambayo kuna tunayoweza yapenda na mengine ambayo ni mabaya kabisa.All in all ana challenge ya kutopoteza dira kwa usalama wa taifa na umoja wetu.Huku kunahitaji busara zaidi ya hata sheria na mengine.Shivji naye anayo majukumu kama hayo ila alipaswa zaidi kuwajibika zaidi kwa kuzuia malumbano yatakayo fanya zoezi liwe kama sensa.Na kumfanya shivji super star ahlafu ageuze zoezi kuwa kama akina Ponda na wenzao wa CUF walivosanya kwa zoezi la sensa ni kutowajibika sana kama watanzania.Penda tusipende kuna sehemu tutahitaji tumia conventional wisdomIngawa pia tunajua maamuzi ya conventional wisdom mara nyngine huyumiwa na watu kama akina ponda kupotosha umma , ila sheria haina kila jibu.
 
Hapa tuko pamoja, ila kuwa out of control pia inatokana na sisi watz wasomi na wasio wasomi kutojiamini na kuwapapatikia watu wenye majina makubwa. No wonder kila mtu anataka kuwa kigogo ili aheshimiwe - small God. Hata hivyo, with time na hizi shule zetu za kata mambo yataboreka.

mimi binafsi naona tayari Shivji kesha kuwa superstar and undisputed ktk jamii yetu.Warioba hakuna shida kwani mara nyingi tuu watu hupingana nae au "kumpotezea" kwa luga ya mjini.Shivji sivyo ingawa mara nyingi ana vionjo vinavyoashiria kuwa next move zitakuwa very ugly.Na kwa vile yupo ktk taasisi kama ya mwalimu Nyerere, basi hali ni kama tumeshampta keys zote za kujiwekea veto ktk mawazo ya wasomi na wasiosoma.NI wasomi wachache sana wanaoweza shtusha na vionjo fulani vya shivji achilia mbalia kufikia kuwa anaweza kuwa anapotosha makusudi wakati anajiweka ktk position ya kuweza mnyamazisha mtu yoyote na watanzania wakasema "anayebishana na nguli Shivji ana kichaa".

Ni taswira mbaya ktk Bunge ila kuna wabunge wengi sana wa CCM ubunge wao utakuwa salama mpaka 2015 km hakuna kifo kwa vile hakuna pingamizi.Hiyo ndio democrasia anayosema warioba bila kusema kama ni nzuri au mbaya,au imebakwa,ila ndio imetuleta hao watu tulio nao.Na hata tukiwa na zoezi jingine la kuchaguawateuzi bado kuna makundi mengi sana yatatuletea watu wa kimkakati kuliko ina values za wawakilishi.
 
Mkubwa hapo unatupotezea muda, hakuna point hapo.Jaji Warioba yuko sahihi zaidi ya sana.Ni ukweli usiopingika kwamba wabunge wamechaguliwa na ni wawakilishi wa wananchi tulio wengi.Sasa kwamba CCM wako wengi na wengine wachache,huo ndio uamuzi wa wananchi AU unataka wengi wawe wenye mawazo yako na chama chako?
Hembu chapa kazi utushawishi tuwachugue wabunge wengi wa cdm ili muwe wengi bt in the meantime ccm wako wengi YES bt ndio matakwa ya watanzania.
Katiba ni mali ya wananchi na sio ya nyinyi viongozi, wawakilishi wetu wa kwanza kabisa ni WABUNGE.Dont play with that,
 
Ukweli husemwa:

Sija bahatika kuyasoma hayo majibizano na tofauti ya mitizamo yao kwenye gazeti, lakini kwa yale uliyoyaandika na maoni yako, inaonekana hujamtendea haki Jaji Warioba.

Tatizo letu Watanzania, pale tunapomuona mtu anasema mambo mengi tunayoafikiana nayo kimaslahi au kiitikadi, basi hata yale mengine atakayoyasema ambayo ni pumba tunayaona ni mchele. Tumejengeka tabia ambayo pale tunapomwamini mtu fulani, basi tunakuwa kama vipofu wa fikra kwa kile akifanyacho.


Tunatakiwa tujenge tabia ya kujongea kila jambo kwa walakini ili tuweze kubainisha kwa undani sababu zilizoko nyuma ya kila jambo kabla ya kulikubali.


Kama Jaji Warioba alivyosema, 'Utawapata wapi watu ( wajumbe wa Bunge la Katiba) ambao hawana maslahi na suala zito kama katiba ya nchi'.

Pro Shivji anasema haya kwa vile labda ana motive behind lakini vilevile kauli zake nyingi zinaonyesha kama anajaribu kuidhalau tume ya katiba.



Kumbuka wabunge ni wawakilishi wa wananchi ambao wanachaguliwa na wavua samaki, wakulima na wafanyakazi. Kwa mantiki na mchanganuo huo, lazima tu watakuwa ni wengi.


Tatizo kubwa ambalo Watanzania linatusumbua katika mchakato mzima wa katiba ni kutanguliza maslahi ya kiitikadi kwanza badala ya uzalendo.


Hatutaki kujifunza kutokana na makosa mengi ambayo tumechangia kuifikisha nchi hapa ilipo.


Hebu tujaribu kuwa wazalendo kwa hili.

Warioba katumia lugha ya kijanja sana,sikuwa nampenda ila nilifuarahi sana alipombana Jussa na wapuuzi wengine kuhusu issue ya Muungano ili wampe ufafanuzi mzuri unaofaa kuandikwa na si blah blah za kujipronote(Jussa alikwenda kujing`arisha kwa kutumia tume),kushindwa kwake kunaweza kusimfurahishe sana Shivji.Yali mafunzo yake kuhusu katiba niliyafuatilia sana ITV, nilimsoma na kumuelewa.Sikupenda motive nilizoweza gundua ndani yake ila weledi wake naukubali pengine kwa vile sikuwa na uwezo wa kutest fani yake kwa level yake.Time will tell, atabishana na wengi sana kabla ya kuanza naye kuwa furious.
 
ni vizuri pia prof shivji angeainisha hizo hela za kufanya uchaguzi wa nchi nzima zingetoka wapi. sio kuongea tu.let we be realistic
Prof ana enjoy stardom bado, anachosema km hakipingwi vile.Jinsi mnavyofunguka mtamfanya Prof na wengine kabla ya kuongea basi wawe wanatazama parameters nyingi zaidi.Si hii tabia ya kufikiria huku wanaongea,wakikosea nasi tukosee nao wakirudi nyuma nasi turudi nao.Lazima tujiwekee viwango vya kufikia kabla ya kupeleka kitu katika jamii pana kw alengo la kutaka wafuate hivyo.Likiwa na makosa mambo yaliyopo at stake ni makubwa na hayarekebishiki.

Makosa ya mtu kama shivji, mika inayokuja yatatumika na watu km akin aponda kuhalalisha kuwa mchakato wa katiba ulikuwa wa kibabe,haramu etc.By that time kama tutakuwa na wasomi wenye fikra kama akina, Le Mutuz, Lipumba watayawakilisha haya kama ushahidi kwa mbwembwe.
 
Hakuna tatizo hata kidogo. kama katiba mpya haitakidhi majarajio ya wengi itafanyiwa marekebisho wakati muafaka ukifika. tunachotakiwa kuhakikisha ni katiba yenye kuimarisha misingi ya demokrasia na kuwajibika kwa viongozi. tuondoe hofu
 
Kosa kubwa alolifanya mzee wangu Warioba ni kutumia Wananchi kuwachagua wabunge kama sababu ya kuwepo kwao ktk kamati hiyo ya Bunge. Hawa Wabunge walichauliwa kwa sababu ya SERA za CCM na uwezo wao ktk kuwawakilisha ili wapate MAENDELEO. Katiba haijengwi kwa sababu hizo hata kwa Ukaribu. KATIBA ni sheria Mama (supreme law) ni Mwongozo ambao hata wao wabunge wanatakiwa kuapa kiapo cha kuufuata na kuilinda na sii wao wawe watunzi wa viapo watakavyo apa kuilinda hii itakuwa mali yao. (have a cake and eat it too) - How can he say that?..
 
Nyie viumbe waajabu sana...Ismail Jussa aliposema huyu Warioba anazeeka na hivyo hata uwezo wake wakuelewa ni mdogo sasa. Nyinyi wana JF mlimuekea uzi hapa kumlaani eti Jussa amekosa Adabu.

Sasa na nyie kuweni na adabu....maana wengine mnamwita mpuuzi.
 
Na kwa nini wananchi wasipewe nafasi ya kufanya referrendum moja kwa moja?
 
Ogopa njaa ogopa rushwa. Posho milioni kumi kwa mwezi,za nini kama sio za kulinda maslahi ya waliwateua!!! Tafakari Chukua Hatua.
 
Sioni ubaya wa scholars kutofautiana, na mijadala kama hii ndio inayojenga. Scholars differ and that's healthy as long as there is no abuse and it's for the better of the country.

Warioba ni ex-AG, ex-Justice Minister, ex-PM, ex-VP. Si "mwana-CCM" wa kawaida.

Kama ana maoni tofauti na CCM halafu sio tu anashindwa kushawishi maamuzi ndani ya chama, bali pia anakubali kazi za serikali ya CCM bila ku leverage influence yake atakuwa very weak indeed.

Na Warioba ninayemjua mimi si weak, alitaka kujiuzulu on principle u PM wakati wa Mwinyi. Huyu ni mtu anayetaka kutuonyesha anaishi kwa principles.

Which means kwamba anakubaliana na CCM on this.
 
Back
Top Bottom