Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu,
Nimesoma mabishano au tofauti ya mtizamo kati ya prof Issa Shivji na Jaji warioba ktk gazeti la Raia mwema la leo. Nimeshangazwa na msimamo wa Jaji Warioba ninayemheshimu sana, nitaeleza.
Kwa mujibu gazeti la Raia mwema la Leo wasomi hawa wawili wetofautiana juu ya wajumbe wa Bunge la Katiba.
Msimamo Shivji;
Akiwa katka Kongamano la Katiba Prof Shivji alisema;
Kuna kasoro kubwa ktk sheria ya kuendesha mchakato wa katiba mpya, hasa kuhusu uundaji muundo wa Bunge la katiba. Chombo muhimu sana kuliko hata Refrendum ( kura ya maoni) ni Bunge la katiba. Linapaswa kuwa Bunge la wananchi, vinginevyo uhalali wa hiyo Bunge utakuwa na Shaka. Ni Busara kwa wajumbe wa Bunge la Katiba kuchaguliwa moja kwa moja wa Wananchi kwa ajili ya kazi hiyo maalum tu.
Msimamo wa Jaji Warioba.
Hata hivyo, akizungumzia hilo Mkiti wa Tume ya Mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba alimweleza mwandishi wetu akihoji; Utawapata wapi watu ( wajumbe wa Bunge la Katiba) ambao hawana maslahi na suala zito kama katiba ya nchi? Aliendelea ingawa jambo hilo siyo sehemu ya hadidu rejea kwa tume hiyo lakini ni suala la kidemokrasia pia kuwaingiza wabunge na wawakilishi kuwa sehemu ya Bunge la Katiba. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi ni watu waliokabidhiwa pia jukumu la kutunga sheria.
Alipoulizwa kuhusu wingi wa wabunge wa ccm ktk bunge hilo na kwamba watalinda maslahi ya chama chao alijibu, wabunge hao wametokana na mfumo wa demokrasia yetu na ndio mtazamo wa wananchi.
My take;
Hivi jaji Warioba hajui kuwa tunacholalamikia ni wingi wa kundi moja - wabunge, ambao nao wana maslahi lakini hatutaki wao wawe wengi huku makundi mengine ya wavua samaki, wakulima na wafanya kazi wakikosa fursa hiyo?
2. Anaposema uwepo wabunge wengi wa ccm ni mtazamo wa wananchi, hajui kuwa moja ya sababu za kutungwa katiba mpya ni udhaifu wa Tume ya uchaguzi kutuletea viongozi wasiochaguliwa wakiwepo hao wa ccm wanaotuhumiwa kuchakachua kura wakisaidiwa na Tume.
NB, Nadhani jaji wangu ninayemheshimu ameteleza ktk hili kama hajavutwa na ushabiki wa kichama zaidi.
Nimesoma mabishano au tofauti ya mtizamo kati ya prof Issa Shivji na Jaji warioba ktk gazeti la Raia mwema la leo. Nimeshangazwa na msimamo wa Jaji Warioba ninayemheshimu sana, nitaeleza.
Kwa mujibu gazeti la Raia mwema la Leo wasomi hawa wawili wetofautiana juu ya wajumbe wa Bunge la Katiba.
Msimamo Shivji;
Akiwa katka Kongamano la Katiba Prof Shivji alisema;
Kuna kasoro kubwa ktk sheria ya kuendesha mchakato wa katiba mpya, hasa kuhusu uundaji muundo wa Bunge la katiba. Chombo muhimu sana kuliko hata Refrendum ( kura ya maoni) ni Bunge la katiba. Linapaswa kuwa Bunge la wananchi, vinginevyo uhalali wa hiyo Bunge utakuwa na Shaka. Ni Busara kwa wajumbe wa Bunge la Katiba kuchaguliwa moja kwa moja wa Wananchi kwa ajili ya kazi hiyo maalum tu.
Msimamo wa Jaji Warioba.
Hata hivyo, akizungumzia hilo Mkiti wa Tume ya Mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba alimweleza mwandishi wetu akihoji; Utawapata wapi watu ( wajumbe wa Bunge la Katiba) ambao hawana maslahi na suala zito kama katiba ya nchi? Aliendelea ingawa jambo hilo siyo sehemu ya hadidu rejea kwa tume hiyo lakini ni suala la kidemokrasia pia kuwaingiza wabunge na wawakilishi kuwa sehemu ya Bunge la Katiba. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi ni watu waliokabidhiwa pia jukumu la kutunga sheria.
Alipoulizwa kuhusu wingi wa wabunge wa ccm ktk bunge hilo na kwamba watalinda maslahi ya chama chao alijibu, wabunge hao wametokana na mfumo wa demokrasia yetu na ndio mtazamo wa wananchi.
My take;
Hivi jaji Warioba hajui kuwa tunacholalamikia ni wingi wa kundi moja - wabunge, ambao nao wana maslahi lakini hatutaki wao wawe wengi huku makundi mengine ya wavua samaki, wakulima na wafanya kazi wakikosa fursa hiyo?
2. Anaposema uwepo wabunge wengi wa ccm ni mtazamo wa wananchi, hajui kuwa moja ya sababu za kutungwa katiba mpya ni udhaifu wa Tume ya uchaguzi kutuletea viongozi wasiochaguliwa wakiwepo hao wa ccm wanaotuhumiwa kuchakachua kura wakisaidiwa na Tume.
NB, Nadhani jaji wangu ninayemheshimu ameteleza ktk hili kama hajavutwa na ushabiki wa kichama zaidi.