Jaji Warioba: Kuteswa ka Kibanda kulipangwa

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Jaji mkuu mstaafu Jaji Sinde Warioba amedai kuwa kipigo na mateso aliyoyapata Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini bwana Kibanda ni tukio la kupangwa na si la kiarifu kama ilivyodaiwa na Kamanda Kova mzee wa seriez.

Concern:
Kama ni mipango na mchunguzi mkuu (Kova) keshatoa taarifa za mwanzo kuwa ni uharifu tutarajie nini kama mtuhumiwa ajichunguze mwenyewe.

Haaiingii akilini hivi raia wa kawaida atatembeaje na bunduki (smg) usiku kama si askari?
 
Jaji mkuu mstaafu Jaji Sinde Warioba amedai kuwa kipigo na mateso aliyoyapata Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini bwana Kibanda ni tukio la kupangwa na si la kiarifu kama ilivyodaiwa na Kamanda Kova mzee wa seriez.

Concern:
Kama ni mipango na mchunguzi mkuu (Kova) keshatoa taarifa za mwanzo kuwa ni uharifu tutarajie nini kama mtuhumiwa ajichunguze mwenyewe.

Haaiingii akilini hivi raia wa kawaida atatembeaje na bunduki (smg) usiku kama si askari?

mimi nachukia sana unafiki wa hawa watu, warioba, viongozi wa kijamii, viongozi wa kidini mlikuwa wapi Dr. Ulimboka alipokuwa analia kuwa amepigwa na maofisa wa ikulu. watu wote niliowataja hapo walikaa kimya isipokuwa wana harakati wachache ndio walijitokeza kuiomba ikulu itoe maelezo kuhusiana na tukio hilo. kwanini viongozi wote hao wasijitokeze hadharani kusimamia ukweli wakati muhimu wanapokuwa wanaitajika. leo wanaibuka na issue ya kibanda wakati hakuna tofauti yeyote katika issue hizi mbili.
 
kama makosa yalifanyika nyuma hatuna haja ya kuendelea kuyafanya sasa. kama zaman tulinyamazia uovu haitakiwi hata leo tuendelee kunyamazia uovu. na baadae tuendelee kunyamazia uovu.
 
Tusitarajie mapya kutoka kwa hawa polisi wetu....kwani yaliyopita yana tofauti gani na hili, ngedere amchunguze nyani.
 
mimi nachukia sana unafiki wa hawa watu, warioba, viongozi wa kijamii, viongozi wa kidini mlikuwa wapi Dr. Ulimboka alipokuwa analia kuwa amepigwa na maofisa wa ikulu.

Watu wote niliowataja hapo walikaa kimya isipokuwa wana harakati wachache ndio walijitokeza kuiomba ikulu itoe maelezo kuhusiana na tukio hilo.

kwanini viongozi wote hao wasijitokeze hadharani kusimamia ukweli wakati muhimu wanapokuwa wanaitajika.

Leo wanaibuka na issue ya kibanda wakati hakuna tofauti yeyote katika issue hizi mbili.


........

Kichwa chako hakina kumbukumbu. Hao wote uliowataja walitoa matamko yao wakati wa Ulimboka. Labda hukuyasoma. Jipange kutoa hoj nyingine.
 
kwa haya yanayotokea kila kukicha (utekaji,utesaji,uuaji wa makusudi wa raia wasio na hatia) na ambacho Ikulu wakati mwingine kuelezwa kuhusika,kumeifanya kusiwe(ikulu) mahala patakatifu tena
 
Nakubaliana na Mh. Warioba 100%. Kama Serikali inataka kujinasua katika hizi lawama basi iombe msaada toka FBI ya Merikani au Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza. Kutumia Kova ni kugeresha tu.


Ikumbukwe kwamba hivi karibuni Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar ilikaribisha FBI kuchunguza mauaji yaliyoonekana ni vigumu Polisi wetu kuchunguza.
 
Nakubaliana na Mh. Warioba 100%. Kama Serikali inataka kujinasua katika hizi lawama basi iombe msaada toka FBI ya Merikani au Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza. Kutumia Kova ni kugeresha tu.


Ikumbukwe kwamba hivi karibuni Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar ilikaribisha FBI kuchunguza mauaji yaliyoonekana ni vigumu Polisi wetu kuchunguza.

Then viongozi wa jeshi la Police wajiuzuru kwa kushindwa kazi. Maana haina maana walipwe mishahara wakati kazi hawafanyi. Wao ni kutoa matamko hata kabla ya uchunguzi. Sasa kama Kova anasema ni waharifu mbona anashindwa kuwakamata?? Kuwaleta FBI ni ushahidi tosha kuwa hakuna kinachoendelea hapa. Rais anatakiwa kuwawajibisha hawa kwa vile kila mmoja wetu pamoja na serikali yenyewe wamekubali kushindwa kazi na ndiyo sababu wanatafuta msaada wa FBI!!
 
Tutegemee mengi kutokea ,kwani viongozi wetu wanaona gharama za usalama wetu ni kubwa mnoooooooo.
 
Yuko wapi nchimbi atutangazie na sisi bara kuna magaidi yana baka yana kongota ni ma dentist waje FBI wachunguze yuko wapi mzee mwana kijiji aje atuambie hawa watu walokua mahodari wa kutoa meno na kucha ni magaidi wanatoka zanzibar mmmmmmmhhhh tanzania eeeee mwanangu kuwa uyaone
 
Jaji mkuu mstaafu Jaji Sinde Warioba amedai kuwa kipigo na mateso aliyoyapata Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini bwana Kibanda ni tukio la kupangwa na si la kiarifu kama ilivyodaiwa na Kamanda Kova mzee wa seriez.

Concern:
Kama ni mipango na mchunguzi mkuu (Kova) keshatoa taarifa za mwanzo kuwa ni uharifu tutarajie nini kama mtuhumiwa ajichunguze mwenyewe.

Haaiingii akilini hivi raia wa kawaida atatembeaje na bunduki (smg) usiku kama si askari?


Mbowe na Tanzania Daima wanayo siri ya Kutekwa na Kujeruhiwa kwa Kibanda

Salaam Wakuu,
Tasnia ya Habari kwa sasa imejawa na simanzi kutokana na kitendo cha kuvamiwa na kuumizwa na watu ambao hawajabainika walikuwa na lengo gani. Mimi kwa ujumla nimesikitishwa sana kutokana na tukio hilo na nawalaani wote waliohusika. Aidha, natumia fursa hii kumuombea ndugu yetu Kibanda apone kwa haraka ili arejee nyumbani salama kuungana na familia yake na hatimaye kuendelea na majukumu yake.

Baada maelezo hayo, naomba kwa pamoja tutafakari mambo yafuatayo;


  1. Juzi Jumanne tarehe 05/03/2013 kulikuwa na kikao cha wadau wa demokrasia nchini kilichoandaliwa na Kituo cha Demokrasia nchini (Tanzania Centre for Democracy – TCD). Wenyeviti wa vyama vyote vya siasa ni wajumbe na walipata barua za mwaliko kuhudhuria kikao hicho. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), FREEMAN MBOWE, ni miongoni mwa wajumbe walioalikwa. Hata hivyo, Mbowe alitoa udhuru ya kutohudhuria kikao hicho kwa madai kuwa atakuwa jimboni kwake, Hai kuhudhuria kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri wilaya ya Hai (Full Council). Hizi zote ni facts na mimi nikiwa miongoni mwa wajumbe wa kikao hicho, nilimsikia ANTHONY KOMU, Mkurugenzi wa Utawala wa CHADEMA ambaye ndiye alimwakilisha Mbowe akitoa maelezo hayo.
  2. Hata hivyo, katika tukio la kuvamiwa na kuumizwa vibaya kwaAbsalom Kibanda, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri wa New Habari Corporation (2006), Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ameonekana Hospitali ya Taifa ya Mhimbili akimjulia hali ndugun yetu Kibanda.
  3. Pia hakuna uthibitisho kuwa Mbowe alienda jimboni kwake kama alivyodai wakati akitoa udhuru wa kutohudhuria kikao cha TCD.
  4. Kwa vile kwa zaidi ya miezi kadhaa sasa, KIBANDA amekuwa na mgogoro na Tanzania Daima gazeti ambalo linamilikiwa na FREEMAN MBOWE, na kwa vile KIBANDA ana siri nyingi sana za CHADEMA na kwa hali hiyo viongozi wa Chama hicho wanamuona kama ni adui, na kwa kuwa kitendo cha Mbowe kutohudhuria kikao cha TCD kilitumika tu kama ushahidi wa yeye kutokuwepo Dar es Salaam wakati wa tukio hilo na hivyo asiwe mshukiwa nambari moja, kitendo cha yeye kuonekana Hospitali ya Mhimbili akimsalimia KIBANDA, kilinishtua na kuniachia maswali mengi.
 
Mbowe na Tanzania Daima wanayo siri ya Kutekwa na Kujeruhiwa kwa Kibanda

Salaam Wakuu,
Tasnia ya Habari kwa sasa imejawa na simanzi kutokana na kitendo cha kuvamiwa na kuumizwa na watu ambao hawajabainika walikuwa na lengo gani. Mimi kwa ujumla nimesikitishwa sana kutokana na tukio hilo na nawalaani wote waliohusika. Aidha, natumia fursa hii kumuombea ndugu yetu Kibanda apone kwa haraka ili arejee nyumbani salama kuungana na familia yake na hatimaye kuendelea na majukumu yake.

Baada maelezo hayo, naomba kwa pamoja tutafakari mambo yafuatayo;


  1. Juzi Jumanne tarehe 05/03/2013 kulikuwa na kikao cha wadau wa demokrasia nchini kilichoandaliwa na Kituo cha Demokrasia nchini (Tanzania Centre for Democracy – TCD). Wenyeviti wa vyama vyote vya siasa ni wajumbe na walipata barua za mwaliko kuhudhuria kikao hicho. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA), FREEMAN MBOWE, ni miongoni mwa wajumbe walioalikwa. Hata hivyo, Mbowe alitoa udhuru ya kutohudhuria kikao hicho kwa madai kuwa atakuwa jimboni kwake, Hai kuhudhuria kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri wilaya ya Hai (Full Council). Hizi zote ni facts na mimi nikiwa miongoni mwa wajumbe wa kikao hicho, nilimsikia ANTHONY KOMU, Mkurugenzi wa Utawala wa CHADEMA ambaye ndiye alimwakilisha Mbowe akitoa maelezo hayo.
  2. Hata hivyo, katika tukio la kuvamiwa na kuumizwa vibaya kwaAbsalom Kibanda, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri wa New Habari Corporation (2006), Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ameonekana Hospitali ya Taifa ya Mhimbili akimjulia hali ndugun yetu Kibanda.
  3. Pia hakuna uthibitisho kuwa Mbowe alienda jimboni kwake kama alivyodai wakati akitoa udhuru wa kutohudhuria kikao cha TCD.
  4. Kwa vile kwa zaidi ya miezi kadhaa sasa, KIBANDA amekuwa na mgogoro na Tanzania Daima gazeti ambalo linamilikiwa na FREEMAN MBOWE, na kwa vile KIBANDA ana siri nyingi sana za CHADEMA na kwa hali hiyo viongozi wa Chama hicho wanamuona kama ni adui, na kwa kuwa kitendo cha Mbowe kutohudhuria kikao cha TCD kilitumika tu kama ushahidi wa yeye kutokuwepo Dar es Salaam wakati wa tukio hilo na hivyo asiwe mshukiwa nambari moja, kitendo cha yeye kuonekana Hospitali ya Mhimbili akimsalimia KIBANDA, kilinishtua na kuniachia maswali mengi.

huu ndio ukweli mchungu, kova anatakiwa aanzie hapa.kovaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa njooooooooooooooooo uchukue ushahidi wa mateso na watesaji wa kibandaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Tutegemee mengi kutokea ,kwani viongozi wetu wanaona gharama za usalama wetu ni kubwa mnoooooooo.

Nasi tumezidi kuilaumu serikali na hivyo maadui zetu kutumia mianya hiyo kutudhuru huku wakijua lawama zitawaendelea viongozi wa serikali
 
vipi raisi awawajibishe ikiwa yeye mwenyewe ahitaji kuwajibishwa kwa maswala mengine uchafu hauwezi kujiondosha.
 
huu ndio ukweli mchungu, kova anatakiwa aanzie hapa.kovaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa njooooooooooooooooo uchukue ushahidi wa mateso na watesaji wa kibandaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Mkuu mimi nashangaa sana POLISI sijui wanawaogopa hawa CDM, mazingira yanaonesha wazi kabisa kuhusika na hili tukio bado wana delay na ndiyo maana Serikali inalaumiwa kuwa haichukui hatua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom