Jaji Joseph Sinde Warioba ameishangaa tume ya uchaguzi ya Tanzania kwa kitendo chake cha kuengua wagombea wa vyama mbalimbali vya upinzani bila kufwata utaratibu.
Ameishangaa kuengua wagombea wa vyama mbalimbali bila kuzingatia katiba badala yake kutumia vigezo dhaifu ktk kumuengua mgombea.
Ameishauri tume kufwata utaratibu mpya badala utaratibu huu Usiokua wa haki.
Pamoja na hayo ameshangaa kuona viongozi wa kisiasa wanashindwa kukaa pamoja kwa ajili ya Taifa badala yake wametanguliza ubinafsi, tamaa ya madaraka na itikadi.
Amewashauri kuachana na itikadi za vyama vyao badala yake waliangalie Taifa.
Ameyasema hayo ktk maadhimisho ya haki za Binadamu Duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Huyu ni Kiongozi wa kwanza mstaafu ambae ameishaanza kuona madhaifu yetu kama nchi ambayo yanaweza kutupeleka kubaya kama nchi na hivyo kutoa tahadhari.
Amevunja ukimya na kujionesha utofauti wake na wengine ambao ni wazalendo maslahi ambao kazi yao kubwa ni kusifu na kuabudu ili kulinda matumbo yao na familia zao.