Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,687
- 15,108
Mhe. Biswalo Mganga,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa mamlaka aliyonayo wewe Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, pamoja na Naibu wako, na kukuteua kuwa Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania.
Mhe. Biswalo Mganga,
Ninachotaka kukwambia, kwa niaba ya wananchi wa Tanzania, hususani Wazalendo kwa taifa letu ni kwamba, baada ya utawala wa hayati Baba wa taifa mwl. Julius Kambarage Nyerere, hakujawahi kutokea Mkurugenzi wa Mashitaka aliyefanya kazi kwa viwango vyako wewe.
Wewe ni Mkurugenzi wa Mashitaka mzalendo kuwahi kutokea, uliyeipenda nchi yako, uliyepambana na wahujumu uchumi, wala rushwa, wakwepaji kodi, mafisadi, majangiri, majambazi, waporaji wa rasilimali za nchi hii, na viongozi waliotumia madaraka yao vibaya kujinufaisha. Umeifanya kazi yako usiku na mchana bila kuchoka wala kuhofia usalama wa maisha yako.
Mhe. Biswalo Mganga,
Wananchi tunatambua jinsi ulivyosimamia uendeshaji wa kesi mbali mbali za uhujumu uchumi ikiwemo ya wazungu wa kampuni ya Barrick pamoja jangiri mashuhuri muuwaji wa tembo ambaye alishindikana kukamatwa tangu alipoanza ujangiri mwaka 1986 kufikia hatua ya kujiita Malikia wa Tembo, lakini kupitia uongozi wako mahiri, leo jangiri huyu yupo gerezani, tembo wamezaliana, wanazurula hadi kwenye makazi ya watu kwa amani na raha mustarehe.
Hata kama mamlaka ya uteuzi wako imeona hufai kuendelea kuhudumu kama Mkurugenzi wa Mashitaka, nataka nikutie moyo kwamba, wananchi tunatambua mchango wa utumishi wako ulioleta matokeo chanya kwenye uchumi hadi nchi kufikia uchumi wa kipato cha kati kabla ya makadirio ya muda uliowekwa 2025.
Ni kupitia wewe, ofisi yako iliweza kurudisha fedha mabilioni yaliyokuwa yakiibwa na wafanya biashara walioigeuza nchi hii kuwa shamba la bibi, akiwemo aliyekuwa akiiba milioni 7 kwa kila dakika kwa njia ya kukwepa kodi kwa kutumia mfumo wa mashine za EFD.
Wewe ndiye Mkurugenzi wa Mashitaka uliyekomesha tabia sugu ya Wana siasa hususani wa upinzani iliyokuwa imeota mizizi ya kutoheshimu sheria, kanuni na taratibu za nchi. Hukuangalia cheo cha mtu wala nafasi aliyonayo katika jamii. Ni nani kama Biswaro Eutropius Mganga?
Mhe. Biswalo Mganga,
Uzalendo wako kwa nchi si tu kwamba ulibakia kulinda rasilimali za ndani bali ulivuka mipaka kwa kufuatilia rasilimali zilizoporwa na kutoroshewa nje ya nchi, ambapo ulifanikisha kurejeshwa kwa madini ya dhahabu na mamilioni ya fedha zikiwemo dola za Marekani zilizoporwa na majambazi nchini mwaka 2013 na kukamatiwa Kenya. Hongera sana kwa hilo.
Kwangu mimi wewe ni shujaa miongoni mwa mashujaa waliowahi kutokea katika kuitetea nchi na rasilimali zake. Wewe ni kiongozi uliyehakikisha kila mkosaji anashitakiwa, bila kujali anayo nafasi gani kwenye jamii au ni maarufu. Ulikomesha majigambo ya waliokuwa wakisema, UNANIJUA MIMI NANI. Uonevu ulikoma kama siyo kumalizika. Hakuna DPP kama wewe. Mungu akutunze.
Nataka nikuhakikishie kwamba, historia ya nchi hii kuhusu ujenzi wa uchumi, ulinzi wa rasilimali za nchi, mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka, haiwezi kuandikwa na kukamilika bila jina lako kutajwa, na kwa msingi huo, historia italiandika jina lako kwa wino wa dhahabu.
Mhe. Biswalo Mganga,
Naomba nihitimishe hoja yangu kwako kwa kusema kwamba, ustawi wa kiuchumi wa taifa lolote duniani, unategemeana kwa kiasi kikubwa na uimara wa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka katika nchi husika.
Mafanikio ya kiuchumi yaliyopatikana kwa nchi yetu ikiwemo ufanisi katika kukusanya kodi, ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile Bwawa la Mwl. Nyerere, Ujenzi wa reli ya Standard Gauge, Ujenzi wa Vituo vya afya, Zahanati, Hospitali za Wilaya, Mkoa na Kanda, Usambazaji wa maji mijini na vijijini, usambazaji wa umeme vijijini, utoaji elimu bure, mikopo ya elimu ya juu, yote haya yamewezekana kutokana na ushupavu wa uongozi wako ukiwa Mkurugenzi wa Mashitaka.
Kwenye nchi yoyote ambayo Mkurugenzi wa Mashitaka anakuwa upande wa wahalifu, haya yasingewezekana kufanyika. Nikuombe nenda kachape kazi kwenye nafasi yako mpya, huku ukimtanguliza Mungu mbele. Tembea kifua mbele, wananchi wazalendo tupo nyuma yako. Usisikilize kelele za maadui wa kazi yako wala kunyong'onyea bali endelea kusimama kwenye nafasi yako ya kulitetea taifa. Hakika uongozi wako umeacha alama isiyofutika..
Lema na Chadema kwa ujumla mkome kumwandama jaji Biswaro Mganga, kesi zenu za uhujumu uchumi ataziamua yeye.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa mamlaka aliyonayo wewe Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, pamoja na Naibu wako, na kukuteua kuwa Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania.
Mhe. Biswalo Mganga,
Ninachotaka kukwambia, kwa niaba ya wananchi wa Tanzania, hususani Wazalendo kwa taifa letu ni kwamba, baada ya utawala wa hayati Baba wa taifa mwl. Julius Kambarage Nyerere, hakujawahi kutokea Mkurugenzi wa Mashitaka aliyefanya kazi kwa viwango vyako wewe.
Wewe ni Mkurugenzi wa Mashitaka mzalendo kuwahi kutokea, uliyeipenda nchi yako, uliyepambana na wahujumu uchumi, wala rushwa, wakwepaji kodi, mafisadi, majangiri, majambazi, waporaji wa rasilimali za nchi hii, na viongozi waliotumia madaraka yao vibaya kujinufaisha. Umeifanya kazi yako usiku na mchana bila kuchoka wala kuhofia usalama wa maisha yako.
Mhe. Biswalo Mganga,
Wananchi tunatambua jinsi ulivyosimamia uendeshaji wa kesi mbali mbali za uhujumu uchumi ikiwemo ya wazungu wa kampuni ya Barrick pamoja jangiri mashuhuri muuwaji wa tembo ambaye alishindikana kukamatwa tangu alipoanza ujangiri mwaka 1986 kufikia hatua ya kujiita Malikia wa Tembo, lakini kupitia uongozi wako mahiri, leo jangiri huyu yupo gerezani, tembo wamezaliana, wanazurula hadi kwenye makazi ya watu kwa amani na raha mustarehe.
Hata kama mamlaka ya uteuzi wako imeona hufai kuendelea kuhudumu kama Mkurugenzi wa Mashitaka, nataka nikutie moyo kwamba, wananchi tunatambua mchango wa utumishi wako ulioleta matokeo chanya kwenye uchumi hadi nchi kufikia uchumi wa kipato cha kati kabla ya makadirio ya muda uliowekwa 2025.
Ni kupitia wewe, ofisi yako iliweza kurudisha fedha mabilioni yaliyokuwa yakiibwa na wafanya biashara walioigeuza nchi hii kuwa shamba la bibi, akiwemo aliyekuwa akiiba milioni 7 kwa kila dakika kwa njia ya kukwepa kodi kwa kutumia mfumo wa mashine za EFD.
Wewe ndiye Mkurugenzi wa Mashitaka uliyekomesha tabia sugu ya Wana siasa hususani wa upinzani iliyokuwa imeota mizizi ya kutoheshimu sheria, kanuni na taratibu za nchi. Hukuangalia cheo cha mtu wala nafasi aliyonayo katika jamii. Ni nani kama Biswaro Eutropius Mganga?
Mhe. Biswalo Mganga,
Uzalendo wako kwa nchi si tu kwamba ulibakia kulinda rasilimali za ndani bali ulivuka mipaka kwa kufuatilia rasilimali zilizoporwa na kutoroshewa nje ya nchi, ambapo ulifanikisha kurejeshwa kwa madini ya dhahabu na mamilioni ya fedha zikiwemo dola za Marekani zilizoporwa na majambazi nchini mwaka 2013 na kukamatiwa Kenya. Hongera sana kwa hilo.
Kwangu mimi wewe ni shujaa miongoni mwa mashujaa waliowahi kutokea katika kuitetea nchi na rasilimali zake. Wewe ni kiongozi uliyehakikisha kila mkosaji anashitakiwa, bila kujali anayo nafasi gani kwenye jamii au ni maarufu. Ulikomesha majigambo ya waliokuwa wakisema, UNANIJUA MIMI NANI. Uonevu ulikoma kama siyo kumalizika. Hakuna DPP kama wewe. Mungu akutunze.
Nataka nikuhakikishie kwamba, historia ya nchi hii kuhusu ujenzi wa uchumi, ulinzi wa rasilimali za nchi, mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka, haiwezi kuandikwa na kukamilika bila jina lako kutajwa, na kwa msingi huo, historia italiandika jina lako kwa wino wa dhahabu.
Mhe. Biswalo Mganga,
Naomba nihitimishe hoja yangu kwako kwa kusema kwamba, ustawi wa kiuchumi wa taifa lolote duniani, unategemeana kwa kiasi kikubwa na uimara wa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka katika nchi husika.
Mafanikio ya kiuchumi yaliyopatikana kwa nchi yetu ikiwemo ufanisi katika kukusanya kodi, ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile Bwawa la Mwl. Nyerere, Ujenzi wa reli ya Standard Gauge, Ujenzi wa Vituo vya afya, Zahanati, Hospitali za Wilaya, Mkoa na Kanda, Usambazaji wa maji mijini na vijijini, usambazaji wa umeme vijijini, utoaji elimu bure, mikopo ya elimu ya juu, yote haya yamewezekana kutokana na ushupavu wa uongozi wako ukiwa Mkurugenzi wa Mashitaka.
Kwenye nchi yoyote ambayo Mkurugenzi wa Mashitaka anakuwa upande wa wahalifu, haya yasingewezekana kufanyika. Nikuombe nenda kachape kazi kwenye nafasi yako mpya, huku ukimtanguliza Mungu mbele. Tembea kifua mbele, wananchi wazalendo tupo nyuma yako. Usisikilize kelele za maadui wa kazi yako wala kunyong'onyea bali endelea kusimama kwenye nafasi yako ya kulitetea taifa. Hakika uongozi wako umeacha alama isiyofutika..
Lema na Chadema kwa ujumla mkome kumwandama jaji Biswaro Mganga, kesi zenu za uhujumu uchumi ataziamua yeye.