Jaji Ramadhani: Haki haikutendeka mchakato wa kupata mgombea 2015

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,998
144,329
Aliekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Agustino Ramadhani amesema utaratibu uliotumiwa na kamati kuu ya CCM(CC) wa kukata majina yao katika uteuzi wa Urais haukuwa wa haki.

Amesema hakupata nafasi ya jina lake kuchekechwa katika uchaguzi huo bali kulaumu ilipita na majina yao yakakatwa, amesema amepanga kwenda kuonana na uongozi wa juu hivi karibuni kutokana na kile alichosema hakubaliani na mambo ndani ya chama hicho tawala.

Chanzo; Mtanzania
 
Ha ha lol, aliendaga wapi huyu MTU mbona alikuwa kimya sana, Na nini kimemtoa huko alipokuwa Na kusema yote haya?
 
Mmoja wa waliokuwa wakigombea kuteuliwa kugombea uraisi na Chama cha Mapinduzi (CCM),Jaji Mstaafu Agustino Ramadhani, amesema kuwa utaratibu wa kumpata mgombea uraisi wa chama hicho katika uchaguzi mkuu uliopita haukuwa wa haki.

Chanzo:Mwananchi
Jaji ndio anasema haya leo? watu tushasahau uchaguzi, hapa ngoma ni Muafaka zenji, atupe msimamo wakeee
 
Mmoja wa waliokuwa wakigombea kuteuliwa kugombea uraisi na Chama cha Mapinduzi (CCM),Jaji Mstaafu Agustino Ramadhani, amesema kuwa utaratibu wa kumpata mgombea uraisi wa chama hicho katika uchaguzi mkuu uliopita haukuwa wa haki.

Chanzo:Mwananchi
Alivyoujubali ushauri wa kuchukua form ya kujiingiza huko siasani ni kama alikubali ushauri wa kuchoma moto CV yake.
 
Ni kweli Jaji dunia nzima na Tanzania iliona uhuni uliofanyika dodoma, na kwakuwa hakupatikana kwa haki Ndio maana hatendi haki, hatetei haki wala hasimamii haki, zaidi ya kutumia nguvu km zilivyotumika Na NEC kumpata yeye
 
Aliekuwa jaji mkuu wa Tanzania, Agustino Ramadhani amesema utaratibu uliotumiwa na kamati kuu ya CCM(CC) wa kukata majina yao katika uteuzi wa Urais haukuwa wa haki.

Amesema hakupata nafasi ya jina lake kuchekechwa katika uchaguzi huo bali kulaumu ilipita na na majina yao yakakatwa, amesema amepanga kwenda kuonana na uongozi wa juu hivi karibuni kutokana na kile alichosema hakubaliani na mambo ndani ya chama hicho tawala.

Chanzo; Mtanzania

Kwa nini hakusema wakati ule ule kama wenzake ili akisadie Chama? Alikuwa anawaza nini muda wote?
 
mi ccm walinifurahisha sana dodoma... nchi ilipofikia ilikuwa lazima ukate watu bila kuangalia sura...

watu walifikiri urais ni lele mama unaupata tu kizembe zembe..
 
mambo ya ccm, mnayabebea bango kwl kwl, haya hebu 2ambie ni wagombea wangapi walichukua form ya kugombea urais kupitia chama chako cha CHADEMA.? hz hakir za kushikiwa na mbowe mtadumu nazo mpaka ln makamanda?
 
Kucheza Basket ball na Mkwere 1977 Znz alidhan kungemsaidia.
CcM haijawahi kwenda Dodoma ikiwa haina jina la Mgombea. Mengine Maigizo. Jk na Mkapa walishamteua Magu tangu January 2015,Mwandosya anasema alielezwa hivyo akadhani utani.
 
Jaji nae heshima iliyokua imebakia kwake anataka iondokee.siku zote mapatano hua ni ufukweni.
 
Back
Top Bottom