Jaji Mutungi Unaiabisha Nafsi na Ofisi Yako

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,489
40,999
Hapo zamani, enzi za akina Jaji Nyalali, Augustino Ramadhani, Rugakingira, Jaji Warioba, ukisikia jaji anasema kitu, unakaa chini ili usikie anasema nini. Kama ni gazeti, lazima utanunua ili ujue anachokitamka jaji.

Ujaji ilikuwa ni nafasi ya heshima kubwa, ilikuwa inaonekana ni kazi takatifu, kwa sababu ilikuwa inaashiria uwezo wa hali ya juu, akili ya kiwango cha juu, maadili ya hali ya juu, na weledi wa masuala ya haki kwa kiwango cha hali ya juu.

Siku za karibuni, nafasi hii ya ujaji, si chochote wala si lolote. Wapo watu wa aina zote, wakiwemo wanafiki, waongo, wala rushwa, wapindisha haki na wapambe wa siasa na wanasiasa. Hakuna weledi wala maadili.

Namshangaa sana Mutungi, na kwa kweli mtu mwenye uweledi wa ujaji asingefanya kama alivyofanya katika kuunda aliyoiita Kamati ya kuyapitia mapendekezo ya namna ya kufanya shughuli za siasa pamoja na kupata Tume huru ya uchaguzi.

Jaji wa kweli angeanza na kanuni zitakazotumika kuwapata wajumbe wa hiyo kamati, na kanuni hizo zikubaliwe na wadau. Hakufanya hivyo. Sijui kama ni tatizo la weledi au dhamira mbaya.

Nchi hii anayelalamikiwa kuvuruga mfumo wa demokrasia, kuiba kura, kutangaza wagombea ambao hawakushinda, kuiba maboksi ya kura, kubambikia wagombea wa vyama vya upinzani kesi, kupora fomu za wagombea wa kutoka vya vya upinzani, kukataa kupokea fomu za wagombea, kukata majina ya wagombea kwa sababu za uwongo, ni CCM kwa kutumia Serikali ikizihusisha kwa karibu taasisi kama:

1) Tume ya uchaguzi
2) Wakurugenzi wa Wilaya na WEOs
3) Polisi
4) Wakuu wa Mikoa
5) Wakuu wa Wilaya
6) Usalama wa Taifa
7) Msajili wa vyama vya siasa

Leo eti unaunda Kamati ya kuangalia namna ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi, kurudishamfumo wa kidemokradia wa kufanya shughuli za siasa, halafu wajumbe wa kufanya hayo, ni hao hao au kutoka kwenye taasisi hizo hizo chafu dhidi ya demokrasia.

Mutungi, nasita hata kukutaja Jaji, kanuni za haki na neutrality unazifahamu? Umefanya kwa kutokufahamu au una dhamira chafu ndani yako?

Kama utaratibu wenyewe wa kuipata Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo huu wa kutumia watu wale wale waliokuwa wanaangamiza demokrasia, zoezi zima halima maana, ni upotezaji wa muda na fedha.

Ni tangu lini jambazi akaweka kanuni nzuri za kuzuia ujambazi?
 
Hapo zamani, enzi za akina Jaji Nyalali, Augustino Ramadhani, Rugakingira, Jaji Warioba, ukisikia jaji anasema kitu, unakaa chini ili usikie anasema nini. Kama ni gazeti, lazima utanunua ili ujue anachokitamka jaji.

Ujaji ilikuwa ni nafasi ya heshima kubwa, ilikuwa inaonekana ni kazi takatifu, kwa sababu ilikuwa inaashiria uwezo wa hali ya juu, akili ya kiwango cha juu, maadili ya hali ya juu, na weledi wa masuala ya haki kwa kiwango cha hali ya juu.

Siku za karibuni, nafasi hii ya ujaji, si chochote wala si lolote. Wapo watu wa aina zote, wakiwemo wanafiki, waongo, wala rushwa, wapindisha haki na wapambe wa siasa na wanasiasa. Hakuna weledi wala maadili.

Namshangaa sana Mutungi, na kwa kweli mtu mwenye uweledi wa ujaji asingefanya kama alivyofanya katika kuunda aliyoiita Kamati ya kuyapitia mapendekezo ya namna ya kufanya shughuli za siasa pamoja na kupata Tume huru ya uchaguzi.

Jaji wa kweli angeanza na kanuni zitakazotumika kuwapata wajumbe wa hiyo kamati, na kanuni hizo zikubaliwe na wadau. Hakufanya hivyo. Sijui kama ni tatizo la weledi au dhamira mbaya.

Nchi hii anayelalamikiwa kuvuruga mfumo wa demokrasia, kuiba kura, kutangaza wagombea ambao hawakushinda, kuiba maboksi ya kura, kubambikia wagombea wa vyama vya upinzani kesi, kupora fomu za wagombea wa kutoka vya vya upinzani, kukataa kupokea fomu za wagombea, kukata majina ya wagombea kwa sababu za uwongo, ni CCM kwa kutumia Serikali ikizihusisha kwa karibu taasisi kama:

1) Tume ya uchaguzi
2) Wakurugenzi wa Wilaya na WEOs
3) Polisi
4) Wakuu wa Mikoa
5) Wakuu wa Wilaya
6) Usalama wa Taifa
7) Msajili wa vyama vya siasa

Leo eti unaunda Kamati ya kuangalia namna ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi, kurudishamfumo wa kidemokradia wa kufanya shughuli za siasa, halafu wajumbe wa kufanya hayo, ni hao hao au kutoka kwenye taasisi hizo hizo chafu dhidi ya demokrasia.

Mutungi, nasita hata kukutaja Jaji, kanuni za haki na neutrality unazifahamu? Umefanya kwa kutokufahamu au una dhamira chafu ndani yako?

Kama utaratibu wenyewe wa kuipata Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo huu wa kutumia watu wale wale waliokuwa wanaangamiza demokrasia, zoezi zima halima maana, ni upotezaji wa muda na fedha.

Ni tangu lini jambazi akaweka kanuni nzuri za kuzuia ujambazi?
Ile ishu la Lipumba na genge lake pale CUF ilinifanya nimdharau huyo mzee kuliko toilet paper!! Inshort ni mtu wa hovyo sana!
 
...
Leo eti unaunda Kamati ya kuangalia namna ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi, kurudishamfumo wa kidemokradia wa kufanya shughuli za siasa, halafu wajumbe wa kufanya hayo, ni hao hao au kutoka kwenye taasisi hizo hizo chafu dhidi ya demokrasia.
...
Nimeona uteuzi wa hicho kinachoitwa "Kamati" umesainiwa na Mutungi; nikajiuliza, hilo ni jukumu la Msajili wa Vyama vya Siasa? Sikupata majibu. Pili, kurudisha mfumo wa kidemokrasia wa kufanya shughuli za siasa! Lol! Kumbe ulikuwa umepotea? Nini kilipelekea ukapotea? "Mashetani" wale wale waliopelekea ukapotea hawataupoteza tena? Assurance iko wapi kwamba sasa utadumu?

Lakini hili nalo ni kichekeso! Tangu lini haki ambazo ziko bayana kikatiba zikaundiwa kamati ya kuzijadili? Katiba na sheria za nchi ziko very clear kuhusu ufanyaji shughuli za kisiasa; hiyo Kamati ita-ammend Katiba na sheria au? Another wastage of time and resources!
 
Hapo zamani, enzi za akina Jaji Nyalali, Augustino Ramadhani, Rugakingira, Jaji Warioba, ukisikia jaji anasema kitu, unakaa chini ili usikie anasema nini. Kama ni gazeti, lazima utanunua ili ujue anachokitamka jaji.

Ujaji ilikuwa ni nafasi ya heshima kubwa, ilikuwa inaonekana ni kazi takatifu, kwa sababu ilikuwa inaashiria uwezo wa hali ya juu, akili ya kiwango cha juu, maadili ya hali ya juu, na weledi wa masuala ya haki kwa kiwango cha hali ya juu.

Siku za karibuni, nafasi hii ya ujaji, si chochote wala si lolote. Wapo watu wa aina zote, wakiwemo wanafiki, waongo, wala rushwa, wapindisha haki na wapambe wa siasa na wanasiasa. Hakuna weledi wala maadili.

Namshangaa sana Mutungi, na kwa kweli mtu mwenye uweledi wa ujaji asingefanya kama alivyofanya katika kuunda aliyoiita Kamati ya kuyapitia mapendekezo ya namna ya kufanya shughuli za siasa pamoja na kupata Tume huru ya uchaguzi.

Jaji wa kweli angeanza na kanuni zitakazotumika kuwapata wajumbe wa hiyo kamati, na kanuni hizo zikubaliwe na wadau. Hakufanya hivyo. Sijui kama ni tatizo la weledi au dhamira mbaya.

Nchi hii anayelalamikiwa kuvuruga mfumo wa demokrasia, kuiba kura, kutangaza wagombea ambao hawakushinda, kuiba maboksi ya kura, kubambikia wagombea wa vyama vya upinzani kesi, kupora fomu za wagombea wa kutoka vya vya upinzani, kukataa kupokea fomu za wagombea, kukata majina ya wagombea kwa sababu za uwongo, ni CCM kwa kutumia Serikali ikizihusisha kwa karibu taasisi kama:

1) Tume ya uchaguzi
2) Wakurugenzi wa Wilaya na WEOs
3) Polisi
4) Wakuu wa Mikoa
5) Wakuu wa Wilaya
6) Usalama wa Taifa
7) Msajili wa vyama vya siasa

Leo eti unaunda Kamati ya kuangalia namna ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi, kurudishamfumo wa kidemokradia wa kufanya shughuli za siasa, halafu wajumbe wa kufanya hayo, ni hao hao au kutoka kwenye taasisi hizo hizo chafu dhidi ya demokrasia.

Mutungi, nasita hata kukutaja Jaji, kanuni za haki na neutrality unazifahamu? Umefanya kwa kutokufahamu au una dhamira chafu ndani yako?

Kama utaratibu wenyewe wa kuipata Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo huu wa kutumia watu wale wale waliokuwa wanaangamiza demokrasia, zoezi zima halima maana, ni upotezaji wa muda na fedha.

Ni tangu lini jambazi akaweka kanuni nzuri za kuzuia ujambazi?
Orodha ya tume ya michongo , mwenye nayo atupandishie hapa tafadhali.
 
Nimeona uteuzi wa hicho kinachoitwa "Kamati" umesainiwa na Mutungi; nikajiuliza, hilo ni jukumu la Msajili wa Vyama vya Siasa? Sikupata majibu. Pili, kurudisha mfumo wa kidemokrasia wa kufanya shughuli za siasa! Lol! Kumbe ulikuwa umepotea? Nini kilipelekea ukapotea? "Mashetani" wale wale waliopelekea ukapotea hawataupoteza tena? Assurance iko wapi kwamba sasa utadumu?

Lakini hili nalo ni kichekeso! Tangu lini haki ambazo ziko bayana kikatiba zikaundiwa kamati ya kuzijadili? Katiba na sheria za nchi ziko very clear kuhusu ufanyaji shughuli za kisiasa; hiyo Kamati ita-ammend Katiba na sheria au? Another wastage of time and resources!
Ni genge la wahuni tupu hapo
 
Ile ishu la Lipumba na genge lake pale CUF ilinifanya nimdharau huyo mzee kuliko toilet paper!! Inshort ni mtu wa hovyo sana!
Yule hakutakiwa kabisa kukalia ofisi Ile. Ukiangalia watangulizi wake kama Jaji Liundi hata na John Tendwa unamuona yeye viatu vyao vimempwaya. Badala ya kuwa mlezi wa vyama yeye amejitwika jukumu la kuviwajibisha hasa Chadema. Ni hovyo kabisa.
 
Yule hakutakiwa kabisa kukalia ofisi Ile. Ukiangalia watangulizi wake kama Jaji Liundi hata na John Tendwa unamuona yeye viatu vyao vimempwaya. Badala ya kuwa mlezi wa vyama yeye amejitwika jukumu la kuviwajibisha hasa Chadema. Ni hovyo kabisa.
Sio kiviwajibisha ila kuvinyonga 🤔.Anazo sifa za mlezi mchawi.
 
Yule hakutakiwa kabisa kukalia ofisi Ile. Ukiangalia watangulizi wake kama Jaji Liundi hata na John Tendwa unamuona yeye viatu vyao vimempwaya. Badala ya kuwa mlezi wa vyama yeye amejitwika jukumu la kuviwajibisha hasa Chadema. Ni hovyo kabisa.
Sioni huyu kuna kitu atajivunia hata siku akiondoka, zaidi ya unafiki. Ni mshirika mkuu katika kuua demokrasia.
 
Back
Top Bottom