July 19, 2019
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma, ameelezea ziara yao ndefu ya kikazi mikoa ya kanda ya ziwa iliyoanza mapema Julai 4, 2019. Mahakama imebaini aina ya adhabu zinazotolewa, kasi ya upelelezi na adhabu zinazotolewa.
Kutokana na hayo, Mh. Jaji Mkuu amekosoa mtindo wa wapelelezi na ofisi ya Mwendesha Mashitaka kufikisha kortini kesi wakati upelelezi haujakamilika.
Pia Jaji Mkuu ana maoni kuwa dhamana iwe ni haki kwa watuhumiwa wote na masharti ya dhamana yapunguzwe. Akaongeza kwa makosa madogo, hata kitambulisho cha uraia kiweze kutumika watuhumiwa wapate dhamana na kupunguza msongamano wa mahabusu.
Jaji Mkuu akatoa mfano wa hulka iliyojengeka ya 'kamata na sukuma ndani' ambayo inapelekea mahabusu na magereza kujaa watuhumiwa kupita kiasi.
Mh. Jaji Mkuu anashangaa hata kesi za madai / civil case kama za kandarasi pia amri hutolewa kuwa mkandarasi atupwe mahabusu wakati kuna taratibu na kanuni ya jinsi ya kushughulikia madai hayo kortini.
Jaji Mkuu Ibrahim Hamisi Juma ametoa mapendekezo kuwa, mamlaka zinazohusika na kutunga sheria za adhabu kutokushikilia kutunga sheria za adhabu kali, bali kuangalia kutunga sheria zinazoendana na uzito wa kosa husika.
Source : millard ayo
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma, ameelezea ziara yao ndefu ya kikazi mikoa ya kanda ya ziwa iliyoanza mapema Julai 4, 2019. Mahakama imebaini aina ya adhabu zinazotolewa, kasi ya upelelezi na adhabu zinazotolewa.
Kutokana na hayo, Mh. Jaji Mkuu amekosoa mtindo wa wapelelezi na ofisi ya Mwendesha Mashitaka kufikisha kortini kesi wakati upelelezi haujakamilika.
Pia Jaji Mkuu ana maoni kuwa dhamana iwe ni haki kwa watuhumiwa wote na masharti ya dhamana yapunguzwe. Akaongeza kwa makosa madogo, hata kitambulisho cha uraia kiweze kutumika watuhumiwa wapate dhamana na kupunguza msongamano wa mahabusu.
Jaji Mkuu akatoa mfano wa hulka iliyojengeka ya 'kamata na sukuma ndani' ambayo inapelekea mahabusu na magereza kujaa watuhumiwa kupita kiasi.
Mh. Jaji Mkuu anashangaa hata kesi za madai / civil case kama za kandarasi pia amri hutolewa kuwa mkandarasi atupwe mahabusu wakati kuna taratibu na kanuni ya jinsi ya kushughulikia madai hayo kortini.
Jaji Mkuu Ibrahim Hamisi Juma ametoa mapendekezo kuwa, mamlaka zinazohusika na kutunga sheria za adhabu kutokushikilia kutunga sheria za adhabu kali, bali kuangalia kutunga sheria zinazoendana na uzito wa kosa husika.
Source : millard ayo
Kamusi Ya Maneno Na Misemo Ya Kisheria | Kenya Law
kenyalaw.org