Jaji mkuu akamilisha jengo la mahakama kwa fedha alizotengewa yeye!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Jaji mkuu Ramadhan amewashangaza watu kwa kutumia pesa ambayo alipewa kukarabati nyumba yake na kuamua kwenda kukarabati jumba la kumbu kumbu ya Jaji mkuu wa kwanza wa Tanzania Bw. Said.

Sherehe hizo zimefanyika leo huku zikihudhuriwa na Waziri Mkuu na mjane mama Said ambaye alizindua sanamu ya mumewe.


mmmh swali langu hizo za kurekebisha nyumba yake atazipataje tena???
 
DAILY NEWS Reporter, 5th March 2010 @ 11:00, Total Comments: 0, Hits: 25

THE Judiciary today made a historic event since independence by inaugurating a 1.3bn/- worth of building in honour of the first indigenous Chief Justice (CJ) in Tanzania, the late Justice Augustine Saidi.

Prime Minister Mizengo Pinda officiated the inauguration ceremony held at the Court of Appeal premises along Kivukoni Front in Dar es Salaam. The Prime Minister praised the current Chief Justice Augustino Ramadhani for his initiatives to ensure the first CJ is honoured in such manner.

The premier was particularly excited by CJ Ramadhani for his decision of allocating funds designed to refurbish his residence and used the same for the construction of the new building that would be used by the country's Supreme Court as an administrative block.

Mr Pinda said what CJ Ramadhani did was a good example to civil and public servants. Time had come for leaders to emulate the same by not enriching themselves first and deal with others problems thereafter, he said.

Mr Pinda further said the spirit of remembering "learned brothers" like CJ Said should be maintained. He therefore thanked the judiciary for initiating the process at such right time.

Earlier, CJ Ramadhani told the premier and other invited guests, including the widow of the late Said, Mrs Elizabeth Said and her family members, retired justices and other judicial officers, that such practices were only observed for politicians in the country.

"We are now opening a new chapter in the country's judiciary. I take this opportunity to express my gratitude to then Court of Appeal Registrars Sophia Wambura and Ferdinand Wambali and the current court's Registrar Francis Mutungi for making this dream a reality," CJ Ramadhani said.

He said that he used resources of funds that were meant for renovation of his house as CJ and decided the money should be used to accomplish the mission to honour the first CJ for the benefit of the majority.

Since his appointment more than three years ago, Mr Ramadhani has not shifted into his designed residence as CJ because it has not been repaired as required. Justice Saidi was born on August 19, 1929 and died on April 19, 1995.

http://www.dailynews.co.tz/home/?n=7954&cat=home
 
Yaani jengo moja la Mahakama ambalo limeenda kufunguliwa na Waziri Mkuu.. lina gharama chini ya nyumba moja ya Gavana wa Benki au Naibu wake halafu tunatoa pongezi!? Hivi Jaji Mkuu wa Tanzania na Gavana wa Benki Kuu nani anaonesha kuijali nchi yake zaidi?

Huu ni uhuni mtupu... Hongera Jaji Ramadhani, kumbe nyumba ya Jaji bado inakalika na haogopi kutekwa kama somebody i know..
 
Leo asubuhi kwenye taarifa ta habari ya TBC walionyesha mahakama za mwanzo za huko Tanzania ni hatari sana, yaani majengo yake yanataka hata kuanguka je kwanini serikali isiongeze, Je kama mahakama zipo hivi je hali ya magereza yetu yapo vipi?? Kutakuwa na ukiukaji mkubwa sana ya haki za binadamu.
 
Yaani jengo moja la Mahakama ambalo limeenda kufunguliwa na Waziri Mkuu.. lina gharama chini ya nyumba moja ya Gavana wa Benki au Naibu wake halafu tunatoa pongezi!? Hivi Jaji Mkuu wa Tanzania na Gavana wa Benki Kuu nani anaonesha kuijali nchi yake zaidi?

Huu ni uhuni mtupu... Hongera Jaji Ramadhani, kumbe nyumba ya Jaji bado inakalika na haogopi kutekwa kama somebody i know..
Nitajaribu kutafuta picha za jengo moja la mahakama za mwanzo na pia kuna swali la muhimu la kujiuliza hapa ni kwamba, kama jengo hili tunajenga kwa gharama hii je huko mikoani itakuaje??
 
Nitajaribu kutafuta picha za jengo moja la mahakama za mwanzo na pia kuna swali la muhimu la kujiuliza hapa ni kwamba, kama jengo hili tunajenga kwa gharama hii je huko mikoani itakuaje??

kumbuka pia kuwa bila aibu Waziri Mkuu anatoa pongezi kwa Jaji Mkuu kupeleka fedha alizotakiwa ziende kwenye nyumba yake kujenga jengo hili. Yaani, serikali haikutenga fedha za jengo la kisasa la Mahakama ila wameenda kusherehekea Jaji Ramadhani kukubali kuendelea kukaa katika nyumba yake na kupisha fedha zilizotakiwa zifanyie matengenezo nyumba yake (kujenga bwawa, kuweka vifaa vya kisasa vya ulinzi, vitasa toka Uchina, mbwa wa kichina n.k) ziende huku!

Jaji Mkuu anastahili pongezi, serikali inastahli aibu!
 
Mwanakijiji,

We have a very few good men like Justice huyu. Angalau serikalini kungekua na watu wenye madaraka ya kuanzia wakurugenzi hadi mawaziri wenye akili na uwananchi na kujali Taifa kama 60 tu ambao wanafuata tabia kama huyu jaji tungekuwa dunia ya pili na sio ya mwisho.
 
Huu ni mfano mzuri wa kiongozi asiyejali maslahi binafsi,natamani viongozi wote wangejali ustawi wa jamii yetu kama jaji mkuu alivyofanya.,kuhusu atapata wapi pesa za kukarabati nyumba yake inawzekana amefanya hivyo kwa kuwa mwisho wa mwaka huu atastaafu so ataenda kwake na hiyo nyumba kwa kuwa ni ya serikali itakrabatiwa na serikali.
 
Angalau Jaji Agustino Saidi (RIP) amekumbukwa. Huyu alipostaafu, alikwenda kuishi kwenye nyumba yake ya kawaida, Msasani Mikoroshini, nyuma ya flats za Drive -In with his Peogeot 404!.

Agustino Saidi ndie alikuwa Advocate wa kwanza mzawa Tanzania huru, kabla ya hapo walikuwa ni wazungu tuu.

He was totally Nyerere type mpaka kifo kilipomuita.

Ifuatayo ni just an amaizing Coincidence.

Yeye na Agustino Ramadhani, wanafafana kwa mengi.
1. Majina yao ya kwanza wote ni jina la Agustino.
2. Majina yao ya kwanza wote ni ya Kikristo
3. Majina yao ya pili wote ni ya Kiislamu, mmoja akiitwa Saidi, mwingine akiitwa Ramadhani.
4, Wote ni Wakristo wachaMungu, Agustino Saidi akihudumu St. Peters na familia yake yote, Agustino Ramadhani akihudumu na mpaka kupiga piano St. Albans.
5. Wote ni majaji Wakuu wa Tanzania wakihudumu chini ya maraisi wenye majina ya JK,
Jaji Saidi chini ya Julius Kambarage, Jaji Ramadhani chini ya Jakaya Kikwete.
 
Kwa mfano huu, kumbe bado tuna watu wanaofikiria boldly in Tanzania? Maana waliowengi hawatosheki kabisa.
 
Mwanakijiji,

We have a very few good men like Justice huyu. Angalau serikalini kungekua na watu wenye madaraka ya kuanzia wakurugenzi hadi mawaziri wenye akili na uwananchi na kujali Taifa kama 60 tu ambao wanafuata tabia kama huyu jaji tungekuwa dunia ya pili na sio ya mwisho.

FP.. alichofanya Jaji Mkuu ni kuimbua serikali; na ndio maana amesema hadharani kuwa fedha zilizotumika zilikuwa ni kwa ajili yake lakini yeye hakuzitumia kujijengea nyumba ya mbinguni duniani wakati kuna mtu katika historia yetu hata kukumbukwa hakumbukwi! Angeweza kumezea tu.. serikali ingejipa ujiko!!!
 
Kitu kingine cha kukiangalia sana kwenye construction industry ni tabia ya kuongezea gharama halisi za project ili baadhi ya watu wapate ten % zao. Ndio maana unaona ukarabati tu wa nyumba unaweza kujenga nyumba nyingine kumi bila wasiwasi wowote.
Nafikiri umefika muda muafaka sasa wa kuanza kuangalia hizi mega projects kama zinajengwa na gharama halisi au la.
 
Kitu kingine cha kukiangalia sana kwenye construction industry ni tabia ya kuongezea gharama halisi za project ili baadhi ya watu wapate ten % zao. Ndio maana unaona ukarabati tu wa nyumba unaweza kujenga nyumba nyingine kumi bila wasiwasi wowote.
Nafikiri umefika muda muafaka sasa wa kuanza kuangalia hizi mega projects kama zinajengwa na gharama halisi au la.

Ndahani.. binafsi ningependa kuliona hilo jengo la Justice Said na kulinganisha na ile nyuma ya Gavana wetu.. haiwezekani kwenye mji mmoja kwa kiasi karibu kile kile kuwe na tofauti kubwa sana ya kiile unachoweza kufanya na fedha ziile zile.
 
Ndahani.. binafsi ningependa kuliona hilo jengo la Justice Said na kulinganisha na ile nyuma ya Gavana wetu.. haiwezekani kwenye mji mmoja kwa kiasi karibu kile kile kuwe na tofauti kubwa sana ya kiile unachoweza kufanya na fedha ziile zile.
Nafikiri mchango wa CRB na EBR na collaboration ya makampuni ya ujenzi ni vital sana kwa hilo. Sasa hivi mtoaji mkubwa wa tender za ujenzi ni serikali na taasisi zake. Lakini mpaka uje kuzipata hizo project ni issue.
Ndio maana hata kampuni kama Estim inaangaliwa kwa shaka shaka hivi maana kuanzia multifuction hall ya ikulu mpaka, na majengo mengine makubwa karibu yote kwenye hii awamu ya nne anapewa yeye. Hivi hakuna wakandarasi wa ndani wengine?
 
Nafikiri mchango wa CRB na EBR na collaboration ya makampuni ya ujenzi ni vital sana kwa hilo. Sasa hivi mtoaji mkubwa wa tender za ujenzi ni serikali na taasisi zake. Lakini mpaka uje kuzipata hizo project ni issue.
Ndio maana hata kampuni kama Estim inaangaliwa kwa shaka shaka hivi maana kuanzia multifuction hall ya ikulu mpaka, na majengo mengine makubwa karibu yote kwenye hii awamu ya nne anapewa yeye. Hivi hakuna wakandarasi wa ndani wengine?

Huwa najua kuwa ni ya PATEL au ROSTAM kumbe wakurugenzi ni Gilabhadi Pindolia na Jianesh Mandwama. reference ktaba wa ujenzi wa jengo la UVCCM.
 
Wengi kumbe hamumjui huyu Jaji Mkuu. Huyu ni mwanasiasa. Hapa anacheza politics kwa sababu ana malengo yake ya kisiasa baada ya kustaafu mwisho wa mwaka. Sintashangaa mweiz Aprili akitoa hukumu ya kuruhusu wagombea binafsi. He is from Zanzibar. One time in the past aliwahi kugombea Urais kama sikosei.
 
Acheni zenu huyu jamaa ameonyesha respect safi sana Tino tuko pamoja na wewe
 
Wengi kumbe hamumjui huyu Jaji Mkuu. Huyu ni mwanasiasa. Hapa anacheza politics kwa sababu ana malengo yake ya kisiasa baada ya kustaafu mwisho wa mwaka. Sintashangaa mweiz Aprili akitoa hukumu ya kuruhusu wagombea binafsi. He is from Zanzibar. One time in the past aliwahi kugombea Urais kama sikosei.
hata kama ni mwanasiasa, lakini kitendo cha yeye kubana matumizi au kuzuia matumizi kwa mambo yasiyo na tija anapaswa kupongezwa.
kwanini aishi maisha yenye kufuru katika lindi na umasikini kama huu, heri kaamua kufanya jambo lingine kwa faida ya UMMA.
wangapi wanaweza kukubali kuishi maisha ya kawaida ili kuinufaisha jamii yao ? wachache sana.
nafikiri mawazo yako yamejaa kutu, sioni mantinki ya wewe kutoona mantinki ya Jaji Mkuu.
 
Back
Top Bottom