Elections 2010 Jaji Mfalila: Chagueni upinzani ASEMA MGOMBEA ATAYETOA ELIMU, AFYA BURE NDIYE ANAFAA

Maoni kama haya kutoka kwa watu wanaoheshimika katika jamii yanasaidia kuondoa wasiwasi kwa wananchi juu ya upinzani kama inavyo chakanuliwa na mafisadi wenye wivu wa kuona wenzao wana elimika na kupata ufahamu juu ya ukweli wa mambo yanavyotakiwa kuwa.

Inawezekana Serikali kutoa huduma za afya bure- Jaji Mfalila
· Ashangaa wanasiasa wanaodai haiwezekani

Na Charles Lucas
22 September 2010

JAJI mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Lameck Mfalila amesema inawezekana serikali kutoa huduma za afya bure endapo wanasiasa watakuwa na dhamira ya kweli kutekeleza jambo hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tamko la Wanaharakati Wasio wa Kiserikali kuhusu Uchaguzi Mkuu, jijini Dar es Salaam jana Jaji Mfalila aliwaponda baadhi ya wanasiasa wanaowabeza wenzao kwa maelezo kwamba haiwezekani serikali kutoa huduma za afya bila malipo na kuwataka kuacha kupinga jambo hilo.

Alisema Tanzania ina rasilimali za kutosha yakiwemo madini ya kila aina na mengine hayapatikani sehemu yoyote duniani hivyo ni wajibu wa serikali kuyatumia vizuri ili yagharamie huduma zingine.

"
Nimesikia sikia mgombea mmoja wa chama kimoja cha siasa ametamka kuwa atatoa huduma za afya bure kwa Watanzania, asibezwe hilo linawezekana ikiwa maadili ya matumizi ya rasilimali za taifa yatazingatia," alisema Jaji Mfalila na kuongeza; "Wanakojeli kauli hizo wana mapungufu ya uongozi au hawana ufahamu," alisema Jaji Mfalila huku akishangiliwa kwa mguvu na washiriki wa mkutano huo.

"Kama zipo ahadi nyingi zinazotolewa na zinatekelezeka kwanini hii moja ya kutoa huduma bure isitekelezeke?" Alihoji.

Alisema inasikitisha kwamba baadhi ya viongozi wanaopinga jambo hilo alisoma nao kuanzia hadi chuo kikuu na walipewa huduma zote bure kuanzia matibabu hadi elimu lakini leo wanapinga jambo hilo kuwa haliwezekani.

Aliendelea kusema Tanzania haistahili kuwa na njaa kutokana na rasilimali kubwa ya mabonde ya kilimo yenye rutuba yanayoweza kuzalisha chakula cha kutosha kwa wananchi wake.

"Mfano Japan ina ardhi ndogo inayofaa kwa kilimo ukilinganisha na Tanzania, ni aibu kwenda kuomba chakula wakati tuna mabonde yenye rutuba ya kuweza kuzalisha vyakula kama Rufiji."

Jaji Mfalila alisema kiongozi hatakiwi kuhamasisha wananchi kwamba misaada ndio majibu ya matatizo yao bali anapaswa kutengeneza mipango na kuwahamasisha kujenga mazingira ya kuwafanywa wajione wana wajibu wa kuwajibika kwa maendeleo ya taifa lao.

"Kitendo cha kuweka mawazo kwenye misaada kinaondoa fikra za kujiamini kwamba sisi wenyewe tunaweza kujitegemea bila kuomba," alisema.

Alisema uchumi wa nchi hauwezi kukua kama hakuna hazina ya kutosha ya madini ndani ya Benki Kuu na kulaumu mtindo wa serikali kupokea mrahaba wa asilimia tatu jambo linaloonesha wazi kunyonywa na wawekezaji.

"Kuna wakati, Bw. Mrema (Augustino) alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu, alichukua jukumu la kununua dhahabu na kuipeleka Benki Kuu, alikusanya kilo 16. Nashangaa kwanini serikali iliondoa utaratibu huo. Ingekuwa afadhali kama katika kila kilo 100 anazochimba mwekezaji serikali ipate walau kilo moja."

Alifafanua kuwa nchi inapokuwa na akiba ya dhahabu, uchumi wake unakuwa mzuri lakini inasikitisha kwamba pamoja na madini hayo hatuna akiba ya kutosha na tunaishia kupata mrahaba wa asilimia tatu ambao si chochote.

Alisema kitendo hicho kimewapa nafasi baadhi ya wawekezaji ambao si waaminifu wanaotumia udhaifu wa mikataba iliyopo kujinufaisha wenyewe na kunukuu kauli ya Mwalimu Nyerere kuonya kupokea ushauri usio na maana.

"
Mwalimu alisema mtu mjinga akikushauri jambo la kijinga na wewe ukalikubali wewe utakuwa mjinga zaidi," alisema Jaji Mfalila na kuwataka viongozi wawe makini wanapopewa ushauri.

Akizungumzia Uchaguzi Mkuu alisema unatoa nafasi adhimu kwa wapiga kura na wagombea kukumbuka malengo ya misingi ya mfumo wa uchaguzi ni kuweka mbele na kulinda maslahi ya taifa.

Alisema kunatakiwa kuwepo mchakato wa uchaguzi wenye uwazi haki na amani unaopinga aina zote za vitisho, rushwa, mizengwe au hila za kupindisha ushindi utokanao na kura halali za wananchi na uzingatia misingi ya kidemokrasia.

Alisema Tanzania inayotakiwa kuwa taifa lenye amani na maendeleo ambalo linaheshimu haki za wananchi wake bila kujali jinsia, hadhi, dini, kabila, imani ya kundi fulani na uwezo kimwili ama kiuchumi.

"Tunataka Tanzania ambayo licha ya kutokuwa na wala rushwa inaendeshwa na viongozi wenye uvumilivu na uadilifu wenye kutumia ipasavyo maliasili na rasilimali hususani watu.

"Tunataka Tanzania inayojitosheleza kwa chakula miundombinu bora yenye misingi ya kiteknolojia na yenye kutafsiri maendeleo ya kitaifa kwa kuangalia afya, elimu, na ustawi wa jamii. Tunaomba wananchi wayasimamie haya na kuyafautilia kwa sababu Tanzania tunayoitaka inawezekana," alisema Jaji Mfalila.

 
Nimefurahiswa sana na kauli ya msomi Jaji Mfalila. Tunategemea kusikia zaidi kutoka kwake na wasomi wengine ili kuwafunga mdomo akina Kinana na Sitta. Mungu ibariki Tanzania. Inshallah tutafika.
 
[/SIZE]

kwa heshima ya waee hawa wawili waliomaua kuweka unafiki pembeni na kusema ukweli kwa mujibu wa Katiba yetu. Nawaomba watanzania [/SIZE]
wote waliosoma Shule za Msingi, Middle School, Secondary Schools na Vyuo Vikuu vya hapa nyumbani na nje ya nchi buree katika utwala wa Mwalimu Nyerere watupatie taarifa kidogo hali ilikuwaje wakati huo? Natambua Mwalimu Nyerer alikuwa akiheshimu sna Katiba ya Nchi, na Haki ya Kupata Elimu Katina inatamka

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Sehemu ya Tatu ya Kifungu ya cha 11 kinasema kuwa “serikali itafanya jitihada kuhakikisha kwamba watu wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo vinginevyo vya mafunzo”.

Naomba mtueleze yafuaatyao:-
a) Mazingira ya shule, vyuo yalikuwaje?
b) Mlikuwa mkisafiri kwa gharama za nani kutoka majumbani hadi mashuleni, vyuoni n.k?
c) Mazingira ya mabweni, chakula katika hizo shule na vyuo vilikuwaje?

Taarifa za aina hii zitachangia kuwapatia picha halisi vijana wetu walioko mashuleni na vyuoni kwa sasa, na hivyo kuwasaidia kupima kwa makini kama wanapata Haki zao za Kikatiba za Elimu hivi sasa.

Hii ni muhimu sana, kwani CCM imewafanya watanzania wengi kuamini kuwa elimu duni inayotolewa hapa nchini tena katika mazingira duni sana ni hisani kutoka viongozi wa CCM na chama hicho na sio haki ya msingi ya Mtanzania kwa mujibu wa Katiba.
Jatropha,
Umeuliza elimu ilikuwaje enzi za Mwalimu. Wakati Jaji Mfalila akiwa sekondari mimi nilikuwa middle school. Tulipewa vitabu, peni na waliokaa mabwenini chakula kilikuwa bure. Wakati shule zinafungwa tulipewa warranti za kupanda treni/meli/mabasi kwenda nyumbani vijijini na kurudi. Pale shuleni kwetu waalimu walikuwa na nyumba nzuri, jioni tukienda kwao kusikiliza redio. Kila mwanafunzi alikuwa na dawati lake. Of course chakula cha shule ni cha shule tu. Tulikula dona na maharage, halafu wikendi tunapewa wali na nyama. Shule nyingine nasikia, kama vile Bwiru, walikuwa na chai na mkate saa kumi jioni. Nadhani hilo jibu linakupa picha ya kutosha.
 
Haya sasa tunaona waliofaidika na sera ya elimu iliyo bure kwa wote kama Jaji L. Mfalila , Prof. Chris Maina Peter, Prof. Lipumba, Dakta Slaa wote wanaona 'ndiyo inawezekana elimu bure kwa wote'.

Swali:
  1. Kwa nini mgombea Urais kwa CCM Mh. Dakta Jakaya Mrisho Kikwete anaona haiwezekani?
  2. Pia kwa Nini wagombea ubunge wa CCM waliosomeshwa buree kama Mustafa Mkulo, Basil Mramba, Bernard Membe, Dr. Nagu, Dr. Buriani, Dr. Mwakyembe, Prof. Mwandosya na wengine wote wa CCM wanasema haiwezekani ?
  3. Wagombea Udiwani wa CCM kwa nini wanaona elimu na huduma za afya haziwezi kuwa bure kwa wote?

Mkuu hiyo kwenye nyekundu,Kikwete anasema haiwezekani kutokana na mianya ya ukwepaji wa kodi nawizi wa maliasili zetu anaoijua na hawezi kuishughulikia kwa kuwa aidha naye ni mnufaika ama inafanywa na rafiki zake wa karibu sana kama akina Rostam Azizi (Caspian, Kampuni ya uwindaji etc), Mohammed Dewji, Somaia (nasikia ndo kanunua hiyo helkopta anayotumia kwenye kampeni), Lowasa (Richmond, Kampuni ya upakuaji mizigo bandarini - TICS), Karamagi (Kampuni ya upakuaji mizigo bandarini - TICS), Kinana (Meli za mizigo), n.k ambao hawezi kuwaambia kitu. Vilevile tumeona amesaini mikataba mibovu inayoinyonya nchi ikiwemo ya madini na makampuni ya kuzalisha umeme (IPTL, Agreko etc) yanayoifilisi nchi na hawezi kufanya chochote. Kwa mtu kama Slaa asiye na ubia na mianya hii ya kuikosesha serikali mapato akiiziba tu na kuwa mkali kwa TRA hela ziko bwelele za kuweza kufanya mambo makubwa sana ya maendeleo kwa nchi yetu.
 
JAJI mstaafu wa Mahakama ya Rufaa nchini, Lameck Mfalila, amewataka Watanzania kuchagua mgombea aliyethubutu kusema; "atasomesha wanafunzi na kutoa huduma ya afya bure." Akitetea msimamo huo, Jaji Mfalila alisema:"Huyu ni shujaa, sio ghilba bali amethubutu kusema anaweza kufanya mabadiliko hayo, mchagueni."

Katika mkutano wa wanaharakati kuhusiana na Uchaguzi Mkuu jijini Dar es Salaam jana, Jaji Mfalila alitoa sifa kwa mgombea mmojawapo wa urais kutoka kambi ya upinzani ambaye ameweka wazi kwamba akiingia Ikulu, elimu na afya zitatolewa bure.
 
Inawezekana Serikali kutoa huduma za afya bure- Jaji Mfalila


PostDateIcon.png
Wednesday, 22 September 2010 05:45
  • Ashangaa wanasiasa wanaodai haiwezekani
Na Charles Lucas

JAJI mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Lameck Mfalila amesema inawezekana serikali kutoa huduma za afya bure endapo wanasiasa watakuwa na dhamira ya kweli kutekeleza jambo hilo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tamko la Wanaharakati Wasio wa Kiserikali kuhusu Uchaguzi Mkuu, jijini Dar es Salaam jana Jaji Mfalila aliwaponda baadhi ya wanasiasa wanaowabeza wenzao kwa maelezo kwamba haiwezekani serikali kutoa huduma za afya bila malipo na kuwataka kuacha kupinga jambo hilo.

Alisema Tanzania ina rasilimali za kutosha yakiwemo madini ya kila aina na mengine hayapatikani sehemu yoyote duniani hivyo ni wajibu wa serikali kuyatumia vizuri ili yagharamie huduma zingine.

" Nimesikia sikia mgombea mmoja wa chama kimoja cha siasa ametamka kuwa atatoa huduma za afya bure kwa Watanzania, asibezwe hilo linawezekana ikiwa maadili ya matumizi ya rasilimali za taifa yatazingatia," alisema Jaji Mfalila na kuongeza; "Wanakojeli kauli hizo wana mapungufu ya uongozi au hawana ufahamu," alisema Jaji Mfalila huku akishangiliwa kwa mguvu na washiriki wa mkutano huo.

"Kama zipo ahadi nyingi zinazotolewa na zinatekelezeka kwanini hii moja ya kutoa huduma bure isitekelezeke?" Alihoji.

Alisema inasikitisha kwamba baadhi ya viongozi wanaopinga jambo hilo alisoma nao kuanzia hadi chuo kikuu na walipewa huduma zote bure kuanzia matibabu hadi elimu lakini leo wanapinga jambo hilo kuwa haliwezekani.

Aliendelea kusema Tanzania haistahili kuwa na njaa kutokana na rasilimali kubwa ya mabonde ya kilimo yenye rutuba yanayoweza kuzalisha chakula cha kutosha kwa wananchi wake.

"Mfano Japan ina ardhi ndogo inayofaa kwa kilimo ukilinganisha na Tanzania, ni aibu kwenda kuomba chakula wakati tuna mabonde yenye rutuba ya kuweza kuzalisha vyakula kama Rufiji."

Jaji Mfalila alisema kiongozi hatakiwi kuhamasisha wananchi kwamba misaada ndio majibu ya matatizo yao bali anapaswa kutengeneza mipango na kuwahamasisha kujenga mazingira ya kuwafanywa wajione wana wajibu wa kuwajibika kwa maendeleo ya taifa lao.

"Kitendo cha kuweka mawazo kwenye misaada kinaondoa fikra za kujiamini kwamba sisi wenyewe tunaweza kujitegemea bila kuomba, " alisema.

Alisema uchumi wa nchi hauwezi kukua kama hakuna hazina ya kutosha ya madini ndani ya Benki Kuu na kulaumu mtindo wa serikali kupokea mrahaba wa asilimia tatu jambo linaloonesha wazi kunyonywa na wawekezaji.

" Kuna wakati, Bw. Mrema (Augustino ) alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu, alichukua jukumu la kununua dhahabu na kuipeleka Benki Kuu, alikusanya kilo 16. Nashangaa kwanini serikali iliondoa utaratibu huo. Ingekuwa afadhali kama katika kila kilo 100 anazochimba mwekezaji serikali ipate alau kilo moja."

Alifafanua kuwa nchi inapokuwa na akiba ya dhahabu, uchumi wake unakuwa mzuri lakini inasikitisha kwamba pamoja na madini hayo hatuna akiba ya kutosha na tunaishia kupata mrahaba wa asilimia tatu ambao si chochote.

Alisema kitendo hicho kimewapa nafasi baadhi ya wawekezaji ambao si waaminifu wanaotumia udhaifu wa mikataba iliyopo kujinufaisha wenyewe na kunukuu kauli ya Mwalimu Nyerere kuonya kupokea ushauri usio na maana.

" Mwalimu alisema mtu mjinga akikushauri jambo la kijinga na wewe ukalikubali wewe utakuwa mjinga zaidi," alisema Jaji Mfalila na kuwataka viongozi wawe makini wanapopewa ushauri.



Akizungumzia Uchaguzi Mkuu alisema unatoa nafasi adhimu kwa wapiga kura na wagombea kukumbuka malengo ya misingi ya mfumo wa uchaguzi ni kuweka mbele na kulinda maslahi ya taifa.

Alisema kunatakiwa kuwepo mchakato wa uchaguzi wenye uwazi haki na amani unaopinga aina zote za vitisho, rushwa, mizengwe au hila za kupindisha ushindi utokanao na kura halali za wananchi na uzingatia misingi ya kidemokrasia.

Alisema Tanzania inayotakiwa kuwa taifa lenye amani na maendeleo ambalo linaheshimu haki za wananchi wake bila kujali jinsia, hadhi, dini, kabila, imani ya kundi fulani na uwezo kimwili ama kiuchumi.

"Tunataka Tanzania ambayo licha ya kutokuwa na wala rushwa inaendeshwa na viongozi wenye uvumilivu na uadilifu wenye kutumia ipasavyo maliasili na rasilimali hususani watu.

"Tunataka Tanzania inayojitosheleza kwa chakula miundombinu bora yenye misingi ya kiteknolojia na yenye kutafsiri maendeleo ya kitaifa kwa kuangalia afya, elimu, na ustawi wa jamii. Tunaomba wananchi wayasimamie haya na kuyafautilia kwa sababu Tanzania tunayoitaka inawezekana," alisema Jaji Mfalila.
 
Viongozi wa CCM wanaodai haiwezekani kutoa huduma za afya bure wana sifa zifuatazo:

(1) Wana uwezo wa kujilipia huduma za afya lakini wakiugua hutibiwa nje BURE (kwa fedha za serikali).

(2) Walilelewa kwenye taifa lenye huduma za afya za bure.

(3) Wanatenga kiasi kikubwa sana cha fedha za walipakodi kwa ajili ya anasa zao (eg. 30bn/- kwa ajili ya chai).

(4) Wakinunua dawa hupeleka risiti serikalini na kurudishiwa gharama zao.

(5) Familia zao zinatibiwa bure (kwa fedha za serikali) kwenye hospitali nzuri kama Aga Khan.

Ndugu zangu; wanachosema viongozi wa CCM ni tiba bure kwa wote hapana. Ni kwa ajili yao tu.
 

" Mwalimu alisema mtu mjinga akikushauri jambo la kijinga na wewe ukalikubali wewe utakuwa mjinga zaidi," alisema Jaji Mfalila na kuwataka viongozi wawe makini wanapopewa ushauri.

.


That sums up everything... wajinga wanataka tuamini na kukubali mambo yao ya kijinga!!! tukatae kuwa wajinga, enough is enough

Naumia sana kusikia watoto wa akina kinana wanasoma South Africa, Mke wa January kajifungulia marekani, Chenge anapeleka suti kufuliwa ulaya nk

halafu wanasema afya ya bure haiwezekani wakati afisa wa kati anatumia gari ya milioni mia mbili, anaishi kibamba na dereva anaishi mbagala na kila siku gari inazunguka na kutumia mafuta ya 60,000 kupeleka mtu kazini na kurudi

sad

well said jaji mfalila
 
Back
Top Bottom