Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,793
- 12,238
Kitendo cha Jaji Joachim Tiganga aliyekuwa anasikiliza kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe na wenzake watatu kuamua kuwa wana kesi ya kujibu na baadaye serikali kupitia kwa DPP kusema hawana nia ya kuendelea na kesi kimeidhalilisha sana mahakama.
Endapo Jaji Tiganga angemaliza kesi hii mara baada ya Jamuhuri kumaliza ushahidi wake kwa kuamua kuwa akina Mbowe na wenzake hawana kesi ya kujibu, mahakama ingejijengea heshima kubwa sana kwa Watanzania na Dunia kwa ujumla. Hivi sasa mahakama imedhihirisha haiko huru na inategemea maoni ya serikali kuamua kesi.
Udhaifu huu wa mahakama umemfanya Samia kuwa shujaa (heroine) na kijizolea sifa asizostahili ndani na nje ya nchi. Sifa ambazo mahakama ingezipata kama ingetoa hukumu ya haki.
Jaji Mkuu anapaswa kujitafakari sana na hasa kwa kauli yake ya kuwataka majaji kutoa hukumu kwa kuzingatia maoni ya Jamuhuri.
Endapo Jaji Tiganga angemaliza kesi hii mara baada ya Jamuhuri kumaliza ushahidi wake kwa kuamua kuwa akina Mbowe na wenzake hawana kesi ya kujibu, mahakama ingejijengea heshima kubwa sana kwa Watanzania na Dunia kwa ujumla. Hivi sasa mahakama imedhihirisha haiko huru na inategemea maoni ya serikali kuamua kesi.
Udhaifu huu wa mahakama umemfanya Samia kuwa shujaa (heroine) na kijizolea sifa asizostahili ndani na nje ya nchi. Sifa ambazo mahakama ingezipata kama ingetoa hukumu ya haki.
Jaji Mkuu anapaswa kujitafakari sana na hasa kwa kauli yake ya kuwataka majaji kutoa hukumu kwa kuzingatia maoni ya Jamuhuri.