Jaji Damian Lubuva katika mtego mzito wa kutangua SHERIA na HAKI

chachana

Member
Aug 4, 2011
57
92
Vikao vimekuwa vizito vya tume ya uchaguzi kufuatia utata wa uraia wa mgombea wa CCM. Hali hiyo imeibuka kufuatia uhalisi wa kisheria kuwa SIOI hakuwa kuukana uraia wa kenya ambao aliupata kwa kuzaliwa nchini humo.

Jaji Lubuva inasemekana ameelezea mtego huo kuwa, kwa mazingira ya kawaida Wazazi wa SIOI ni watanzania hata yeye ni mtanzania lakini kisheria alitakiwa kuukana uraia wa kenya alipofika miaka 18 kwa sababu aliupata kwa kuzaliwa nnchini humo. Jambo hili watu wengi waliozaliwa nje hulisahau kabisa kwa sababu za kawaida kabisa kuwa wazazi ni watanzania na kuacha sheria kutimiza matakwa ya sheria.

Uhalisi wa suala hili kisheria ni kuwa mgombea SIOI SUMARI hakuwahi popote kuukana uraia wa kenya na kuchukua uraia wa watanzaia. Jaji lubuva ameendelea kukuna kichwa na viongozi wa ccm wameendelea kutengeneza sababu na kujaribu kutengenza viambatanisho ambavyo mpaka kufika mchana wa leo jaji lubuva hakuwa amekubaliana nao kwa vile huu ni mtihani mkubwa sana kwa Lubuva kuhusu kusimamia haki na sheria na kitendo cha kupindisha sheria katika hatua hizi za mwanzo ni kama kujifukuzisha kazi mapema.
 
Hapo jaji Lubuva ndio tutaona anasimamia kwenye nini mazoea ama sheria maana hao CCM wamezoea kupindisha sheria na matokeo yake ndio kama yale ya uteuzi wa meya ya Arusha. Ni juu yako Lubuva kujenga imani kwa watanzania au kwa CCM
 
Kwa CCM yote yawezekana. Kama walipitisha sheria ya uchaguzi, wakaivunja na Puppet wao msajiri akabariki uvunjwaji huo, itakuwa hili la kusema ni raia ama la! Mbona mkurugenzi wa uhamiaji keshasema ni raia sababu wazazi wake wote ni raia.
 
Kwa CCM yote yawezekana. Kama walipitisha sheria ya uchaguzi, wakaivunja na Puppet wao msajiri akabariki uvunjwaji huo, itakuwa hili la kusema ni raia ama la! Mbona mkurugenzi wa uhamiaji keshasema ni raia sababu wazazi wake wote ni raia.

kama umetumwa hivyo imekuLa kwako. Tayari tume ya uchaguzi pasipo shaka imejiridhisha na kuthibitisha kuwa sumari hana uraia wa Tanzania wala ule wa Kenya. Habari walizozipata toka uhamiaji kenya zinasema hakuna sehemu yoyote Sumari aliukana uraia wa Tanzania alipofikisha miaka 22 na hivyo kukosa sifa ya kuwa mkenya. Vile vile anaonekana kumiliki passport ya Kenya isivyo halali na analipaswa kufukuzwa nchi Kenya maramoja. vile vile hata hapa Tanzania hakufanya hivyo kwa uraia wa kenya alipofikisha miaka 18 anapaswa kufukuzwa mara moja.
 
Vikao vimekuwa vizito vya tume ya uchaguzi kufuatia utata wa uraia wa mgombea wa CCM. Hali hiyo imeibuka kufuatia uhalisi wa kisheria kuwa SIOI hakuwa kuukana uraia wa kenya ambao aliupata kwa kuzaliwa nchini humo.

Jaji Lubuva inasemekana ameelezea mtego huo kuwa, kwa mazingira ya kawaida Wazazi wa SIOI ni watanzania hata yeye ni mtanzania lakini kisheria alitakiwa kuukana uraia wa kenya alipofika miaka 18 kwa sababu aliupata kwa kuzaliwa nnchini humo. Jambo hili watu wengi waliozaliwa nje hulisahau kabisa kwa sababu za kawaida kabisa kuwa wazazi ni watanzania na kuacha sheria kutimiza matakwa ya sheria.

Uhalisi wa suala hili kisheria ni kuwa mgombea SIOI SUMARI hakuwahi popote kuukana uraia wa kenya na kuchukua uraia wa watanzaia. Jaji lubuva ameendelea kukuna kichwa na viongozi wa ccm wameendelea kutengeneza sababu na kujaribu kutengenza viambatanisho ambavyo mpaka kufika mchana wa leo jaji lubuva hakuwa amekubaliana nao kwa vile huu ni mtihani mkubwa sana kwa Lubuva kuhusu kusimamia haki na sheria na kitendo cha kupindisha sheria katika hatua hizi za mwanzo ni kama kujifukuzisha kazi mapema.
Kufukuzwa kazi kwa Tanzania si rahisi ila sema atakuwa anaidhalilisha taaluma yake.
 
Lubuva inampasa achukuwe precedent ya uraia wa Azim Premji wa Kigoma katika rufaa ya Kabourou mwaka 1994. CJ Nyalali aliona kasoro ya uraia wa Premji hivyo kumuengua ubunge.
 
hili jukwaa inaelekea hamjajua vizuri mbinu na mikakati ya ccm,. hivi kuna mtu anategemea jaji Lubuva mteule wa JK mwenyekiti wa CCM atamke kuwa Sioyi mteule wa ccm mkwe wa Lowassa sio raia na amwondoe kwenye kugombea ujbumbe Arumeru mashariki?? That will never happen hakuna hata haja ya kusubiri,Sioyi sana sana itumike nguvu na akili nyingi sana kumwengua kwa njia ya kura lakini mkondo huu wa kisheria wa Tanzania umepinda sana haufai kutegemewa!!
 
Back
Top Bottom