Jaji Bomani: Wageni wanaimaliza nchi kupitia sekta ya madini

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
jaji-mark-bomani.jpg


Mwenyekiti wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za

Madini Serikalini (TEITI), Jaji Marck Bomani



MWENYEKITI wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za Madini Serikalini (TEITI), Jaji Marck Bomani, amesema wageni wanazidi kuimaliza nchi kupitia sekta ya madini, yakiwa ni matokeo ya sheria mbovu. Jaji Bomani imeishauri Serikali kubadilisha haraka sheria zilizopo kuhusu sekta hiyo ili kuwawezesha wananchi kujua kila kinachopatikana kutokana na raslimali hiyo.

Alisema uchimbaji wa madini utaendelea kuwanufaisha wageni kwa kuhamishia fedha na madini nchi za nje na kwamba hilo linatokana sheria zilizopo kuwapa mwanya.Jaji Bomani alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika warsha ya uelimishaji na uhamasishaji umma juu ya taarifa ya kwanza ya ulinganisho wa malipo na mapato kutoka kampuni za uchimbaji madini na gesi asili, katika mwaka wa fedha 2008/2009 iliyofanyika jijini Tanga

Alisema ni jambo la kushangaza kuona Tanzania pekee ikitoa mwanya kwa wawekezaaji kuchimba madini na kuyasafirisha nje kwa ajili ya kuyauza.Jaji Bomani alisema mabaya zaidi makampuni hayo yametakiwa kulipa kodi baada ya kuondoa gharama zote za uendeshaji au uzalishaji. Hakuna mfanyabiashara anayeweza kusema ukweli juu ya faida ganayoipata kutokana na kuchimba madini, haiwezekani Tanzania tuendelee kuwa masikini wakati madini yetu yanayotoka yangeweza kusukuma mbele maendeleo yetu,alisema Bomani.

Alisema katika taarifa ya awali imebainika kuwa uchambuzi uliofanyika kuna tofauti kubwa ya taakribani zaidi ya Sh 46 bilioni kati ya malipo yaliyodaiwa kulipwa na kampuni na fedha iliyopokelewa serikalini. Akiwasilisha mada ya mtizamo wa wadau na jamii juu ya ripoti ya kwanza ya TEITI na matarajio ya ripoti ya pili, mjumbe wa kamati hiyo, Askofu Stephen Munga alisema unahitajika uzalendo wa hali ya juu kwa viongozi waliopewa madaraka ya kuwaongoza wananchi.

Alisema haiwezekani rasilimali ya nchi kuendelea kuvunwa na kutoroshwa nje ya nchi kijanja na kuwanufaisha wageni huku Watanzania wakiendelea kuwa masikini na kwamba ni lazima hatua za makusudi za kuinusuru nchi zichukuliwe.
 
Huyu naye amesomea uchumi wapi? Watanzania bwana mwanasheria anaongelea uchumi, mchumi anaongelea siasa, mwanasiasa anaongelea dini, padri/sheikh anaongelea siasa.... bora kila ki2 shaghala baghala mimi sijaona statement ya maana aliyoongea huyu jaji mstahafu.... NB: Alikuwa kwenye at least commercial court? mmmhhhhh galagabaho....
 
Huyu naye amesomea uchumi wapi? Watanzania bwana mwanasheria anaongelea uchumi, mchumi anaongelea siasa, mwanasiasa anaongelea dini, padri/sheikh anaongelea siasa.... bora kila ki2 shaghala baghala mimi sijaona statement ya maana aliyoongea huyu jaji mstahafu.... NB: Alikuwa kwenye at least commercial court? mmmhhhhh galagabaho....

Hao wachumi ndio wanaoshirikiana na wezi kutoka mataifa ya nje kuiba rasilimali zetu na kuzipitisha kwa njia za panya, na hao hao wachumi ndio wanaowalinda. Kufikia kiwango cha kutorosha wanyamapori kupitia uwanja wa kimataifa wa ndege unaolindwa usiku na mchana, kwa nini isiwezekane kwa madini unayoweza kuyaweka mfukoni au kwenye handbag?

Wewe unaonekana ni mmoja wa wale wanaohusika kujinufaisha na wizi huo na hivyo umeshtukia deal kuanikwa hadharani.
 
Huyu naye amesomea uchumi wapi? Watanzania bwana mwanasheria anaongelea uchumi, mchumi anaongelea siasa, mwanasiasa anaongelea dini, padri/sheikh anaongelea siasa.... bora kila ki2 shaghala baghala mimi sijaona statement ya maana aliyoongea huyu jaji mstahafu.... NB: Alikuwa kwenye at least commercial court? mmmhhhhh galagabaho....

YOU ARE NOT SERIOUS!
KWELI? Watanzania ndio maana fursa nyingi zinawapita shauri ya "MYOPIA"...
Msomage fani zaidi ya moja basi! Vinginevyo mtaishia kulialia wenzenu walio multi-disciplinary" watakapokuja kuchukua fursa zenu zote.Kumbe hujui kwa mfano India na nchi nyingine huwezi kusomea sheria kama hujasoma fani nyingine.Wanasheria sasa hivi wanasoma fani nyingine - Engineering, Public Health, Management, Environmentals studies etc.and Vice Versa ikimaanisha walio na fani nyingine nao wanasomea Sheria.
 
YOU ARE NOT SERIOUS!
KWELI? Watanzania ndio maana fursa nyingi zinawapita shauri ya "MYOPIA"...
Msomage fani zaidi ya moja basi! Vinginevyo mtaishia kulialia wenzenu walio multi-disciplinary" watakapokuja kuchukua fursa zenu zote.Kumbe hujui kwa mfano India na nchi nyingine huwezi kusomea sheria kama hujasoma fani nyingine.Wanasheria sasa hivi wanasoma fani nyingine - Engineering, Public Health, Management, Environmentals studies etc.and Vice Versa ikimaanisha walio na fani nyingine nao wanasomea Sheria.

At least i'm ahead of the game, thus why I'm able to challenge him! read his statement carefully and you will see the falacies and shambles.....
 
Huyu naye amesomea uchumi wapi? Watanzania bwana mwanasheria anaongelea uchumi, mchumi anaongelea siasa, mwanasiasa anaongelea dini, padri/sheikh anaongelea siasa.... bora kila ki2 shaghala baghala mimi sijaona statement ya maana aliyoongea huyu jaji mstahafu.... NB: Alikuwa kwenye at least commercial court? mmmhhhhh galagabaho....

mkuu akili unazo kweli au? We unadhani ili kujua kama yai ni zima au bovu basi ni lazima nawe uwe unataga mayai? We mbumbumbu kweli.

Heri ungeuliza alikuwa wapi wakati yuko 'active' ktk utawala wa nchi hii maana wanaomaliza nchi kwa kushirikiana na hao wageni ni watu ambao anajuana nao.
 
hilo analosema Bomani sio jipya na lilishazungumziwa mpaka bungeni lkn serikali haitaki kufanya mabadiliko kutokana na sababu wanazozijua wenyewe.Labda kwenye hii katiba mpya tuingize vipengele vitakavyo ruhusu mikataba yote mikubwa ijadiliwe bungeni kabla ya kusainiwa ndo tutapona.
 
At least i'm ahead of the game, thus why I'm able to challenge him! read his statement carefully and you will see the falacies and shambles.....

Unajua nini unaongea au ni hulka tu ya kujenga ubishi? Mangapi unachangia hapa JF wakati huna ujuzi nayo? Wewe ni mchumi?
 
mkuu akili unazo kweli au? We unadhani ili kujua kama yai ni zima au bovu basi ni lazima nawe uwe unataga mayai? We mbumbumbu kweli.

Heri ungeuliza alikuwa wapi wakati yuko 'active' ktk utawala wa nchi hii maana wanaomaliza nchi kwa kushirikiana na hao wageni ni watu ambao anajuana nao.

Asante kwa mawazo mazuri, yananisaidia kujua nawasiliana na watu gani! keep it up!
 
hilo analosema Bomani sio jipya na lilishazungumziwa mpaka bungeni lkn serikali haitaki kufanya mabadiliko kutokana na sababu wanazozijua wenyewe.Labda kwenye hii katiba mpya tuingize vipengele vitakavyo ruhusu mikataba yote mikubwa ijadiliwe bungeni kabla ya kusainiwa ndo tutapona.
Ndio na mimi nawashangaa hawa viongozi wakitoka kwenye system kidogo, ndio wa kwanza kukosoa mfumo wa serikali, lakini wakiwa ndani ya system ni kimyaaaaaaaa!!!!!!!!!!

Sasa ngojeni sera atakazo kuja nazo mheshimiwa jaji Lewis Makame labda wampe kazi nyingine.
 
jaji-mark-bomani.jpg

Mwenyekiti wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za
Madini Serikalini (TEITI), Jaji Marck Bomani

MWENYEKITI wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za Madini Serikalini (TEITI), Jaji Marck Bomani, amesema wageni wanazidi kuimaliza nchi kupitia sekta ya madini, yakiwa ni matokeo ya sheria mbovu. Jaji Bomani imeishauri Serikali kubadilisha haraka sheria zilizopo kuhusu sekta hiyo ili kuwawezesha wananchi kujua kila kinachopatikana kutokana na raslimali hiyo.

Alisema uchimbaji wa madini utaendelea kuwanufaisha wageni kwa kuhamishia fedha na madini nchi za nje na kwamba hilo linatokana sheria zilizopo kuwapa mwanya.Jaji Bomani alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika warsha ya uelimishaji na uhamasishaji umma juu ya taarifa ya kwanza ya ulinganisho wa malipo na mapato kutoka kampuni za uchimbaji madini na gesi asili, katika mwaka wa fedha 2008/2009 iliyofanyika jijini Tanga

Alisema ni jambo la kushangaza kuona Tanzania pekee ikitoa mwanya kwa wawekezaaji kuchimba madini na kuyasafirisha nje kwa ajili ya kuyauza.Jaji Bomani alisema mabaya zaidi makampuni hayo yametakiwa kulipa kodi baada ya kuondoa gharama zote za uendeshaji au uzalishaji. "Hakuna mfanyabiashara anayeweza kusema ukweli juu ya faida ganayoipata kutokana na kuchimba madini, haiwezekani Tanzania tuendelee kuwa masikini wakati madini yetu yanayotoka yangeweza kusukuma mbele maendeleo yetu,"alisema Bomani.

Alisema katika taarifa ya awali imebainika kuwa uchambuzi uliofanyika kuna tofauti kubwa ya taakribani zaidi ya Sh 46 bilioni kati ya malipo yaliyodaiwa kulipwa na kampuni na fedha iliyopokelewa serikalini. Akiwasilisha mada ya mtizamo wa wadau na jamii juu ya ripoti ya kwanza ya TEITI na matarajio ya ripoti ya pili, mjumbe wa kamati hiyo, Askofu Stephen Munga alisema unahitajika uzalendo wa hali ya juu kwa viongozi waliopewa madaraka ya kuwaongoza wananchi.

Alisema haiwezekani rasilimali ya nchi kuendelea kuvunwa na kutoroshwa nje ya nchi kijanja na kuwanufaisha wageni huku Watanzania wakiendelea kuwa masikini na kwamba ni lazima hatua za makusudi za kuinusuru nchi zichukuliwe.

Serikali iliyopo madarakani ndiyo inaimaliza nchi, wageni ni mojawapo ya viungo vidogo vyakuimaliza nchi. Serikali legelege kila kitu legelege.
Eti mwenyekiti wa tume ya kufuatilia makampuni ya madini, yeye kachukua maaumuzi gani magumu kuhusiana na hii hali ya nchi kumalizwa? Viongozi kazi yao kulialia na kulalamika tu kama mbayuwayu.
 
Hivi aliye saini hii mikataba ya madini ni nani haswa? amesomea wapi sheria? maana haiwezekani mtu anasaini mkataba eti nichimbapo madi hakuna wa kuyamonitor,yanasafirishwa hadi SA wanaosha mchanga then wanakuja kutueleza kuwa eti tumevuna madini kg kadhaa kutoka Tz,hivi inaingia akirini kweli,mzungu akuonee wewe huruma kwa kukueleza ukweli ni kiasi gani cha madini kavuna inawezekana kweli?

Angaria Tanzanite makao makuu ya soko yapo USA na inafahamika kuwa muzaji mkuu ni SA jamani hii ni aibu sana
attachment%20(1).php

attachment%20(1).php

attachment%20(1).php
 
Anayo sema huyu mkuu ni ya kweli ! Uwajibikaji na utekelezaji wa mawazo sahihi ni ngumu sana kwa WATANZANIA kama hakutakuwa na mapinduzi ya kifikira na kiitikadi, tutaendelea kuwa watu wakulalamika na kujilaumu.
 
Ndyoko saafi sana, kuna siku huyu Mzee alisema kuwavua mafisadi magamba ni kuharibu amani ya taifa, halafu leo amegeuka tena na hao mediocre media hakuna wa kumlisha matapishi yake na some of us thinks he is a hero kwa kutuambia an empty song ambayo huhitaji instruments wala wapigaji kuiimba cause we can all sing it, badala ya kuwataja cause anawajua mafisadi wote wa huo wimbo anaouimba hasa rafiki yake mpenzi Mkapa na Net Group yao! Ha! Ha! nchi hii bwana wananchi wajinga ndio waliwetu! - Le Baharia
 
MWENYEKITI wa Tume ya Kufuatilia Kampuni za Madini Serikalini (TEITI), Jaji Marck Bomani, amesema wageni wanazidi kuimaliza nchi kupitia sekta ya madini, yakiwa ni matokeo ya sheria mbovu. Jaji Bomani imeishauri Serikali kubadilisha haraka sheria zilizopo kuhusu sekta hiyo ili kuwawezesha wananchi kujua kila kinachopatikana kutokana na raslimali hiyo.

Huyu naye aache kuwa scapegoat hao wageni. Kama wenyewe tunatunga misheria mibovu basi na tujilaumu wenyewe. Kulaumu wengine kwa mapungufu yako mwenyewe ni kukwepa uwajibikaji.
 
Hivi Tanzania uhuru uliopatikana 61 desemba 9 ilikuwa wa namna gani? Maana wakoloni hawajaacha kumiliki rasilimali zetu kama ilivyokuwa kabla na baada ya uhuru. Ardhi yenye rutuba ya inchi yetu, madini ya thamani ya inchi yetu, wanyama pori wa inchi yetu wao ndiyo wanaomiliki. Na kibaya zaidi wanamadharau sana wametuona sisi wajinga kiasi kwamba wanataka hata kuwaoa watoto wetu wa kiume walale nao kinyume na maumbile. Hivi hawa wazungu kwa nini viongozi wetu wasione hayo yote. Au wanataka kuonyesha kwamba wao ni ule ule uzao wa akina chifu Magungo wa Msevero waliofanya boargas treatment na akina Karl Peters. Tanzania haiko huru hata kidogo hapa ni kwamba tunapigwa changa la macho tu lakini hamna kitu in fact. Tumwombe Mungu tumpate kiongozi jasiri kama Robart Mgabe wa Zambia aje aikomboe nchi yetu kutoka kwa wakolon.
 
Back
Top Bottom