Jairo hana kosa

Mhoja

JF-Expert Member
Aug 13, 2010
207
24
Kwa wanasheria wenzangu tuhuma za jairo za kuchangisha fedha hazina base ya sheria, bali ni base ya kisiasa. Tujadili!
 
kisiasa kivipi ebu fafanua vzuri mana luhanjo kamsafisha ajatakata ebu na ww kama mwanasheria msafishe hapa jamvini labda atasafishika
 
teh teh napita tu,,ukitaka kuishi TZ kwa amani uachane na siasa uchwara....dirty politicssss,,,,,,
 
Who cares kama ni msafi kisheria!..Sheria yenyewe ya Bongo ilimtia hatiani nani wewee?

Tunachoumia nacho ni ukosefu wa sense of responsibility miongoni mwa viongozi wa miongo hii!
Unaponyooshewa vidole na jamii ya WaTanzania wengi hivi, bila kustuka wala dhamiri kukugusa kuwa umekosea, basi hufai hata kuchunga mbuzi, maana hutowaonea huruma!
Jairo has to go!
 
Kwa wanasheria wenzangu tuhuma za jairo za kuchangisha fedha hazina base ya sheria, bali ni base ya kisiasa. Tujadili!

Ningependa kukuuliza Je mtu anapokiuka taratibu zilizowekwa za kifedha ni kosa au sio kosa? Aren't finacial regulations backed by statutes?
 
Mkuu kuna sheria nyingi...

Sheria za kutokutoa au kupoke rushwa....
Sheria za kikazi na maadili
Sheria za kuwajibika na kutumikia Umma

Kwahiyo mkuu in the end kama itagundulika kwamba huo utaratibu wa wizara wa kuchangisha pesa ili kufanikisha Bajeti sio utaratibu wa kisheria, basi yeye Jairo kama muhusika wa kuchangisha atakuwa na hatia..., (ila sio yeye tu bali na waliochanga na wote waliohusika wizarani na kupitisha huu utaratibu bila kuukemea)

Lakini kama kuchangisha pesa ili bajeti ipite ni suala la kawaida kisheria (na sio ufujaji pesa za umma) basi hakuna mwenye hatia
 
Who cares kama ni msafi kisheria!..Sheria yenyewe ya Bongo ilimtia hatiani nani wewee?<br />
<br />
Tunachoumia nacho ni ukosefu wa sense of responsibility miongoni mwa viongozi wa miongo hii!<br />
Unaponyooshewa vidole na jamii ya WaTanzania wengi hivi, bila kustuka wala dhamiri kukugusa kuwa umekosea, basi hufai hata kuchunga mbuzi, maana hutowaonea huruma!<br />
Jairo has to go!
<br />
<br />
kwa nini asiwe ngereja na hii ukiiangalia inaonekana ndio kinacho fanywa na wizara zote ila hapo kwa jairo kuna kitu cha kumnufaisha mtu..
 
Tatizo accusation hazijawa framed in correspondence to law, wanasema rushwa hushahidi wakuna wa mbunge hata mmoja aliyepewa rushwa! kufahamu cause of action ni moja ya kufanikiwa kama hufahamu cause of action utaishia kubwabwaja tu.
 
Kwa wanasheria wenzangu tuhuma za jairo za kuchangisha fedha hazina base ya sheria, bali ni base ya kisiasa. Tujadili!

Tuhuma za Jairo zina base ya kisheria, kwa kuanzia lazima tufahamu idhini ya kukusanya fedha kwa accounting officer(permanent secretary) kama jairo anaongozwa na finance act ambayo hupitishwa na bunge na hatimaye kupewa baraka na rais na humo ndimo vyanzo vyote na viwango vya kukusanya vimepata (parliamentary approval) swali ni hivi hizo taasisi zilizotoa mchango huo zilitoa fedha wapi? yaani ni ndani ya kile kilichoidhinishwa na bunge kwenye appropriation act kwa kuzingatia mgawanyo wa matumizi yaliyoidhinishwa na bunge? na kama zintokana na vyanzo vyao wenyewe (appropriation in aid) iwe ziada ya makusanyo ilipata idhini kutoka wapi? lakini pia ukisoma public fiance act 2001 Revised 2004 inatamkwa wazi kuwa kutumia fedha yoyote ya serikali pasipo approval ya perliament (over expenditure) na kama kuna uhitaji wa zarura bado utaratibu upo wazi taratibu zimeainishwa. hapa siyo siri pana tatizo si tu la kimfumo lakini nidhamu katika usimamizi wa fedha ya umma, ingawa mimi naamini wapo waliochangishwa fedha hiyo na hizo wakala za wizara ya nishati na madini na most probably wachimbaji wetu wa madini, walikuwa wamingizwa mkenge
 
maana hiyo MBUGI tunaama kutoka kwenye rushwa hadi kwenye hadi financila mismanagement sasa kama alishtakiwa kwa rushwa we ungemconvict au ungemuachia?
 
Kwa mtazamo wangu hatua ya rais kumrudisha dj(david jairo)likizo ili kuipa kamati ya bunge nafasi ya kumchunguza jairo inaweza kuleta mtafaruku wa kisheria hapo baadae kwa mantiki kwamba bwn jairo ni mtumishi wa serikali na sio mtumishi wa bunge kwa msingi huo hata kama taarifa ya kamati ya bunge itamtia hatiani bado itabidi waishauri serikali hatua za kumchukulia jairo na sio kumwajibisha, pili kwa kua kwa upande wa serikali(kupitia bwn luhanjo) umeshamsafisha jairo itakua vigumu serikali hiyo hiyo kumuadhibu bwn jairo kwa maelekezo ya bunge, aidha mimi sioni kwa hali ilivyo sasa kama kamati ya bunge katika mazingira haya inaweza kuwa 'neutral' ili uchunguzi uwe huru wakati huo huo kama taasisi za kitaaluma katika uchunguzi yaani CAG na PCCB hazikuona hatia juu ya bwn jairo nashindwa kuona ni namna gani timu wa wanasiasa (kamati ya bunge) inawezaje kufanya uchunguzi huo wa kitaalam na kutoa majibu chanya. je haikua busara kwa wabunge kuelekeza suala hili mahakamani ambapo ndiko haki inaposimamiwa aidha kwa msingi wa mihimili ya dola mahakama iko netral na ingesimama katikati ya serikali na bunge pengine watanzania tungeona mwanga mpya , hofu yangu uchunguzi huo unaweza kupika majibu ili mhimili mmoja uonekane bora zaidi ya mwingine.
 
Ila kwa hili la jairo serikali imetia aibu, no matter kwamba Jairo ana hatia amb la, alipewa likizo ili uchunguzi. je Luhanjo hakuwasiliana kwanza na mkuu wake? aibu sana serikalini no communication.
 
Back
Top Bottom