Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi (K-Lynn) aomba marejeo ya kesi yake ya mirathi dhidi ya Watoto wa Mengi

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,803
4,467
Salaam Wakuu,

Ile kesi iliyofunguliwa na Mjane wa Marehemu Ragnard Mengi, Jackline Mengi dhidi ya Mtoto wa Mengi na wenzake watano inataraji kuanza kusikilizwa katika mahakama ya rufaa mwishoni mwa mwezi huu.

Kesi hiyo ambayo ni marejeo namba 332/1/2021 iko mbele ya jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Jacob Mwambegele.

Katika kesi ya marejeo Jackline Mengi anapinga maamuzi ya Mahakama Kuu yaliyobatilisha wosia wa Regnard Mengi. Pia, Jackline anapinga uteuzi wa Benjamini Mengi na mwenzie kama wasimamizi wa mirathi ya marehemu Regnard Mengi.

PIA, SOMA: Wosia wa Mirathi ya Dkt. Reginald Mengi: Jacqueline Ntuyabaliwe adondokea pua



UPDATES
- Jacqueline Mengi apeta mahakama ya Rufani, mahakama yakubali kumsikiliza kinyume na mapingamizi ya watoto wakubwa
 
Huyu Mjane atendewe Haki.

Nashangaa kwa nini taasisi za kutetea haki za wanawake haswa wajane wamekaa kimya?!

Huyu mjane ananyanyaswa na ndugu wa marehemu mchana kweupe!!

Anafanyiwa figisu na faulo kibao ili tu asipate haki zake.

lkn naamini vyovyote vile itakavyo kuwa lazima Haki zake zitapatikana
 
Huyu Mjane atendewe Haki.

nashangaa kwa nini taasisi za kutetea haki za wanawake haswa wajane wamekaa kimya?!
huyu mjane ananyanyaswa na ndugu wa marehemu mchana kweupe!!

anafanyiwa figisu na faulo kibao ili tu asipate haki zake.
lkn naamini vyovyote vile itakavyo kuwa lazima Haki zake zitapatikana
 
Yaani uamuzi wa mahakama kuu yeye anaupinga? Naomba huko juu anakokwenda wamnyang'anye hata hicho alichonacho. Yaani watoto imekuwa nongwa?

Kwani nani mwenye uhakika kwamba watoto ni wa mengi kweli? Binti mwenyewe bongo fleva! Ndugu wa mengi piganeni3 hadi kieleweke mkishindwa wekeni watani zenu wanaouza ng'ombe waendeshe kesi ya kuku!
 
Haki gani tena zaidi yahiyo ya mahakama..
au waandamane?
Huyu mjane anahaki zaidi kulingana na wosia aliopewa na Marehemu Mume wake.
Wosia wa Marwhemu Mume wake ulibatilishwa kimakosa, lazima wosia wa marehemu ufuatwe kama ulivyo bila kubatilisha chochote.

Wosia wa Marehemu ulikuwa halali na aliutoa akiwa na akili timamu na alimaanisha alicho kiandika.
Mjane na watoto wake wanayo haki ya kurithi kulingana na wosia wa Marehemu.
 
Huyu Mjane atendewe Haki.
nashangaa kwa nini taasisi za kutetea haki za wanawake haswa wajane wamekaa kimya?!
huyu mjane ananyanyaswa na ndugu wa marehemu mchana kweupe!!
anafanyiwa figisu na faulo kibao ili tu asipate haki zake.
lkn naamini vyovyote vile itakavyo kuwa lazima Haki zake zitapatikana
Ndugu gani wa marehemu anamnyanyasa mjane wakati hapo ni taratibu za kisheria zimefuatwa.
 
huyu mjane anahaki zaidi kulingana na wosia aliopewa na Marehemu Mume wake.
Wosia wa Marwhemu Mume wake ulibatilishwa kimakosa, lazima wosia wa marehemu ufuatwe kama ulivyo bila kubatilisha chochote.
Wosia wa Marehemu ulikuwa halali na aliutoa akiwa na akili timamu na alimaanisha alicho kiandika.
Mjane na watoto wake wanayo haki ya kurithi kulingana na wosia wa Marehemu.
Wosia una vigezo, mahakama imetengua wosia kwa sababu imeona haujakidhi vigezo.
 
Huyu Mjane atendewe Haki.

Nashangaa kwa nini taasisi za kutetea haki za wanawake haswa wajane wamekaa kimya?!

Huyu mjane ananyanyaswa na ndugu wa marehemu mchana kweupe!!

Anafanyiwa figisu na faulo kibao ili tu asipate haki zake.

lkn naamini vyovyote vile itakavyo kuwa lazima Haki zake zitapatikana
Wamekaa kimya sababu wanajua hastahili hivyo anavyovidai Wala hajavitolea jasho
 
Yaani uamuzi wa mahakama kuu yeye anaupinga? Naomba huko juu anakokwenda wamnyang'anye hata hicho alichonacho. Yaani watoto imekuwa nongwa?

Kwani nani mwenye uhakika kwamba watoto ni wa mengi kweli? Binti mwenyewe bongo fleva! Ndugu wa mengi piganeni3 hadi kieleweke mkishindwa wekeni watani zenu wanaouza ng'ombe waendeshe kesi ya kuku!
Naona una utan na watu....hahahahahaha
 
Back
Top Bottom