Asalaam Mh. Mwenyekiti wangu
Baada ya salaam naomba kukupa hongera kwa hekaheka za hapa na pale huku pia nikikutia moyo usonge mbele kuendelea kupanga safu na vikosi vyako vizuri kwa sababu mambo yameiva mkuu. Kwetu huku kwa watu wa Pwani kuna msemo usemao
*"kurukaruka kwa maharage ndiyo kuiva kwake"*
Mhe. Mwenyekiti wangu, Mungu atupe nini zaidi ya haya yanayoendelea sasa? Siasa imekuwa nyepesi kuliko miaka yote 25 mliyoanzisha vuguvugu la mabadiliko nchini. Siku hizi wasomi, wafanya biashara, viongozi wa dini, wasanii na hata mabishoo nao wanapiga siasa vizuri kuliko hata baadhi ya waanzilishi na waasisi wa siasa za mabadiliko.
Dalili ni njema sana na matunda ya kazi za watangulizi wote wa mageuzi, kuanzia waliokimbia upande wetu mpaka tulionao leo. Mimi mmoja wa wapiganaji (askari) wako wa miguu, nakuhakikishia mambo mazuri sana mtaani.
Je Mh. Mwenyekiti umeliona teke la farasi anayekufa? Kwa kule majuu wanaita *"the last kick of the dying horse"*
Kwa sasa CCM na serikali yake hawana tena jipya na wameacha kufanya siasa tena. Ndiyo maana husikii mashambulizi kwetu kama zamani ooh mara siasa za ukanda, mara udini, mara kununua wapinzani zaidi ya yule BWANA YULE....siyo wajinga walishajua haisaidii tena na muda umekwenda sana na wameanza kuachwa nao.
Teke la farasi anayekufa baya sana Mh. Mwenyekiti. Huwa lina nguvu sana. Huweza kukusababishia kifo. Huwa ndiyo karata yake ya mwisho ya kupambania uhai wake. Bahati nzuri ni kwamba huwa pia ni dalili ya kwamba amezidiwa na hana mbinu nyingine tena kabla ya kusalimu amri ya kifo. *Ndiyo farasi anakufa hivyo*
CCM ndiyo kinahitimisha utawala wake wa miaka arobaini na ushee tangu kianzishwe na kinajua kinaelekea kufa ama kufutika kabisa.
Jambo pekee wanalodhania litawaokoa na kifo cha chama chao na serikali yao ni kuua, kuteka na kupoteza wapinzani na wakosoaji wa serikali yao. Ili kupunguza kupingwa kila kona ama kutia watu uoga.
Kumbe jambo ambalo farasi anayekufa hakuwa anajua ni kwamba, wakosoaji kwenye nchi si nyinyi peke peke yenu kama zamani bali moto wa fikra za mabadiliko ulishawaka nchi nzima. Sisi tunaoishi na watu huku mitaani tunaona.
Mh. Mwenyekiti kila tawala ya kidhalimu inapokaribia kutoweka inatumia mbinu hizo. Majirani zetu Afrika Kusini chini ya makaburu walikutana na hali hii walipokuwa wanawaondoa makaburu madarakani. Waliuwawa, waliteswa na wengine walipotezwa hata maiti zao hazikuonekana kabisa.
Lakini hawakurudi nyuma bali walianzisha makambi ya vijana na kauli mbiu ya "UMKHONTO WE SIZWE" kulinda wanachama wa ANC viongozi wake na wananchi wanyonge dhidi ya makaburu. Ikawa 'teka tuwateke, poteza tuwapoteze na vunja tukuvunje'.
Kila ngazi ya chama chao ANC palikuwa na BLACK BOOK ya kusajili majina na anuani za watesi wao kwenye likitabu la kumbukumbu......wapo wananchi wetu huku chini wanaanza kushauri kuwa hilo hata sisi tunaweza kulifanya.
Juzi mmoja akaniuliza kwanini Mh. Mwenyekiti usiitishe vikao vya chama na tuazimie na tutangazie wanachama wetu wote na wapenzi wa mabadiliko hali ya hatari, ili tujihami wote? Tuhesabu kondoo wako zizini. Wasipotee zaidi ya hao waliopotea. Tusilalamike kuumizwa wakati na sisi tunacho cha kufanya. Hili pekee ndilo litakalofanya tuwe salama na tuheshimiane ikibidi kukaa chini meza moja kwa mazungumzo ya kuamua mstakabali mwema wa pamoja wa nchi yetu, Mama Tanzania.
Tangaza hari ya hatari kwa wanachama wako na wafuasi wote, kisha mikoa na wilaya za kichama zikae chini kutoa vijana wa kike na kiume kila upande. Tupewe mafunzo ya tahadhari na kujihami dhidi ya vikundi vya kifedhuli na nina imani vijana tutakupa ushirikiano mkubwa sana,
sababu wakosoaji na wapinzani wa serikali hii hatuna mpango wa ku retreat au kuacha kabisa kuikosoa na kuipinga kwa namna ilivyopoteza malengo na muelekeo ambao Watanzania walitarajia.
Haitakuwa mara ya kwanza kwa chama kufanya hivyo na haitakuwa mara ya mwisho kwa wewe kulaumiwa kwa kuongoza vikao vya chama kufanya maamuzi ya kulinda hadhi na utu wa wanachama wetu na jamii nzima ya Watanzania.
Tunashauri ufanye hima... hima Mh. Mwenyekiti wetu, vijana wako tumalizie kazi ambayo wewe na Wazee wetu wengine mmeisimamia kwa miaka yote 25 kwa ajili ya MABADILIKO YA KWELI NA UHURU WA KWELI ndani ya nchi yetu Tanzania.
Na BONIFACE JACOB
MJUMBE KAMATI KUU
SENIOR COUNCILOR UBUNGO
Baada ya salaam naomba kukupa hongera kwa hekaheka za hapa na pale huku pia nikikutia moyo usonge mbele kuendelea kupanga safu na vikosi vyako vizuri kwa sababu mambo yameiva mkuu. Kwetu huku kwa watu wa Pwani kuna msemo usemao
*"kurukaruka kwa maharage ndiyo kuiva kwake"*
Mhe. Mwenyekiti wangu, Mungu atupe nini zaidi ya haya yanayoendelea sasa? Siasa imekuwa nyepesi kuliko miaka yote 25 mliyoanzisha vuguvugu la mabadiliko nchini. Siku hizi wasomi, wafanya biashara, viongozi wa dini, wasanii na hata mabishoo nao wanapiga siasa vizuri kuliko hata baadhi ya waanzilishi na waasisi wa siasa za mabadiliko.
Dalili ni njema sana na matunda ya kazi za watangulizi wote wa mageuzi, kuanzia waliokimbia upande wetu mpaka tulionao leo. Mimi mmoja wa wapiganaji (askari) wako wa miguu, nakuhakikishia mambo mazuri sana mtaani.
Je Mh. Mwenyekiti umeliona teke la farasi anayekufa? Kwa kule majuu wanaita *"the last kick of the dying horse"*
Kwa sasa CCM na serikali yake hawana tena jipya na wameacha kufanya siasa tena. Ndiyo maana husikii mashambulizi kwetu kama zamani ooh mara siasa za ukanda, mara udini, mara kununua wapinzani zaidi ya yule BWANA YULE....siyo wajinga walishajua haisaidii tena na muda umekwenda sana na wameanza kuachwa nao.
Teke la farasi anayekufa baya sana Mh. Mwenyekiti. Huwa lina nguvu sana. Huweza kukusababishia kifo. Huwa ndiyo karata yake ya mwisho ya kupambania uhai wake. Bahati nzuri ni kwamba huwa pia ni dalili ya kwamba amezidiwa na hana mbinu nyingine tena kabla ya kusalimu amri ya kifo. *Ndiyo farasi anakufa hivyo*
CCM ndiyo kinahitimisha utawala wake wa miaka arobaini na ushee tangu kianzishwe na kinajua kinaelekea kufa ama kufutika kabisa.
Jambo pekee wanalodhania litawaokoa na kifo cha chama chao na serikali yao ni kuua, kuteka na kupoteza wapinzani na wakosoaji wa serikali yao. Ili kupunguza kupingwa kila kona ama kutia watu uoga.
Kumbe jambo ambalo farasi anayekufa hakuwa anajua ni kwamba, wakosoaji kwenye nchi si nyinyi peke peke yenu kama zamani bali moto wa fikra za mabadiliko ulishawaka nchi nzima. Sisi tunaoishi na watu huku mitaani tunaona.
Mh. Mwenyekiti kila tawala ya kidhalimu inapokaribia kutoweka inatumia mbinu hizo. Majirani zetu Afrika Kusini chini ya makaburu walikutana na hali hii walipokuwa wanawaondoa makaburu madarakani. Waliuwawa, waliteswa na wengine walipotezwa hata maiti zao hazikuonekana kabisa.
Lakini hawakurudi nyuma bali walianzisha makambi ya vijana na kauli mbiu ya "UMKHONTO WE SIZWE" kulinda wanachama wa ANC viongozi wake na wananchi wanyonge dhidi ya makaburu. Ikawa 'teka tuwateke, poteza tuwapoteze na vunja tukuvunje'.
Kila ngazi ya chama chao ANC palikuwa na BLACK BOOK ya kusajili majina na anuani za watesi wao kwenye likitabu la kumbukumbu......wapo wananchi wetu huku chini wanaanza kushauri kuwa hilo hata sisi tunaweza kulifanya.
Juzi mmoja akaniuliza kwanini Mh. Mwenyekiti usiitishe vikao vya chama na tuazimie na tutangazie wanachama wetu wote na wapenzi wa mabadiliko hali ya hatari, ili tujihami wote? Tuhesabu kondoo wako zizini. Wasipotee zaidi ya hao waliopotea. Tusilalamike kuumizwa wakati na sisi tunacho cha kufanya. Hili pekee ndilo litakalofanya tuwe salama na tuheshimiane ikibidi kukaa chini meza moja kwa mazungumzo ya kuamua mstakabali mwema wa pamoja wa nchi yetu, Mama Tanzania.
Tangaza hari ya hatari kwa wanachama wako na wafuasi wote, kisha mikoa na wilaya za kichama zikae chini kutoa vijana wa kike na kiume kila upande. Tupewe mafunzo ya tahadhari na kujihami dhidi ya vikundi vya kifedhuli na nina imani vijana tutakupa ushirikiano mkubwa sana,
sababu wakosoaji na wapinzani wa serikali hii hatuna mpango wa ku retreat au kuacha kabisa kuikosoa na kuipinga kwa namna ilivyopoteza malengo na muelekeo ambao Watanzania walitarajia.
Haitakuwa mara ya kwanza kwa chama kufanya hivyo na haitakuwa mara ya mwisho kwa wewe kulaumiwa kwa kuongoza vikao vya chama kufanya maamuzi ya kulinda hadhi na utu wa wanachama wetu na jamii nzima ya Watanzania.
Tunashauri ufanye hima... hima Mh. Mwenyekiti wetu, vijana wako tumalizie kazi ambayo wewe na Wazee wetu wengine mmeisimamia kwa miaka yote 25 kwa ajili ya MABADILIKO YA KWELI NA UHURU WA KWELI ndani ya nchi yetu Tanzania.
Na BONIFACE JACOB
MJUMBE KAMATI KUU
SENIOR COUNCILOR UBUNGO