TANZIA Jackson Makwetta (Mbunge na Waziri wa zamani) afariki dunia

ripoti yake ya maboresho ya elimu mpaka sasa haijafanyiwa kazi. ndo maana kafa.R.I.P
 
R i p Mzee wangu kiroho safi siye tulikupenda na Mungu kakupenda zaidi ni majonzi ya ukweli kwa wana Njombe na Tanzania kwa ujumla
 
Tujifunze kuthamini watu wakiwa Hai,sifa zote hizi na kumbukumbu ya mazuri yake mngeyasema enzi za uhai wake ili hata watoto waliozaliwa enzi za Mwinyi waijue historia ya viongozi waliopita na kutaka kujua wanafanya nini kwa sasa.

mnapoyasema haya sasa hayana faida kwani tayari mavumbini amerudi.

Ilitupasa kujua yuko wapi,anafanya nini na anaendeleaje kwa kipindi chote cha nyuma.

ndugu zangu wataandaa mazishi kwa gharama,wakati hata matibabu yalikuwa tabu kumhudumia.

RIP.MAKWETA (I will miss you for ever,a good friend,a client.)
 
..RIP Jackson Makweta.

..alikuwa waziri wa elimu wakati taifa likipita ktk matatizo makubwa sana ya kiuchumi.

..kazi aliyoifanya, na rekodi yake kama waziri wa elimu, itakumbukwa na wengi.

..Jackson Makweta ndiye aliyeanzisha mtihani wa form 2.
 
Tujifunze kuthamini watu wakiwa Hai,sifa zote hizi na kumbukumbu ya mazuri yake mngeyasema enzi za uhai wake ili hata watoto waliozaliwa enzi za Mwinyi waijue historia ya viongozi waliopita na kutaka kujua wanafanya nini kwa sasa.
)

Hayo tuliyoyanena hapo juu yamo humu JF katika profile za viongozi mbali mbali, tuliyaandika hata kabla hajafa. Wasifu wa kila kiongozi, mazuri na mabaya yake yamo humu JF. Tafuta information zaidi, utazipata.
 
R.I.P Jackson Makweta, nitakukumbuka hasa katika utumishi wako ukiwa waziri wa elimu enzi hizo
 
Alikuwa mtu mkweli kisiasa kitu ambacho kilimsababishia kuukosa Uwaziri pale Mkapa alipoingia madarakani na kumteua Sumaye Waziri Mkuu 1995. Makwetta kama senior minister na immediate formern boss wa Sumaye akaombwa kutoa speech wakati wa kum-endorse Sumaye na ndio likaharibikia hapo. Alikaririrwa akidai kuwa aliwahi kumkaripia Sumaye wakati akaiwa deputy wake. Hakurudi tena kwenye uwaziri
 
Mzee huyu alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wa CCM waliotumikia taifa lao kwa uadilifu na kwa uzalendo wa hali ya juu, akiwa waziri wa serikali kwa miaka 25 mfululizo (1975 - 2000), lakini hakuna mahali alitumia vibaya madaraka yake kwani inasemekana kwamba hata nyumba ya kuishi nje kidogo ya jiji la Dar-es-salaam alijengewa na wanae kabla ya kustaafu na hata hivyo haikukamilika ipasavyo; na katika kipindi karibia chote cha ustaafu wake alikuwa anaishi kwao kijijini;

Lakini kwa vile serikali yetu ya CCM haijali watu kama hawa, msiba wake utaendeshwa kinafiki tu; Misiba yenye kupewa uzito ni ile ya viongozi wasiokuwa wazalendo ambao utashi wao unapimwa kwa utajiri wao; Lakini ipo siku yote haya yatabadilika;

Poleni wafiwa; Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi Mzee wetu Makweta, Amen;

Angekuwa mwanamziki au mwigizaji CCM wangeuchakalikia huo msiba na serikali ingetoa 10 million............. Hakuna deal la kisiasa kwa Makweta........... Rais atapeleka mwakilishi.

RIP Jakson.
 
Kijijini kwetu tunamkumbuka sana kwa jinsi alivyopigana kiume mpaka tukapata barabara na RTC enzi hizo akiwa mbunge wa njombe ( Ludew,Makete,Wanging`ombe zilikuwa bado kumegwa). Kweli watu wazuri wanakufa yanabaki manung`ayembe yanayotuhangaisha.

Kwa njombe, alipigania elimu sana kupitia NDDT, shule zikafunguliwa kwa wingi. Mungu amekupenda zaidi.

RIP MAKWETA.
Alifanya kazi kubwa sana katika kujenga mji wa Makambako kwani wanaokumbuka Makambako ya miaka ya 80 na 70 ukilinganisha na ya sasa huwezi kuamini.
 
Mzee huyu alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wa CCM waliotumikia taifa lao kwa uadilifu na kwa uzalendo wa hali ya juu, akiwa waziri wa serikali kwa miaka 25 mfululizo (1975 - 2000), lakini hakuna mahali alitumia vibaya madaraka yake kwani inasemekana kwamba hata nyumba ya kuishi nje kidogo ya jiji la Dar-es-salaam alijengewa na wanae kabla ya kustaafu na hata hivyo haikukamilika ipasavyo; na katika kipindi karibia chote cha ustaafu wake alikuwa anaishi kwao kijijini;

Lakini kwa vile serikali yetu ya CCM haijali watu kama hawa, msiba wake utaendeshwa kinafiki tu; Misiba yenye kupewa uzito ni ile ya viongozi wasiokuwa wazalendo ambao utashi wao unapimwa kwa utajiri wao; Lakini ipo siku yote haya yatabadilika;

Poleni wafiwa; Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi Mzee wetu Makweta, Amen;


GT tuwe wa kweli na taarifa tunazozitoa.

Mimi namfahamu sana Makweta nilifanya nae kazi kwa karibu sana nikiwa Wizara ya fedha (Muungano) na hata nilipoamishiwa Mkoa wa Mwanza.

Binafsi sio tu nimefika kwake Dar lakin pia mpaka kule kijijini kwake nilifika wati huo.

Je unajua nini wananchi wake wa jimbo lake waliamua kumuondoa kwa kumnyima Kura katika kura za maoni na kushindwa na kijana Mdogo Sanga?

Usimpe swifa mtu asonazo, mzungumze vile alivyo.

Usione mtu kashindwa maisha basi ukasema alikuwa mwadilifu. Kuna wengi wa kariba yake akina Mwingira anayeishi kule Kigamboni.

Mola aiweke pahala panapo stahiki Roho ya jackson Makweta.
 
GT tuwe wa kweli na taarifa tunazozitoa.

Je unajua nini wananchi wake wa jimbo lake waliamua kumuondoa kwa kumnyima Kura katika kura za maoni na kushindwa na kijana Mdogo Sanga?

Mola aiweke pahala panapo stahiki Roho ya jackson Makweta.

Je unajua kuwa DEO SANGA (JAH PEOPLE) alitumia nguvu ya pesa kuwaangusha MAKWETTA ubunge na MANGULA uenyekiti wa CCM mkoa? Au ndio kuishi mbali unasahau kwenu? Na huyu Sanga sio bwana mdogo kama unavyotaka tuamini.

DSC06904.JPG
 
Je unajua kuwa DEO SANGA (JAH PEOPLE) alitumia nguvu ya pesa kuwaangusha MAKWETTA ubunge na MANGULA uenyekiti wa CCM mkoa? Au ndio kuishi mbali unasahau kwenu? Na huyu Sanga sio bwana mdogo kama unavyotaka tuamini.

DSC06904.JPG

Hujui ulinenalo .

Huwajui hata kidogo watu wa Njombe (wabena) ndio maana unasema wananunulika Kirahisi hivyo.

Siwezi ongea mengi lakin Nikuulize je unamjua yule ndugu yake aliyewahi kuwa Civil Engineer wa Tz railways. Anzia hapo sasa kisha endelea utajua kwanini alinyimwa kura.

Lakin Nimesema Bwana Mdogo Sanga kwa sababu Sanga ni mdogo sana kwa Makwetta. Samahani kama nitakuwa nimekukwaza kwa kumwita Sanga Bwana mdogo kwani nilikusudia hivyo.

RIP Makweta
 
RIP Mzee Makweta! Poleni wafiwa. Niliwahi kupata nafasi ya kufahamiana na mwanae mmoja anaitwa Atwite, hatujaonana muda mrefu sana. Poleni sana Atwite na nduguzo wote.
 
Back
Top Bottom