J. Mnyika: How and Why did you loose Ubungo 2005?

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Yohana wa Mnyika,

Ndugu yangu naomba leo nikuulize swali gumu na very personal.

Kulitokea nini Ubungo 2005 ukashindwa kuchukua Ubunge wa jimbo?

Jimbo la Ubungo, liko Dar Es Salaam, mji mkubwa Tanzania. Nakadiria kuwa karibu 50% ya wakazi wa Ubungo ni "middle class", wasomi na wenye kupenda maendeleo na si rahisi kubabaishwa na siasa za CCM.

Sasa najiuliza leo, nikiwa najikumbusha ninavyokufahamu na hata kwa kusoma Waraka mbali mbali ulizoandika, ni kitu gani kilisababisha Ubungo kuangukia mikononi mwa CCM?

Je ilikuwa ni wizi wa kura?
Je ilikuwa ni hongo, rushwa na takrima?
Je ilikuwa ni uwezo mdogo wa kifedha kwako na Chadema kupambana na CCM?
Je ilikuwa ni kukosekana kwa mikakati na mipango mizuri kujitangaza na hata kuendesha kampeni na kuweza kukonga na kuteka nyoyo za Wana-Ubungo?
Je ilikuwa ni Ujana na ukosefu wa ujuzi wa michuano ya kisisasa?
Je ulishindwa kujiuza kisera na kiitikadi kwa Wana-Ubungo?
Je ni kwa kuwa ulikuwa Chadema na si CCM, CUF, TLP, NCCR au chama kingine cha siasa?
Je mlikanyagana viatu na wagombea wa vyama vingine na kuishia kumpa Keenja ushindi wa bure?

Kumbukumbu zangu zaniambia kulifunguliwa kesi ya Uchaguzi.

Lakini najiuliza tena, kijana mahiri kama wewe ulishindwaje kulichukua jimbo la Ubungo kwa nguvu kubwa na kuishia kwenda mahakamani?

Nikiangalia Ubungo na wakazi wake, kama Chadema na wewe kama mgombea, mngekuwa na mikakati mizuri, suala la uhamasishaji na kukonga nyoyo lingekuwa ni rahisi.

Ubungo imezungukwa na taasisi za Elimu ya juu nyingi. Anzia UDSM, Ardhi, Maji, DIT, kuna mashirika na taasisi zenye maendeleo makubwa na watu wenye upeo mkubwa wa mawazo, je ilishindikana vipi kujiuza kwa hawa watu haswa waalimu na wanafunzi ili waeneze Injili ya Mnyika na Chadema?

Najua wanafunzi ni wapita njia, lakini je walitumika japo kusaidia kufanya kampeni na kulipeperusha jina la Mnyika na Chadema? au nao walikuwa wagumu kuuziwa na kununua bidhaa ya Mnyika na Itikadi na Sera Chadema?

Je 2010 inavyokuja unatarajia kugombea tena? kama utagombea, ni mambo gani ambayo unafikiri ni lazima uyafanye ili ujipatie Ushindi wa Tsunami?

Najua mikakati mingine ni siri yako ya moyoni na chama chako na ni mapema sana kumwaga mchele kwenye kuku. Lakini kama Mwana Jamii mwenzako na Mwanaharakati, inabidi niulize na nikuulize kati yetu ili kama kulikuwa na makosa, tuyarekebishe, kama ni kujenga mikakati, basi tukusaidie ili Bunge letu lipate Mwana JF wa pili (au zaidi ikitegemea wale wanaojificha!) baada ya Zitto.

Kwa wewe na Zitto, tambueni kuwa pamoja na JF kuwa imetapakaa dunia nzima, lakini ni Jimbo moja mahiri ambalo mnalihitaji kwa nguvu sana!

La mwisho, katika jimbo la Ubungo, ni kata ngapi na kuna madiwani wangapi ambao ni wa Chadema au Upinzani?

Nasubiri majibu yako na hata ya wengine ambao wanafahamu kwa undani kilichotokea 2005.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani tumsubiri mwenyewe ila mimi nilishamshauri huko nyuma hana uwezo wa kumshinda Keenje Ubungo atafute jimbo la mikoani kama mwenzake Zitto.
In Africa, democracy is not voting, but counting the votes - January Makamba, Tanzanian (Ikulu)
 
tatizo la wapinzani wengi hawana pesa za kushindana na CCM,kama huna pesa basi atleast uwe na jina...nina uhakika wapinzani wangeweza kuchukua majimbo yote ya Dar kama wangesimamisha watu wenye majina kama Mrema,mapesa,Mbowe,zitto etc lakini tatizo lao wote hao wanataka uraisi ambao ni ndoto za alinacha kwa siasa za bongo...ila ndugu mnyika sio vibaya ikifika uchaguzi njoo utuombe dollar mimi nitakukatia check bila tatizo labda itasaidia.
 
Well ili kushinda uchaguzi wa kisiasa kwa hii demokrasia ya ya kileo unahitaji vitu vitatu

1. Message

2. Money

3. Election machine

Sasa kwa mkuu wangu mnyika nna uhakika message alikuwa nayo maana niliwahi kumsikia live kule mabibo akihutubia and watu walikuwa very impressed. Tatizo kubwa naloliona ni kwenye hayo maeneo mawili yaliyobaki Money and election machine Mkuu inabidi 2010 kama mpango huo bado upo akomae na hayo maeneo, lakini pia message nayo ni lazima ireflect wakati wa sasa
 
mimi sijui ukweli kwa ndani, ila tuliokuwapo ubungo wakatu huo tulimpigia kura (au tudanganyana?)
(hearsay) Keenja aliamua kuishika manzese, na sehemu zilizo highly populated akatilia msisitizo kwa kila hali, kuanzia khanga, tshirts, kofia mpaka sherehe na vikao vya usiku(niliona baadhi). Sikuona tshirt ya mnyika.
Mnyika alizunguka sana tangu mwanzo, jimbo zima akaeleweka vizuri kabisa, akapendeka, Keenja alikwama mwanzoni kabisa ila mwishoni akawateka watu kwa mshtukizo kwa ahadi na zawadi, wakamuhama mnyika.
hiyo ni hoja tuliojipa wakati ule baada ya kuona kura hazikutimia.
Anyway, bado tunajua wewe ndio ulifaa. Ukitumia nguvu ile hadi mwisho pia safari hii mtapata. Labda asije keenja. aje kijana kama wewe toka ccm.
 
Jamani naomba kujua je Mnyika alipata kura kiasi gani ukilinganisha na mpinzani wake?. hilo ni mhimu sana katika kujipanga upya kipute kijacho. samahani sana kuwaridisha 2005, lakini humu ndani ya JF lazima hizo data mnazo tafadhali kwa faida yangu na wengine wenye wazo kama lakwangu.
Natanguliza shukrani
 
Ninavyofahamu kidogo kuhusu uchaguzi huu (2005), Keenja kama ilivyokuwa kwa Rita kule Kawe walisaidiwa sana na KABILA yao ambao wametapakaa sana kwenye MAJIMBO haya na wana nguvu kubwa za KIUCHUMI kuanzia mabaa, nyumba za wageni, maduka, ... Jamaa hawa inapofika kuchagua kati ya CHAMA au KABILA huchagua KABILA.
 
ni ahadi gani hizo na zawadi alizotoa keenja? najua hela za epa zilikuwa kazini hapo.

2010 hakuna hela za EPA, hakuna mabavu ya Nkapa, hakuna kampeni za Malecela, may be wapinzani wataanza kuwika!!!! Lakini mpaka sasa sielewi kwa nini Dar yote iko chi ya CCM!!!
 
Ninavyofahamu kidogo kuhusu uchaguzi huu (2005), Keenja kama ilivyokuwa kwa Rita kule Kawe walisaidiwa sana na KABILA yao ambao wametapakaa sana kwenye MAJIMBO haya na wana nguvu kubwa za KIUCHUMI kuanzia mabaa, nyumba za wageni, maduka, ... Jamaa hawa inapofika kuchagua kati ya CHAMA au KABILA huchagua KABILA.

Inawezekana kabisa ila hawatofautiani na wadau walee wanaotumia ndizi za matoke...kashozi kule..Mnyika alishindwa kwa tofauti ya kubwa kiasi nadhan kama kura 90,000+
 
Ninavyofahamu kidogo kuhusu uchaguzi huu (2005), Keenja kama ilivyokuwa kwa Rita kule Kawe walisaidiwa sana na KABILA yao ambao wametapakaa sana kwenye MAJIMBO haya na wana nguvu kubwa za KIUCHUMI kuanzia mabaa, nyumba za wageni, maduka, ... Jamaa hawa inapofika kuchagua kati ya CHAMA au KABILA huchagua KABILA.

ni ukweli usiopingika
 
Inawezekana kabisa ila hawatofautiani na wadau walee wanaotumia ndizi za matoke...kashozi kule..Mnyika alishindwa kwa tofauti ya kubwa kiasi nadhan kama kura 90,000+

hiyo tofauti ni kubwa sana, kama unavyosema ambao ni ukweli kabila lake lilimsaidia, ataweza kushinda uchaguzi ujao iwapo atagombea mtu mwingine tofauti na huyu Keenja, ambaye atapita tena kwa hiyo influence.
 
Lakini mpaka sasa sielewi kwa nini Dar yote iko chi ya CCM!!!

Mkuu zero hili swali mimi huwa najiuliza sana, maana hata kwenye zile nchi zenye demokrasia kiduchu kama Zimbabwe, Ethiopia, Cameroon na hata Sierra Leone mji mkuu huwa na majimbo/ maeneo yanashikwa na upinzani lakini DAR ni kwa nini????????
 
Mkuu zero hili swali mimi huwa najiuliza sana, maana hata kwenye zile nchi zenye demokrasia kiduchu kama Zimbabwe, Ethiopia, Cameroon na hata Sierra Leone mji mkuu huwa na majimbo/ maeneo yanashikwa na upinzani lakini DAR ni kwa nini????????

Ukichunguza vizuri huko yametumika MAKABILA au DINI. Mnayataka haya hapa kwetu Tz?
 
Kwa kuangalia haraka haraka na kupembua kauli za wachangiaji, inaelekea kikubwa kilikuwa Strategy.

Nafikiri ni Haika aliyesema kuwa Keenja alikwenda Manzese na kutangaza sera, mahali ambako "walalahoi" inasemekana (maneno yangu si Haika kuhusu Walalahoi), wako, je ni kwa nini Mnyika hakuwezea nguvu kila kona aliyopita Keenja? Bandika bandua?

Strategy ya Chadema na Mnyika 2005 Ubungo ilikuwa nini?

Je inawezekana alichokuwa anakiuza Mnyika na Chadema kilikuwa haki-resonate na hali halisi ya jimbo?

Kama ni Pesa, Ukabila na Dini, mnataka kuniambia kuwa sasa tuanze kujijenga kisiasa kwa kutumia nguzo hizo na si Sera zinazoeleweka na kukubalika kwa Wananchi?

Kwa wale wa CCM kina Kada Mpinzani, Paparazi Muwazi, tuambieni mliwezaje kumpiga mtama Mnyika wetu?

What should Mnyika do differently 2010 if he goes for Ubungo again?

Tuendelee wakati tunamsubiri Mnyika hata wenzake Asha na Zitto watuletee majibu.
 
Ni vyema Mnyika aje kutupa maoni yake, mimi nina maoni yangu ambayo naomba kuyareserve mpaka Mnyika mwenyewe akishachangia. Kwa changamoto tu, tujaribu kufikiria hypothetical situation ambapo Mnyika anagombea kwa kupitia CCM na Keenja anagombea kwa kupitia CHADEMA then tunaweza kuona tatizo kuu lilipo ingawa sababu za kushindwa zinaweza kuwa nyingi.
 
Mkuu zero hili swali mimi huwa najiuliza sana, maana hata kwenye zile nchi zenye demokrasia kiduchu kama Zimbabwe, Ethiopia, Cameroon na hata Sierra Leone mji mkuu huwa na majimbo/ maeneo yanashikwa na upinzani lakini DAR ni kwa nini????????

Jibu la swali lako linapatikana kwenye wabunge wenyewe,

Angalia wabunge wa ccm Dar kisha uwalinganishe na wale wa mikoani ndipo ujue kinachoendelea.
 
Ni vyema Mnyika aje kutupa maoni yake, mimi nina maoni yangu ambayo naomba kuyareserve mpaka Mnyika mwenyewe akishachangia. Kwa changamoto tu, tujaribu kufikiria hypothetical situation ambapo Mnyika anagombea kwa kupitia CCM na Keenja anagombea kwa kupitia CHADEMA then tunaweza kuona tatizo kuu lilipo ingawa sababu za kushindwa zinaweza kuwa nyingi.

Kama jimbo ni Ubungo, Keenja bado ATAPETA. Wanaodhani UKABILA haupo au sio kigezo muhimu katika chaguzi zetu wajiulize ni kwa nini karibu kila mtu anakwenda kugombea KWAO alikozaliwa.
Hali haikuwa hivyo wakati ule wa ukoloni ambako akina Mwalimu, Rashidi, Jamal,Dereck Brycone wanagombea.
 
Nijuavyo mimi na ballot paper ilichangia, naam kwa ujumla iliyo leteleza kishindo cha asilimia 80! ukipiga hapa, ukikunja v inahamia kwingine, Chinese technlogy at his best!

Note: Kuna kituo kimoja mgombea alijipigia kura, matokeo yakaonyesha kituo hicho chama chake kilipata kura 0; na hapo je?

Ila 2010 si mbali labda itokee EPA nyingine.
 
Ngoja tumsibiri atupe majibu ya uhakika..ila kwa upande wangu najua ccm walifanya maruhani kama kule znz.
 
Back
Top Bottom