Iwe sharti wanaume kuhamisha mali kwa watoto wa mwanzo kabla ya kuoa mke mwingine ili kuepusha dhuluma kwenye urithi baada ya kufariki

Unakuta mamtu mazima nayo yanagombania mali za urithi na watoto wadogo........hadi mnakuwa watu wazima mzee ameshawapa michongo yote au mmeshatafuta dili zenu, mali za urithi achieni watoto wadogo au zisimamieni kwa niaba yao.
Umeandika kitu usichokuwa na uelewa nacho, endelea kujifunza duniani kuna haki na kuna wajibu, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, halafu unafuata wajibu.
 
Binafsi nimeona kabla mwanaume hajaoa mwanamke mwengine (hasa hawa wazee wanao oa mabinti) , ingependeza haya mambo ya urithi yawe wazi ili kuepusha shari huko mbele, hii itakuwa kama bima ya kuwakinga watoto wa mwanzo kudhulumiwa urithi wao.

Baada ya ndoa wanawake huwa wanajiongeza sana kutumia mbinu kadha na kadha kumtawala mwanaume kwenye suala la kuhakikisha mali zote zinabaki kwake yeye na watoto wake, baada ya kifo watoto wa mwanzo hujikuta hawana chao kwenye urithi wa baba yao, hii kitu inauma sana jamani.

nadhani kuwe na sheria za kuwalinda watoto wa mwanzo, kama baba anataka kuoa ni sawa haina shida lakini alazimishwe kuwajibika linapokuja swala la watoto wake wa mwanzo

Mifano ipo mingi sana ila kwa watu maarufu ni kama

1. Watoto wa marehemu Mengi wa mwanzo walivyotaka kunyimwa urithi, urithi karibu wote ungeenda kwa mama yao wa kambo, ilibidi wapambane sana kupata haki yao.

2. Watoto wa Marehemu Likwelile, ambao sasa wanapitia msoto, Mama yao wa kambo ni Vicky Kamata ambae kajihamishia uriithi huku watoto wa mwanzo wakiwa hoi bin taaban.

3. Watoto wa Marehemu Kimambi nao walipitia huu msoto, ilibidi wafike huko mahakamani wayamalize ila bila hivyo, mama wa kambo alikuwa anazoa kila kitu.
Wewe ukihamisha ya kwako kuna shida?
 
Umeandika kitu usichokuwa na uelewa nacho, endelea kujifunza duniani kuna haki na kuna wajibu, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, halafu unafuata wajibu.
Kuna zee moja lina zaidi ya miaka 70 lilikuwa linagombania eneo ambalo ni moja ya maeneo ya mzee wao na kijana mdogo wa miaka 25 ambaye ni mtoto wa uzeeni wa baba yake tena mbele ya baba yao...........aisee niliona kuna mamtu hayana akili kabisa, miaka 70 umeshindwa kutafuta maeneo yako hadi ugombee maeneo ya baba yako.
 
Kuna zee moja lina zaidi ya miaka 70 lilikuwa linagombania eneo ambalo ni moja ya maeneo ya mzee wao na kijana mdogo wa miaka 25 ambaye ni mtoto wa uzeeni wa baba yake tena mbele ya baba yao...........aisee niliona kuna mamtu hayana akili kabisa, miaka 70 umeshindwa kutafuta maeneo yako hadi ugombee maeneo ya baba yako.
Wote wawili wana matatizo, huwezi kugombea mali ya mtu aliye hai, hakuna urithi wa mali ya mtu aliye hai.
 
Bakhresa ana akili nyingi pale kila mtoto kampa kampuni yake within the group.

Hamna kugombaniana mali kila mtu kapewa shavu mfano Yusuph yuko na mchongo wote wa majini na investment za Zanzibar ile mijumba na Hotel Verde.
Na wewe G-Funk! Umeishapewa mgao wako?
 
Nadhani ni wakati muafaka wa washua kujifunza kugawa mali zao kabla hawajadedi ili kuzuia vurugu.

Pia suala la pre-nup n muhim katika ndoa hasa hasa za uzeeni, maana hapo bi mdogo anaingia ndani akiwa anajua kbsa atakachoondoka nacho.

Sema kibongo bongo umwinyi mwingi! Wazee vichwa ngumu
 
Unakuta mamtu mazima nayo yanagombania mali za urithi na watoto wadogo........hadi mnakuwa watu wazima mzee ameshawapa michongo yote au mmeshatafuta dili zenu, mali za urithi achieni watoto wadogo au zisimamieni kwa niaba yao.
NDuGU Kama wewe hukuachiwa urithi acha wenye urithi wapambne.

Mali ya mdingi au Maza uziachie kienyeji tu ndugu kweli??

Wafaidi watu hta ambao hawahusik...

Utapenda hili litokee Kwa watoto wako huko mbele. ??
 
KWA SHERIA ZA TANZANIA, WATOTO HAWANA HAKI YA KURITH MALI ZA WAZAZI.

WAZAZI WANA WAJIBU WA KULEA MTOTO MPAKA PALE WATAKAPO WEZA KUJITEGEMEA.


HIVI HAO WATOTO WA MKE WA KWANZA WASIPO KUWA WA KWANGU?
 
KWA SHERIA ZA TANZANIA, WATOTO HAWANA HAKI YA KURITH MALI ZA WAZAZI.

WAZAZI WANA WAJIBU WA KULEA MTOTO MPAKA PALE TAKAPO WEZA KUJITEGEMEA.


HIVI HAO WATOTO WA MKE WA KWANZA WASIPO KUWA WA KWANGU?
Sheria za vijiweni huwa hazitambuliki mahakamani....
 
Binafsi nimeona kabla mwanaume hajaoa mwanamke mwengine (hasa hawa wazee wanao oa mabinti) , ingependeza haya mambo ya urithi yawe wazi ili kuepusha shari huko mbele, hii itakuwa kama bima ya kuwakinga watoto wa mwanzo kudhulumiwa urithi wao.

Siku hizi pia kumekua na trend ya wazee wanaoamua kuoa mabinti wadogo wakidhani wamepata kumbe wao ndio wamepatikana, binti anakua amehapiga hesabu zake anajua kabisa huyu mzee ni tajiri na havuki miaka 10 kwisha habari, Hapa binti atamzuzuzua kwa mapenzi moto moto huyo mzee mpaka mzee anajikuta anatoa mali zote, mzee akiwa mgumu basi anapigwa juju na malimbwata ya kumhamisha akili kushoto ili ahamishe mali kwa huyo binti.

nadhani kuwe na sheria za kuwalinda watoto wa mwanzo, kama baba anataka kuoa ni sawa haina shida lakini alazimishwe kuwajibika linapokuja swala la watoto wake wa mwanzo

Mifano ipo mingi sana ila hii ni michach

1. Watoto wa marehemu Mengi wa mwanzo walivyotaka kunyimwa urithi, urithi karibu wote ungeenda kwa mama yao wa kambo, ilibidi wapambane sana kupata haki yao.

2. Watoto wa Marehemu Likwelile, ambao sasa wanapitia msoto, Mama yao wa kambo ni Vicky Kamata ambae kajihamishia uriithi huku watoto wa mwanzo wakiwa hoi bin taaban.

3. Watoto wa Marehemu Kimambi nao walipitia huu msoto, ilibidi wafike huko mahakamani wayamalize ila bila hivyo, mama wa kambo alikuwa anazoa kila kitu.

4. Nakumbuka mwenzetu tuliekuwa tunasomanae chuoni alikatisha masomo yake mwaka wa pili baada ya baba yake kufariki kwa sababu mali zote zilienda kwa mama yao wa kambo ambae aliacha hata kumlipia ada na kumpa hela za matunzo.

5. Mzee Mrema, pongezi kwako, nimeona habari unakaribia kuoa binti lakini jitahadhari please.


Urithi ni haki ya watoto, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, Hata kama mtoto wa mwanzo anatembelea mkongojo na mtoto mwengine anatambaa, wote wana haki ya urithi wa mali za baba yao.
Mtu hawajibiki kufanya hivyo, inshort tafuta mali zako, hizo zake mwache azitumie atakavyo, si zake?! Wewe tafuta za kwako!!
 
Mtu hawajibiki kufanya hivyo, inshort tafuta mali zako, hizo zake mwache azitumie atakavyo, si zake?! Wewe tafuta za kwako!!
Ni kitu rahisi sana mkuu, kama hutaki kurithisha kitu nenda hospitalini kakate hio mishipa ya korodani, hutakuja kuwa na watoto, uta enjoy sana mali zako...
 
Binafsi nimeona kabla mwanaume hajaoa mwanamke mwengine (hasa hawa wazee wanao oa mabinti) , ingependeza haya mambo ya urithi yawe wazi ili kuepusha shari huko mbele, hii itakuwa kama bima ya kuwakinga watoto wa mwanzo kudhulumiwa urithi wao.

Siku hizi pia kumekua na trend ya wazee wanaoamua kuoa mabinti wadogo wakidhani wamepata kumbe wao ndio wamepatikana, binti anakua amehapiga hesabu zake anajua kabisa huyu mzee ni tajiri na havuki miaka 10 kwisha habari, Hapa binti atamzuzuzua kwa mapenzi moto moto huyo mzee mpaka mzee anajikuta anatoa mali zote, mzee akiwa mgumu basi anapigwa juju na malimbwata ya kumhamisha akili kushoto ili ahamishe mali kwa huyo binti.

nadhani kuwe na sheria za kuwalinda watoto wa mwanzo, kama baba anataka kuoa ni sawa haina shida lakini alazimishwe kuwajibika linapokuja swala la watoto wake wa mwanzo

Mifano ipo mingi sana ila hii ni michach

1. Watoto wa marehemu Mengi wa mwanzo walivyotaka kunyimwa urithi, urithi karibu wote ungeenda kwa mama yao wa kambo, ilibidi wapambane sana kupata haki yao.

2. Watoto wa Marehemu Likwelile, ambao sasa wanapitia msoto, Mama yao wa kambo ni Vicky Kamata ambae kajihamishia uriithi huku watoto wa mwanzo wakiwa hoi bin taaban.

3. Watoto wa Marehemu Kimambi nao walipitia huu msoto, ilibidi wafike huko mahakamani wayamalize ila bila hivyo, mama wa kambo alikuwa anazoa kila kitu.

4. Nakumbuka mwenzetu tuliekuwa tunasomanae chuoni alikatisha masomo yake mwaka wa pili baada ya baba yake kufariki kwa sababu mali zote zilienda kwa mama yao wa kambo ambae aliacha hata kumlipia ada na kumpa hela za matunzo.

5. Mzee Mrema, pongezi kwako, nimeona habari unakaribia kuoa binti lakini jitahadhari please.


Urithi ni haki ya watoto, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, Hata kama mtoto wa mwanzo anatembelea mkongojo na mtoto mwengine anatambaa, wote wana haki ya urithi wa mali za baba yao.
Tufanye kazi ,tuache kujiita watoto japo tuna umri wa kustaaf
 
Ni kitu rahisi sana mkuu, kama hutaki kurithisha kitu nenda hospitalini kakate hio mishipa ya korodani, hutakuja kuwa na watoto, uta enjoy sana mali zako...
Kuzaa na Kurithisha ni vitu viwili tofauti, ukizaa unawajibika kumtunza huyo mtoto kwa malazi, chakula, nguo, elimu na afya hadi atakapotimiza miaka 18. Zaidi ya hapo ni mapenzi yako wewe mwenyewe, ukitaka unaweza ukalilea jitu hadi likafika miaka 50, hukatazwi hayo ni mapenzi yako, lakini si lazima!! Hali kadhalika kumpa mtu urithi ingali upo hai si lazima, ni uamuzi wako!! Na ukifariki kuna miongozo ya nani atachukua nini na kwa kiwango gani..., ila, mtu chake, atakitumia atakavyo!! Wewe tafuta vya kwako!!!
 
Binafsi naamini ni busara kufa nikiwa nimewaachia watoto Mali....

sioni haja kwa nini watoto waje kutanga tanga baada ya Kifo changu ingali nilikuwa na nafasi ya kuwaachia kitu flani
Kuna muda Watoto wanazinguwa hadi kuna Madingi wengine wako radhi hata Mali zao zichukuliwe na Msikiti ama kanisa!!
 
Binafsi nimeona kabla mwanaume hajaoa mwanamke mwengine (hasa hawa wazee wanao oa mabinti) , ingependeza haya mambo ya urithi yawe wazi ili kuepusha shari huko mbele, hii itakuwa kama bima ya kuwakinga watoto wa mwanzo kudhulumiwa urithi wao.

Siku hizi pia kumekua na trend ya wazee wanaoamua kuoa mabinti wadogo wakidhani wamepata kumbe wao ndio wamepatikana, binti anakua amehapiga hesabu zake anajua kabisa huyu mzee ni tajiri na havuki miaka 10 kwisha habari, Hapa binti atamzuzuzua kwa mapenzi moto moto huyo mzee mpaka mzee anajikuta anatoa mali zote, mzee akiwa mgumu basi anapigwa juju na malimbwata ya kumhamisha akili kushoto ili ahamishe mali kwa huyo binti.

nadhani kuwe na sheria za kuwalinda watoto wa mwanzo, kama baba anataka kuoa ni sawa haina shida lakini alazimishwe kuwajibika linapokuja swala la watoto wake wa mwanzo

Mifano ipo mingi sana ila hii ni michach

1. Watoto wa marehemu Mengi wa mwanzo walivyotaka kunyimwa urithi, urithi karibu wote ungeenda kwa mama yao wa kambo, ilibidi wapambane sana kupata haki yao.

2. Watoto wa Marehemu Likwelile, ambao sasa wanapitia msoto, Mama yao wa kambo ni Vicky Kamata ambae kajihamishia uriithi huku watoto wa mwanzo wakiwa hoi bin taaban.

3. Watoto wa Marehemu Kimambi nao walipitia huu msoto, ilibidi wafike huko mahakamani wayamalize ila bila hivyo, mama wa kambo alikuwa anazoa kila kitu.

4. Nakumbuka mwenzetu tuliekuwa tunasomanae chuoni alikatisha masomo yake mwaka wa pili baada ya baba yake kufariki kwa sababu mali zote zilienda kwa mama yao wa kambo ambae aliacha hata kumlipia ada na kumpa hela za matunzo.

5. Mzee Mrema, pongezi kwako, nimeona habari unakaribia kuoa binti lakini jitahadhari please.


Urithi ni haki ya watoto, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, Hata kama mtoto wa mwanzo anatembelea mkongojo na mtoto mwengine anatambaa, wote wana haki ya urithi wa mali za baba yao.
Urithi uandikwe na kifanyike kikao kila mtu a ajue, kama kupinga, pinga wakati mwenye mali yu hai. Isiwe Siri.
 
Urithi uandikwe na kifanyike kikao kila mtu a ajue, kama kupinga, pinga wakati mwenye mali yu hai. Isiwe Siri.
Ukajiroga ukaandika urithi kwenye kikao kama hivyo na kila mnufaika akajua kwamba yeye anachukua nini, i assure you, humalizi mwaka utaondoka hapa duniani kwa namna ya kutatanisha, maana wataona kama wanachekewa kupewa urithi wao kwa kutokufa kwako
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom