Iwe sharti wanaume kuhamisha mali kwa watoto wa mwanzo kabla ya kuoa mke mwingine ili kuepusha dhuluma kwenye urithi baada ya kufariki

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,028
Ishu kuu ni hawa mama wa kambo kuchota kila kitu huku, watoto wa mwanzo wanaambulia patupu...Je ni haki hawa mama wa kambo kuzoa kila kitu?

Binafsi nimeona kabla mwanaume hajaoa mwanamke mwengine (hasa hawa wazee wanao oa mabinti) , ingependeza haya mambo ya urithi yawe wazi ili kuepusha shari huko mbele, hii itakuwa kama bima ya kuwakinga watoto wa mwanzo kudhulumiwa urithi wao.

Siku hizi pia kumekua na trend ya wazee wanaoamua kuoa mabinti wadogo wakidhani wamepata kumbe wao ndio wamepatikana, binti anakua amehapiga hesabu zake anajua kabisa huyu mzee ni tajiri na havuki miaka 10 kwisha habari, Hapa binti atamzuzuzua kwa mapenzi moto moto huyo mzee mpaka mzee anajikuta anatoa mali zote, mzee akiwa mgumu basi anapigwa juju na malimbwata ya kumhamisha akili kushoto ili ahamishe mali kwa huyo binti.

nadhani kuwe na sheria za kuwalinda watoto wa mwanzo, kama baba anataka kuoa ni sawa haina shida lakini alazimishwe kuwajibika linapokuja swala la watoto wake wa mwanzo

Mifano ipo mingi sana ila hii ni michache.

1. Watoto wa marehemu Mengi wa mwanzo walivyotaka kunyimwa urithi, urithi karibu wote ungeenda kwa mama yao wa kambo, ilibidi wapambane sana kupata haki yao.

2. Watoto wa Marehemu Likwelile, ambao sasa wanapitia msoto, Mama yao wa kambo ni Vicky Kamata ambae kajihamishia uriithi huku watoto wa mwanzo wakiwa hoi bin taaban.

3. Watoto wa Marehemu Kimambi nao walipitia huu msoto, ilibidi wafike huko mahakamani wayamalize ila bila hivyo, mama wa kambo alikuwa anazoa kila kitu.

4. Nakumbuka mwenzetu tuliekuwa tunasomanae chuoni alikatisha masomo yake mwaka wa pili baada ya baba yake kufariki kwa sababu mali zote zilienda kwa mama yao wa kambo ambae aliacha hata kumlipia ada na kumpa hela za matunzo.

5. Mzee Mrema, pongezi kwako, nimeona habari unakaribia kuoa binti lakini jitahadhari please.

Urithi ni haki ya watoto, haki ya mtu ni haki yake haijarishi umri, Hata kama mtoto wa mwanzo anatembelea mkongojo na mtoto mwengine anatambaa, wote wana haki ya urithi wa mali za baba yao.
 
Siku vijana mkijua kuwa mali za baba yako sio zako na unajukumu la kutafuta zako dunia itakuwa sehemu salama sana.

Mtajifunza kuwa watafutaji.

Baba amehangaika kutafuta mali mwacheni aamue yeye atampa nani urithi wake.

Vijana wengi huwa mkiwa wakubwa mnaungana na mama kumnyanyapaa baba, anakuwa mnyonge sana katika mji wake.

Kama binadamu anatafuta faraja mahali akipata mtu anaemjali anahamishia mapenzi yake huko, siku akifa mnaanza nongwa.

Si mliaminishwa na mama kuwa baba ni mbaya mkamtenga?

Hakuna na hayupo baba ambae ana mapenzi na upendo kwa familia yake akifa akaacha kuwarithisha mali!
 
Siku vijana mkujua kuwa mali za baba yako sio zako na unajukumu la kutafuta zako dunia itakuwa sehemu salama sana. Mtajifunza kuwa watafutaji.
Kwa hio hii ndio sababu ya Mama wa kambo kujirithisha mali zote na kuwaacha watoto wa mwanzo wasipate chao, hebu peleka ujinga wako pembeni wewe.

Alafu kuna kitu kinaitwa generational wealth, nakushauri ufatilie hilo

Vijana wengi huwa mkiwa wakubwa mnaungana na mama kumnyanyapaa baba, anakuwa mnyonge sana katika mji wake. Kama binadamu anatafuta faraja mahali akipata mtu anaemjali anahamishia mapenzi yake huko, siku akifa mnaanza nongwa. Si mliaminishwa na mama kuwa baba ni mbaya mkamtenga?
What ever the case, hiki sio kisingizio cha watoto wa mwanzo kunyimwa haki yao ya urithi
 
Kwa hio hii ndio sababu ya Mama wa kambo kujirithisha mali zote na kuwaacha watoto wa mwanzo wasipate chao, hebu peleka ujinga wako pembeni wewe..... Alafu kuna kitu kinaitwa generational wealth, nakushauri ufatilie hilo


What ever the case, hiki sio kisingizio cha watoto wa mwanzo kunyimwa haki yao ya urithi
Mjinga mwenyewe
 
Kimsingi mtu aliye hai hana mirathi na alithiwi.

Busara tu kwa hiyari yake akiamuwa kugawa mali zake kwa watoto akiwa hai hilo ni jambo jema zaidi.

Mfano Bakhresa ile kampuni ya Omar packaging amempa mwanae Omar Bakhresa hivyo yani.
Bakhresa ana akili nyingi pale kila mtoto kampa kampuni yake within the group.

Hamna kugombaniana mali kila mtu kapewa shavu mfano Yusuph yuko na mchongo wote wa majini na investment za Zanzibar ile mijumba na Hotel Verde.
 
Kimsingi mtu aliye hai hana mirathi na alithiwi.

Busara tu kwa hiyari yake akiamuwa kugawa mali zake kwa watoto akiwa hai hilo ni jambo jema zaidi.

Mfano Bakhresa ile kampuni ya Omar packaging amempa mwanae Omar Bakhresa hivyo yani.
Huu ndo ukweli.....
 
Kimsingi mtu aliye hai hana mirathi na alithiwi.

Busara tu kwa hiyari yake akiamuwa kugawa mali zake kwa watoto akiwa hai hilo ni jambo jema zaidi.

Mfano Bakhresa ile kampuni ya Omar packaging amempa mwanae Omar Bakhresa hivyo yani.
Kwahiyo mtu anapokufa azikwe na Mali zake, au wewe unadhani kurithi ni kufanya nini?
 
Ifike wakati watu tuelewe mtu chake ni chake....,

Hata akiamua kuwaachia omba omba, so long as alikidhi obligations zake zote (kusomesha kulea na kuhakikisha umekuwa mtu mzima) hayo mengine ni choice yake..

Sasa kama hata mali uliyochuma mwenyewe huwezi kuifanyia choices unazotaka mali ya nini?

Angalizo hapa naongelea mali aliyochuma yeye na sio ile iliyochumwa kwa nguvu ya familia
 
Ifike wakati watu tuelewe mtu chake ni chake.

Hata akiamua kuwaachia omba omba, so long as alikidhi obligations zake zote (kusomesha kulea na kuhakikisha umekuwa mtu mzima) hayo mengine ni choice yake..

Sasa kama hata mali uliyochuma mwenyewe huwezi kuifanyia choices unazotaka mali ya nini ? Angalizo hapa naongelea mali aliyochuma yeye na sio ile iliyochumwa kwa nguvu ya familia
Hayo ulioandika umetoa wapi au mawazo yako kwa nijuavyo hakuna imani yoyote kuanzia za mababu zako au iwe ukristo au uwisilamu hamna kitu Kama hicho isipokua watu wanafanya na Kama wanafanya haikifanyi kua sahihi
 
Unakuta mamtu mazima nayo yanagombania mali za urithi na watoto wadogo........hadi mnakuwa watu wazima mzee ameshawapa michongo yote au mmeshatafuta dili zenu, mali za urithi achieni watoto wadogo au zisimamieni kwa niaba yao.
 
Kwahiyo mtu anapokufa azikwe na Mali zake, au wewe unadhani kurithi ni kufanya nini?
Umeelewa nilichoandika au unakurupuka?

Mtu anapokufa mali zake zinamilikiwa na msimamizi wa Mirathi na kama ni taasisi au kampuni inasimamiwa na Kabidhi wasii Rita.
 
Hayo ulioandika umetoa wapi au mawazo yako kwa nijuavyo hakuna imani yoyote kuanzia za mababu zako au iwe ukristo au uwisilamu hamna kitu Kama hicho isipokua watu wanafanya na Kama wanafanya haikifanyi kua sahihi
Naam ni Mawazo yangu, na Sababu ni Mawazo yangu nakatazwa kufanya kama mawazo yangu. Na mawazo yangu ni kama ifuatavyo:-

Kama mzazi ana obligations zake ambazo inabidi azifanye. Mambo ya shule na malezi (hayo sio ombi wala favor, kama aliweza kuwazaa basi ni lazima awatunze)

Kama individual na kuna mali ambayo sio ya familia (ya kwake binafsi) basi ana haki ya kuitumia unless kuna mtu alisaidia kuitafuta..., Hapa tofautisha mali aliyopata mkiwepo mfano nyumba (huenda mtoto alisaidia hata kumwagilizia na kubeba tofari) ila zile personal things kama zipo basi ni uamuzi wake mtu binafsi wala sio uungwana kumpangia.
 
Back
Top Bottom