ivo 1-0 kaseja...the sagga continua

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
baada ya timu yetu ya taifa kubolonga katika mashindano makubwa na kushindwa kupata nafasi ya kucheza michuano mikubwa ya afrika na kombe la dunia, na mashindano mbalimbali ya soka ulaya na kwengineko kuwa yamekwisha watanzania sasa wamerudi nyumbani kufuatilia kombe la kagame ambalo zamani lilijulikana kama klabu bingwa afrika mashariki na kati.

ni nadra kukuta makipa wenye viwango sawa wanakuwa timu moja na kugombea namba. hii imezoeleka kwa wachezaji wa ndani katika vilabu mbali mbali vya soka na ndo maana wahenga walisema "kuku mmoja hachinjwi na watu wawili". lakni kwa yanga imeonekana kuwa si kitu cha kustusha kwani imetumia gharama nyingi kumnyakuwa kipa kutoka kwa hasimu wake simba bwana juma kaseja al maaruf kama ilala one.

leo napenda kuzungumzia kwa kifupi tu kinyang'anyiro cha kugombea lango katika klabu ya yanga kati ya tanzania one ivo mapunda na ilala one juma kaseja. tathmini za haraka haraka zinaonyesha kuwa yanga mpaka sasa imeshacheza mechi mbili katika kombe hili na kujikusanyia pointi 4, magoli matatu ya kufunga na mawili ya kufungwa.

mabao hayo mawili ya kufungwa alifungwa ilala one juma kaseja, na yote yakitokana na mipira iliyotokana na adhabu, kitu kilichopelekea baadhi ya washabiki wa yanga kusema kama kaseja kaonyesha udhaifu wa kufungwa mipira iliyokufa je itakuwaje siku akipata mashambulizi ya nguvu ya mipira iliyo hai?

na sasa wanajiuliza wakati ivo ameweza kudaka na kuhakikisha yanga wanaondoka na ushindi kitu ambacho ilala one kaseja alishindwa kukifanya basi kwa nini asiaminiwe ivo kupewa milingoti?

kivumbi hiki cha kugombea namba kinaendelea, na kuna matabaka yameshaanza kujitenga mengine yakimtaka ivo huku yakisema "nazi ya muda mrefu mtini ndo iliyo komaa na tayari kwa kuliwa" na mengine yanamtetea kaseja yakisema "hata mbuyu ulianza kama mchicha" na mimi nasema "the sagga continua" na iko siku tutakamilisha ule msemo wa wahenga kuwa "dobi wa kweli utamjua siku akipewa nguo nyeupe" kwani tutamjua wa ukweli ni yupi na kanjanja ni yupi.
 
Last edited:
mkuu gang
mi binafsi simkubali kaseja.
kutokana na ufupi alionao ndio ulisababisha APR kupata goli lile la pili la kusawazisha. na kama hiyo haitoshi makipa woote wakubwa duniani wana vimo virefu tofauti na huyo jamaa. hivyo mi kura yangu naiangushia kwa mngoni mapunda.
 
hapa ishu sio kipa bora ni kwamba Yanga wanataka kuwaonesha simba kuwa wanapesa hii ni mikakati isiyofaa kwa sababu wangeweza kutumia pesa hizo kuwa-motivate wachezaji wao kuliko kujionesha kuwa wanaweza makuu. Bado tuna matatizo ya vision na how to excute it.
 
hapa ishu sio kipa bora ni kwamba Yanga wanataka kuwaonesha simba kuwa wanapesa hii ni mikakati isiyofaa kwa sababu wangeweza kutumia pesa hizo kuwa-motivate wachezaji wao kuliko kujionesha kuwa wanaweza makuu. Bado tuna matatizo ya vision na how to excute it.

kwa hiyo GM huu usajili wa kaseja kama wewe ungekuwa kwenye uongozi wa yanga ungeuchomolea?
 
..............kaseja anajuta kwenda yanga ...kwa sababu kiukweli ..haipendi yanga ..kama anavyosema mwenyewe kafuata pesa....cha pili ni kuwa ameondoka simba ambako alikuwa akiheshimiwa kwa miaka 6 ...kama kipa chaguo namba moja....na kipenzi cha mashabiki....ameenda yanga ambako kazi ya kwanza ngumu inayomkabili ni kujenga imani kwa mashabiki wake wapya.....natabiri mwisho wa kaseja.......

leo kipa aliyechukua namba yake simba ,AMANI simba...ameonekana kumudu mchezo hasa baada ya aliyekuwa akitegemewa kuwa simba namba 1....barthez...kufungwa kirahisi na TUSKER...ni wazi...kuwa simba ni nyumbani kwa makipa na ma strike wazuri ....akitoka dhahabu anakuja almasi.....

kaseja leo alikuwa uwanjani na wenzake wa yanga na alionekana myonge...tofauti na enzi zake simba ambazo zilijaa raha...ni wazi kuwa pesa kapata lakini na kazi anayo.........kama hautakuwa mwisho wake ..mwakani ataomba kurudi simba hata bure....maana mkataba wake na yanga ni mwaka mmoja tu!!!!
 
... alafu nimesahau kusema kuwa leo simba walicheza kama brazil..ni ..ta..ta..ta..ta..hizo ni gonga hizo..walahi kama alivosema waziri kapuya mwaka huu tutawakambisha watu majani bila kuangalia kama wametumia milioni 800 kufanya usajili....
 
Najiuliza mara kwa mara lengo la huyu jamaa kwa hii timu ya jangwani.....
Hafanyi chochote kwa manufaa ya timu, hafanyi kitu cha kuendeleza timu...SUSTAINABILITY HAKUNA.
Kwa uhalisi akisema kuanzia leo Yanga basi, itabidi kina Madega wasahau uanasheria wao na kwenda kumpigia magoti!
 
Najiuliza mara kwa mara lengo la huyu jamaa kwa hii timu ya jangwani.....
Hafanyi chochote kwa manufaa ya timu, hafanyi kitu cha kuendeleza timu...SUSTAINABILITY HAKUNA.
Kwa uhalisi akisema kuanzia leo Yanga basi, itabidi kina Madega wasahau uanasheria wao na kwenda kumpigia magoti!

roya weka wazi huyo jamaa ni nani?
 
Lakini mbona IVO anaondoka zake anaenda kwa Micho na Micho juzi alikuja kushughulikia usajili wake kwa hiyo Kaseja atakuwa huru semeni kikwazo kitakuwa kwa yule kipa Mzungu aliyesajiliwa na Yanga toka Serbia yule hatujajua uwezo wake na huyu ndo atakuwa mwiba mchungu kwa Kaseja.Lakini swala la Ivo ataondoka muda si mrefu na kutumikia St.George ya Ethiopia.
 
Lakini mbona IVO anaondoka zake anaenda kwa Micho na Micho juzi alikuja kushughulikia usajili wake kwa hiyo Kaseja atakuwa huru semeni kikwazo kitakuwa kwa yule kipa Mzungu aliyesajiliwa na Yanga toka Serbia yule hatujajua uwezo wake na huyu ndo atakuwa mwiba mchungu kwa Kaseja.Lakini swala la Ivo ataondoka muda si mrefu na kutumikia St.George ya Ethiopia.

ni mpaka atakapoondoka ndo kaseja atakunywa maji yakashuka.
lakini kwa sasa kazi anayo bado na ndo tunachokizungumzia hapa...
 
au CCM nayo imejikita huko kwenye michezo ndio maana tunaboronga?
Subiri timu yetu moja ichukue kombe la Kagame utamsikia Chiligati anasema ni kutokana na sera nzuri za chama ........................
 
Subiri timu yetu moja ichukue kombe la Kagame utamsikia Chiligati anasema ni kutokana na sera nzuri za chama ........................

kwi! kwi! kwi! kwi!
kweli kabisa saizi kakauka kau kama yupo likizo vile wakinyakua kombe ndo anatoka mafichoni.Sasa sijui CCM inasaidia vp michezo hapa TZ mala kibao tunasikia wizara ya michezo haina pesa kusafirisha wachezaji matatizo kibao sielewe bajeti yao iwa inaishia kwenye nini mifukoni au wapi?Hata hao TFF ni njaa tupu hata waingize mamilioni hapa uwanja mpya matatizo hayaishi.
 
Huko tuinapoelekea, Kaseja na Ivo zitaanza kutembea "ndumba".
Ee Mungu tuepushe hili balaa
 
kwi! kwi! kwi! kwi!
kweli kabisa saizi kakauka kau kama yupo likizo vile wakinyakua kombe ndo anatoka mafichoni.Sasa sijui CCM inasaidia vp michezo hapa TZ mala kibao tunasikia wizara ya michezo haina pesa kusafirisha wachezaji matatizo kibao sielewe bajeti yao iwa inaishia kwenye nini mifukoni au wapi?Hata hao TFF ni njaa tupu hata waingize mamilioni hapa uwanja mpya matatizo hayaishi.

na viwanja vingi vya soka hapa nchini viko chini ya milki yao but kuviendeleza wanashindwakwa nini visirudishwe serikalini?
 
ooooh nimedokezwa
kumbe yanga wana kipa mzungu?
kwa hiyo battle ni kati ya ivo, kaseja na mtasha duh?
 
Huko tuinapoelekea, Kaseja na Ivo zitaanza kutembea "ndumba".
Ee Mungu tuepushe hili balaa

aaaaaaaaaah kwani mpaka tufike huko?
ngoma imeshaanza sasa hivi ila mambo hayajaana itika tu, utasikia oooh fulani ana enka, mara goti, mara mgongo, mwisho kimyaaaa... msimu ujao anasajili mbagala market au mji mpwapwa na ndo mwisho wa soka...mark n bind my word
 
aaaaaaaaaah kwani mpaka tufike huko?
ngoma imeshaanza sasa hivi ila mambo hayajaana itika tu, utasikia oooh fulani ana enka, mara goti, mara mgongo, mwisho kimyaaaa... msimu ujao anasajili mbagala market au mji mpwapwa na ndo mwisho wa soka...mark n bind my word

ikiwa bunge tu wameshindwa kuanika uchawi
nyie huo wa wachezaji mkiombwa kuthibitisha mtaweza?
 
... alafu nimesahau kusema kuwa leo simba walicheza kama brazil..ni ..ta..ta..ta..ta..hizo ni gonga hizo..walahi kama alivosema waziri kapuya mwaka huu tutawakambisha watu majani bila kuangalia kama wametumia milioni 800 kufanya usajili....

mkuu hizo ta...ta...ta...ta....ni baruti au risasi?
hao simba wangekuwa wanazigonga pasi hizo basi tungewaona CAF champios league au hata kombe la shirikisho.
lakini kwa uozo mliouonyesha last season hamna tofauti na JKT ruvu, mji mpwapwa au kagera rangers
 
mkuu hizo ta...ta...ta...ta....ni baruti au risasi?
hao simba wangekuwa wanazigonga pasi hizo basi tungewaona CAF champios league au hata kombe la shirikisho.
lakini kwa uozo mliouonyesha last season hamna tofauti na JKT ruvu, mji mpwapwa au kagera rangers

Nakubali! Sawa tu na AFC Arusha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom