Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Inashangaza chombo cha habari kikubwa kama ITV kinalikosea kuliandika jina la Mwenyeketi wa Tume ya Uchaguzi Jaji Mkuu Mstaafu Damiani Lubuva na kumwita Damian Luduva. Hili nimeliona katika kipindi cha matukio ya wiki ambacho kinaendelea hivi sasa. Kwa vile haya ni matukio ya wiki inamaana kipindi hiki kilirushwa siku za nyuma kati ya jumatatu haji jumamosi ya wiki hii, sina uhakika kama hawakugundua kosa hilo na hivyo kulifanyia masahihisho ama ni udhaifu wa utamkaji wa maneno alionao aliyeandika habari hiyo. Lakini Mhariri wa kipindi naye yuko wapi.