Kiwi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 1,054
- 990
Habari za kazi wanajamvi,
Mimi ni mtazamaji mzuri wa ITV online kwa kuwa siko Tanzania. Jambo moja linalonikera sana ni kwamba taarifa zinazotolewa na ITV zimekuwa finyu zisizokuwa na uchambuzi au 'analysis' ya kutosha. Wanapoongelea jambo lolote hawalifanyii uchambuzi wa kina kama ambavyo unapaswa kufanywa na vyombo vingine vya habari. Muda uliopo wa Taarifa ya Habari ni mrefu wa kutosha kwamba wangeweza kuchambua yale wanayoyatangaza. Mifano halisi ipo kadhaa, mmojawapo ni wanapoonyesha kampeni za uchaguzi Igunga. Hatuhitaji tu kuona yaliyojiri kwa siku hiyo, bali ingekuwa vyema wakatumia dakika chache kuchambua yaliyojiri.
Mfano wa pili juzi walipozungumzia 'typhoon' iliyotokea Philippines. Kwanza wao wameita typhoon kwa kiswahili kuwa ni kimbunga, ambayo siyo sahihi. Tafsiri ya neno 'typhoon' ni tufani na siyo kimbunga. Kimbunga ni 'cyclone' na ni upepo mkali usioambatana na mvua. Kimbunga kinaweza kuezua nyumba lakini hakileti mafuriko!
Mfano wa tatu ni kuhusu kifo cha Prof. Wangari Maathai wa Kenya. ITV walitangaza tu kuwa Prof Maathai amefariki dunia baada ya kuugua kansa. Kwa mtu muhimu kama huyu, aliyekuwa mwanamke wa kwanza mwafrika kupokea tuzo ya Nobel, nilifikiri ITV wangetumia muda kiasi kutoa wasifu wake, hata kumwita mtu aliyemfahamu na kuongelea kwa kifupi kuhusu Prof. Maathai.
Hii yote ni dalili ya kuwa ITV inapokea tu taarifa na kuzitangaza (broadcast) bila utafiti wa kina. Na ikumbukwe kuwa ITV ilikuwa TV station ya kwanza (kama sikosei wakuu) kuanza kazi ya kurusha matangazo hapa Tanzania (Bara). Nilitumaini kuwa itakuwa na uzoefu zaidi wa kazi hiyo na kuifanya iwe bora zaidi kuliko hata TV zingine zilizofuata. Watazamaji tutaendelea kuangalia, lakini tungependa kuona wanajisahihisha, ili kuifanya ITV kuwa kweli chombo cha kutoa habari za uhakika na zenye uchambuzi wa kina. Nina imani ya kuwa uwezo wa kufanya hivyo wanao.
Mimi ni mtazamaji mzuri wa ITV online kwa kuwa siko Tanzania. Jambo moja linalonikera sana ni kwamba taarifa zinazotolewa na ITV zimekuwa finyu zisizokuwa na uchambuzi au 'analysis' ya kutosha. Wanapoongelea jambo lolote hawalifanyii uchambuzi wa kina kama ambavyo unapaswa kufanywa na vyombo vingine vya habari. Muda uliopo wa Taarifa ya Habari ni mrefu wa kutosha kwamba wangeweza kuchambua yale wanayoyatangaza. Mifano halisi ipo kadhaa, mmojawapo ni wanapoonyesha kampeni za uchaguzi Igunga. Hatuhitaji tu kuona yaliyojiri kwa siku hiyo, bali ingekuwa vyema wakatumia dakika chache kuchambua yaliyojiri.
Mfano wa pili juzi walipozungumzia 'typhoon' iliyotokea Philippines. Kwanza wao wameita typhoon kwa kiswahili kuwa ni kimbunga, ambayo siyo sahihi. Tafsiri ya neno 'typhoon' ni tufani na siyo kimbunga. Kimbunga ni 'cyclone' na ni upepo mkali usioambatana na mvua. Kimbunga kinaweza kuezua nyumba lakini hakileti mafuriko!
Mfano wa tatu ni kuhusu kifo cha Prof. Wangari Maathai wa Kenya. ITV walitangaza tu kuwa Prof Maathai amefariki dunia baada ya kuugua kansa. Kwa mtu muhimu kama huyu, aliyekuwa mwanamke wa kwanza mwafrika kupokea tuzo ya Nobel, nilifikiri ITV wangetumia muda kiasi kutoa wasifu wake, hata kumwita mtu aliyemfahamu na kuongelea kwa kifupi kuhusu Prof. Maathai.
Hii yote ni dalili ya kuwa ITV inapokea tu taarifa na kuzitangaza (broadcast) bila utafiti wa kina. Na ikumbukwe kuwa ITV ilikuwa TV station ya kwanza (kama sikosei wakuu) kuanza kazi ya kurusha matangazo hapa Tanzania (Bara). Nilitumaini kuwa itakuwa na uzoefu zaidi wa kazi hiyo na kuifanya iwe bora zaidi kuliko hata TV zingine zilizofuata. Watazamaji tutaendelea kuangalia, lakini tungependa kuona wanajisahihisha, ili kuifanya ITV kuwa kweli chombo cha kutoa habari za uhakika na zenye uchambuzi wa kina. Nina imani ya kuwa uwezo wa kufanya hivyo wanao.