ITV Malumbano ya Hoja: Vyumba vya Madarasa na miundombinu Shule

VAPS

JF-Expert Member
Jul 10, 2012
5,610
13,160
Nashauri wadau serikali wafatilie maoni ya wadau. Machache:

1. Serikali iwe na takwimu na mwelekeo kuweza kupanga mipango.
2. Kushirikikisha wadau sector binafsi.
3. Ikibidi kukopa kujenga miundombinu ya uhakika.
4. Wazazi washirikishwe kuchangia walau sehemu fulani inayohimillika.
5. Uzazi wa mpango ni muhimu kujenga familia inayowajibika.
6. Ubora wa elimu (Quality)
7. Mfumo wa elimu idadi miaka
8. Elimu ya ufundi kuanza ngazi za chini baada ya darasa la tatu
9. Kufuatia sera ya elimu bure na maboresho shule za umma tutarajie mafuriko makubwa zaidi baada miaka 7,2016+7: 2022...
 
Mmnh!
Zamani walikuwa wanafaulu kutokana na nafasi zilizipo sasa siku hizi sijui ni uoga au nini ili wasionekane wame under perform?

Mambo ya michango kwa kweli mtihani.
 
Tuwashauri waache kununua magari ya serikali ya gharama na kukata matumizi mengine yasiyo ya lazima pesa hizo toka kwenye budget zijenge Shule na mabweni.
 
Inasikitisha kuona pesa zile za rasimu ya katiba kama zimepitea bure bora zingejenga madasara na huduma ya maji na mabweni
 
Unajua serikali inaingia gharama kubwa sana ktk kuwalipa watu wengi anbapo kazi ingefanyika kwa mtu mmoja tu.

Matharani;
Wilaya moja inakuwa na
1 . DC
2. DED
3.DAS
4. Mbunge
5. DCO
6. Etc

Hao hapo alitakiwa abaki mmoja au 2 tu

Sasa kila mkoa hivyo, mkoa mmoja una Wilaya chungu nzima , imagine!

Tu tafakari .

Hata kwenye taasisi za Umma baadhi kuna doublications za watu kuingiliana majukumu kwa watu kufanya kazi zile zile na wote kulipwa!
 
Nashauri wadau serikali wafatilie maoni ya wadau. Machache
1. Serikali iwe na takwimu na mwelekeo kuweza kupanga mipango...
Binafsi sifikiri ni haki kuwachangisha wazazi pesa ya kujenga madarasa. Raia wanalipa kodi wanastahili kupata hizi huduma. Kama serikali inaweza kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa chato, inaweza kujenga uwanja wa mpira chato, inaweza kujenga hospitali ya rufaa chato, inaweza kuanzisha mbuga ya wanyama chato, inaweza kununua ndege 10 cash, inaweza kujenga mafly-over nk., na makusanyo tra yameongezeka, wafanyakazi hewa wameondolewa, hakuna ajira mpya, ufisadi umekomeshwa nk; srikali hiyohiyo inashindwa vipi kujenga madarasa?
 
Binafsi sifikiri ni haki kuwachangisha wazazi pesa ya kujenga madarasa. Raia wanalipa kodi wanastahili kupata hizi huduma. Kama serikali inaweza kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa chato, inaweza kujenga uwanja wa mpira chato, inaweza kujenga hospitali ya rufaa chato, inaweza kuanzisha mbuga ya wanyama chato, inaweza kununua ndege 10 cash, inaweza kujenga mafly-over nk., na makusanyo tra yameongezeka, wafanyakazi hewa wameondolewa, hakuna ajira mpya, ufisadi umekomeshwa nk; srikali hiyohiyo inashindwa vipi kujenga madarasa?
2022/3 wahitimu shule msingi, zao la elimu ya bure, ni vyema watakwimu watoe idadi, ni vyema tukawa na vyuo vingi ufundi kila kata vipokee 70%, mbali ya kufikiri kuongeza madarasa sekondari pekee.
 
Back
Top Bottom