ITV kutangaza LIVE Bunge la Afrika Mashariki. Je, ITV sasa ni zaidi ya TV ya Taifa?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,582
Wanabodi,

Nilikuwa naangalia taarifa ya habari ya ITV leo asubuhi na kukutana na habari hii ya ITV kulitangaza Live Bunge la Afrika Mashariki, (japo habari yenyewe ni ndefu zaidi ya dakika 5 ambayo ni kinyume cha kanuni za Radio/TV News Clip), habari hii ni habari njema sana kwa Watanzania, sio tuu ili kulifahamu zaidi hili Bunge la Afrika Mashariki, bali pia Watanzania watapata fursa ya kuufahamu zaidi Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tukubali, tukatae, Watanzania tuko nyuma nyuma katika kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana kwa Mtangamano wa Afrika Mashariki, hivyo kitendo cha vyombo vya habari vya IPP, kulitangaza live vikao vya Bunge la Afrika Mashariki, kinastahili pongezi za dhati!.

Na kwakufanya hivyo, Kituo cha ITV sasa, licha ya kuwa ni chombo cha habari cha binafsi, kwa kulitangaza live Bunge la Afrika Mashariki, ITV sasa inafanya kazi ambayo ingepaswa kufanywa na vyombo vya habari vya umma, hivyo sasa ITV ni zaidi ya Televisheni ya Taifa!.

Tangu kuasisiwa kwa Jumuiya mpya ya Afrika Mashariki na kuundwa kwa Bunge la Afrika Mashariki, hii ndio mara ya kwanza katika maisha ya bunge hili, kuendesha kikao chake jijini Dar es Salaam.

Japo siko ndani ya Sekretariati ya Afrika Mashariki, EALA, au Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naamini EALA walituma maombi kwa Televisheni ya Taifa (TBC) kuiomba TBC kulitangaza live bunge hili, TBC itakuwa ilitoa majibu kuwa hili haliwezekani kwa sababu kikao hiki cha EALA kitakuwa kinakwenda sambamba na vikao vya Bunge la Katiba ambavyo TBC inalitangaza live, hivyo its logical kwa TBC haiwezi kutangaza live mabunge mawili yaliyo sehemu tofauti kwa wakati mmoja!, hivyo EALA wakapeleka maombi kwa Mzee Mengi, wakakubaliwa!.

Kwa maoni yangu, licha ya TBC kulitangaza live Bunge la Katiba, bado TBC has the capacity kulitangaza live na Bunge la Afrika Mashariki kupitia Chaneli yake ya pili ya TBC 2, kwa sababu hata ITV wenyewe unaweza kukuta watalitangaza Bunge hili la Afrika Mashariki kupitia EATV ili kupunguza loss of revenue kama watatumia ITV kulitangaza Bunge hili, then watafuta vipindi vyote kwa siku zote hizo za bunge hilo, kitu ambacho I don't ni kitu rahisi!.

Hongera sana Mzee Reginald Mengi, Hongera vyombo vya habari vya IPP, Hongera ITV!,
Jee mtakubaliana na mimi kuwa sasa ITV ni zaidi ya TBC?!.

Wasalaam.

Pasco

====http://youtu.be/Skuo2Bk2VoA=========================


Dr Reginald Mengi amesema ushirikiano wa Afrika mashariki uwe wa wananchi wa nchi wanachama

ippleo.png

Mwenyekiti mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi amewataka wabunge wa bunge la Afrika mashiriki kuhahikisha kuwa ushirikiano wa Afrika mashariki hauwi wa viongozi pekee bali uwe wa wananchi wa nchi wanachama.

Mwenyekiti mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa chakula cha mchana alichowaandalia wabunge wa bunge la Afrika mashariki baada ya kutembelea vyombo vya habari vya IPP kushuhudia jinsi vinavyofanya kazi.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo spika wa bunge hilo Mhe. Dr. Margareth Ziwa ameviomba vyombo vya habari sema wabunge wa Afrika mashariki wanao kama wabunge wana majukumueliza mwenyekiti wa wabunge wa afrika mashariki kutoka tanzania Mhe. Adam Kimbisa ameomba vyombo vya habari vya ipp na tanzania kwa ujumla vifuatilie shughuli za bunge hilo litakalofanya vikao vyao kwa mara ya kwanza jijini Dar es Salaam ili kuwawezesha wananchi kufahamu kinachojili bungeni humo.

Kamati ya uongozi ya bunge la Afrika mashariki imetembelea vyombo vya habari vya IPP na kujionena namna vinavyofanya kazi ambapo spika wa bunge hilo Mh Margret ziwa ameviomba vyombo hivyo kuripoti mkutano wa bunge hilo unaotarajiwa kuanza jumatano ya wiki ijayo jijini Dar es Salaam.

Ziara ya wabunge hao imeanzia katika ofisi za The Guardian ambapo walipokewa na mkurugenzi mtendaji bw kiondo mshana ambapo aliwatembeza katika maeneo mbalimbali ya kampuni hiyo na kuwapatia maelezo huku akiita ziara ya wabunge hao ni tukio la heshima kwa kampuni za ipp na nchi kwa jumla.

Baada ya kutembelea katika upande wa uchapishaji wa magazeti wabunge hao walitembelea vituo vya utangazani vya east african televisheni na redio, redio one na capital redio kisha itv na kupatiwa maelezzo kutoka kwa wakuu wa idara.

Mwenyekiti wa chapter ya Tanzania katika bunge hilo mh adamu kimbisa amesema umefika wakati kwa vyombo vya habari kufuatilia kwa kina mambo yanayofanywa katika bunge hilo kama kweli ipo nia ya dhati ya kuona jumuiya ya afrika mashariki inakuwa.

Kwa upande wake Mh spika amesema wao kama wabunge wanajukumu kubwa la kusimamia na kuweka mambo sawa japo wao kama binadamu kuna mambo yanaweza yasiwe sawa na hivyo ndio nafasi nzuri kwa vyombo vya habari kulisaidia bunge na jumuiya kwa ujumla kukua.

[video=youtube_share;Skuo2Bk2VoA]http://youtu.be/Skuo2Bk2VoA[/video]
 
R.mengi kweli ana mambo mengi mazuri na yenye tija kwa umma wa watanzania.
Sasa mzee s.sitta alikuwa amekunywa viroba gani hadi akajitangazia mgogoro na ipp media? Kweli six kichwa box.
Hongera mzee mengi kwa kuonyesha uzalendo wa kweli ambao unapatikana kwa matajiri wachache sana duniani.
 
IPP ni zaidi ya baraza zima la JK kiutendaji. Na siwezi kabisa kuilinganisha ITV dhidi ya TBC kwani vi vyombo viwili vilivyoachana kwa mbali sana kiutendaji na kifikra, yani ni kama kuilinganisha Chalinze na London.

Kwa kifupi niseme sasa ITV inaikaribiba BBC ,CNN, ALJAZEERA nk.
 
IPP ni zaidi ya baraza zima la JK kiutendaji. Na siwezi kabisa kuilinganisha ITV dhidi ya TBC kwani vi vyombo viwili vilivyoachana kwa mbali sana kiutendaji na kifikra, yani ni kama kuilinganisha Chalinze na London.

Kwa kifupi niseme sasa ITV inaikaribiba BBC ,CNN, ALJAZEERA nk.
Wachagga mnavyopenda sifa za kijinga
 
R.mengi kweli ana mambo mengi mazuri na yenye tija kwa umma wa watanzania.
Sasa mzee s.sitta alikuwa amekunywa viroba gani hadi akajitangazia mgogoro na ipp media? Kweli six kichwa box.
Hongera mzee mengi kwa kuonyesha uzalendo wa kweli ambao unapatikana kwa matajiri wachache sana duniani.

Kumbe Itv wanafanya hivyo kutokana na SITTA kusema ukweli juu ya hujuma za Itv kwenye bunge la matiba?.SITTA anaathirika vipi na uamuzi huo wa mangi?
 
umeshasema bunge la afrika mashariki, lina uhusiano gani taifa, kwani nini usihoji KBC au UBC kutotangaza bunge hilo?
Wachagga mnavyopenda sifa za kijinga

Kumbe Itv wanafanya hivyo kutokana na SITTA kusema ukweli juu ya hujuma za Itv kwenye bunge la matiba?.SITTA anaathirika vipi na uamuzi huo wa mangi?


kuwa mwanaccm isiwe ndio ishara ya kutokuwa na uwezo wa kufikiri nakupembua mambo.
 
Pasco nakubaliana na wewe baada ya TBC "kupoteza nafasi/hadhi" yake kama chombo cha habari cha taifa na baada StarTV kuanza kutumika kisiasa kwa manufaa ya chama tawala, sasa ITV inaonekana kuwa kituo kinachopendwa na kuaminiwa na watz wengi katika kusimamia maslahi mapana ya taifa kwa hivyo naunga mkono hoja yako: ITV ni kituo cha habari cha taifa kwa sasa.
 
ITV ni kama televisheni teule ya Taifa (Disignated National Broadcasting Corporation)
Wakati ITV wanaonyesha midahalo ya katiba TBC inarusha cherekochereko.

ITV wanatakiwa waanze kupewa ruzuku kwa kuhabarisha umma.

Wewe ni miongoni mwa vichwa hapa JF ambavyo vinawakilisha maana halisi ya JF, "a home of great thinkers". You are a Great Thinker Dude!!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
R.mengi kweli ana mambo mengi mazuri na yenye tija kwa umma wa watanzania.
Sasa mzee s.sitta alikuwa amekunywa viroba gani hadi akajitangazia mgogoro na ipp media? Kweli six kichwa box.
Hongera mzee mengi kwa kuonyesha uzalendo wa kweli ambao unapatikana kwa matajiri wachache sana duniani.

Baba wawili ana bonge la pua,kama sunche na kapeto
 
IPP ni zaidi ya baraza zima la JK kiutendaji. Na siwezi kabisa kuilinganisha ITV dhidi ya TBC kwani vi vyombo viwili vilivyoachana kwa mbali sana kiutendaji na kifikra, yani ni kama kuilinganisha Chalinze na London.

Kwa kifupi niseme sasa ITV inaikaribiba BBC ,CNN, ALJAZEERA nk.

Kama hujarogwa basi utakuwa umechanganya gongo na ugoro, cnn,bbc wenye wawakilishi dunia nzima? Ipp inayoongoza kwa kulipa mishahara inayotosha kutumia kwa wiki moja na kiasi kingine serikali inachangia kupitia bahasha za khaki?@pasco
 
thatha;
Kumbe Itv wanafanya hivyo kutokana na SITTA kusema ukweli juu ya hujuma za Itv kwenye bunge la matiba?.SITTA anaathirika vipi na uamuzi huo wa mangi?



WEWE KILAZA thatha hapo bluu ndio bunge gani hilo? au Umenyweshwa mataputapu na Kinena leo badala ya wali maharage hapo Lumumba fc?
 
Last edited by a moderator:
ITV ni chombo cha habari kinachorafuta habari zenye manufaa kwa taifa wakati TBC ni chombo cha habari kinachoeneza propaganda na siasa za CCM.Habari za Bunge la Katiba ni moja wapo ya siasa chafu za CCM ambazo TBC hupenda kuzichangamkia,Habari za Bunge la Afrika Mashariki hazina manufaa kwa CCM na hivyo hivyo kwa TBC pia wakati kiuhalisia ndizo habari ambazo Watanzania wanapaswa kujuzwa.Hiyo ndiyo tofauti kati ya TBC na ITV.
 
Back
Top Bottom