It's time we burst the Pandora Box!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Wakati wa Azimio tulisema ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora.

Hali halisi ya sasa hivi ya Tanzania inatubidi turudi tena na kujiuliza ili tuende tunahitaji nini?

Tunahitaji Pandora Box la Tanzania livunjwe, vilivyomo ndani vianikwe!

Hatutaweza kuendelea na kupiga hatua kama hatuta chukua hatua hii madhubuti, ngumu na chungu kujua ukweli wa yaliyotusibu na kutufikisha hapa tulipo.

Huu uoga wa nchi kuyumba, ohh mtikisiko utatishia Amani, Utulivu, Mshikamano na Demokrasia yetu ni UNAFIKI mtupu ambao unaendelea kutudumaza kwa kutufanya waoga, kuhofia ukweli.

Tuliimba nitasema Kweli Daima, Fitina kwangu ni Mwiko, ni wakati tudai haki zetu kutoka kwa Serikali na Watawala.

Ili tuendelee kama Taifa tunahitaji vifuatavyo;

  • Ukweli na Uwazi kuhusu Uhujumu wa BOT
  • Ukweli na Uwazi kuhusu sakata la Zanzibar na Mwafaka
  • Ukweli na Uwazi kuhusu Uhujumu na Uzembe uliotuletea IPTL, ATCL, NMB, TRL, RICHMOND
  • Ukweli kuhusu mikataba yote ya Madini
  • Ripoti ya Warioba ya mambo ya Rushwa
  • Maelezo ya Rostam yaliyozuiwa na CCM kuhusu Richmond
  • Ukweli kuhusu Chenge na Vijisenti vyake kuhusiana na kashfa ya Radar
  • Ukweli na uwazi kuhusu mauaji ya Mwembechai, Zanzibar, Bulyanhulu na kwenye migodi mingine
  • Ukweli na Uwazi kuhusu Mapato na matumizi ya Serikali
  • Ukweli na Uwazi kuhusu mali za Viongozi wote wa Serikali tangu mwaka 1992
  • Ukweli na Uwazi kuhusu nia ya kuundwa kwa Katiba mpya
  • Ukweli na Uwazi kuhusu sera za Uwekezaji, misamaha ya kodi na ushuru kwa wawekezaji
Tusipoupata ukweli pamoja na uchungu wake, kamwe hatutaweza kupiga hatua kama Taifa. Pamoja na kujua Ukweli huu, tuwe tayari wote kama Taifa kwa matokeo ya juhudi hizi.

The Pandora box has to be opened. For our country to make steady progress in development and bring back accountability, the Pandora Box has to burst open.

Yes there will be blood, tears and teeth gnashing.

However without those things to happen, we will never have a chance to have a positive reflection to shape up our new direction towards maendeleo na uwajibikaji.
 
Wakati wa Azimio tulisema ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora.

Hali halisi ya sasa hivi ya Tanzania inatubidi turudi tena na kujiuliza ili tuende tunahitaji nini?

Tunahitaji Pandora Box la Tanzania livunjwe, vilivyomo ndani vianikwe!

Hatutaweza kuendelea na kupiga hatua kama hatuta chukua hatua hii madhubuti, ngumu na chungu kujua ukweli wa yaliyotusibu na kutufikisha hapa tulipo.

Huu uoga wa nchi kuyumba, ohh mtikisiko utatishia Amani, Utulivu, Mshikamano na Demokrasia yetu ni UNAFIKI mtupu ambao unaendelea kutudumaza kwa kutufanya waoga, kuhofia ukweli.

Tuliimba nitasema Kweli Daima, Fitina kwangu ni Mwiko, ni wakati tudai haki zetu kutoka kwa Serikali na Watawala.

Ili tuendelee kama Taifa tunahitaji vifuatavyo;

  • Ukweli na Uwazi kuhusu Uhujumu wa BOT
  • Ukweli na Uwazi kuhusu sakata la Zanzibar na Mwafaka
  • Ukweli na Uwazi kuhusu Uhujumu na Uzembe uliotuletea IPTL, ATCL, NMB, TRL, RICHMOND
  • Ukweli kuhusu mikataba yote ya Madini
  • Ripoti ya Warioba ya mambo ya Rushwa
  • Maelezo ya Rostam yaliyozuiwa na CCM kuhusu Richmond
  • Ukweli kuhusu Chenge na Vijisenti vyake kuhusiana na kashfa ya Radar
  • Ukweli na uwazi kuhusu mauaji ya Mwembechai, Zanzibar, Bulyanhulu na kwenye migodi mingine
  • Ukweli na Uwazi kuhusu Mapato na matumizi ya Serikali
  • Ukweli na Uwazi kuhusu mali za Viongozi wote wa Serikali tangu mwaka 1992
  • Ukweli na Uwazi kuhusu nia ya kuundwa kwa Katiba mpya
  • Ukweli na Uwazi kuhusu sera za Uwekezaji, misamaha ya kodi na ushuru kwa wawekezaji
Tusipoupata ukweli pamoja na uchungu wake, kamwe hatutaweza kupiga hatua kama Taifa. Pamoja na kujua Ukweli huu, tuwe tayari wote kama Taifa kwa matokeo ya juhudi hizi.

The Pandora box has to be opened. For our country to make steady progress in development and bring back accountability, the Pandora Box has to burst open.

Yes there will be blood, tears and teeth gnashing.

However without those things to happen, we will never have a chance to have a positive reflection to shape up our new direction towards maendeleo na uwajibikaji.

Na kiongozi jasiri na asiye na woga na aliyekuwa na mapenzi ya kweli kwa Tanzania atakayekuwa tayari kumfukuza kazi yeyote mara moja bila kuchelewa kwa manufaa ya Tanzania.

Hizi hadithi za Abunuwas hawa ni matajiri wakubwa wakikamatwa na kufilisiwa eti nchi italipuka au hawa ni matajiri wakubwa kuwafungulia kesi ni kitu kigumu mno tumechoka na hatutaki kuzikia tena.
 
Bubu,

Tusisubiri kiongozi mkuu atusaidie kwenye hili. Sisi kama wananchi inabidi tuwakalie kooni wabunge wetu na kuyadai haya. Tukikutana na viongozi wetu tuwahoji kuhusu haya. Tuchape madai haya magazetini, kwenye redio na kila kona kuishinikiza Serikali itoe ukweli.

Mambo ya kuundiwa tume na kamati yamepitwa na wakati na ni ufujaji wa pesa kama ile kamati ya Mwafaka.

Someone has to be bold and tell the story. Infact I would urge Rostam to come out of the closet and tell Watanzania what he wanted to tell Wabunge, because Bunge ni Wananchi!
 
Rev. Kishoka mkuu, mawazo mazuri sana hayo, tatizo hawa wabunge wetu, wengi wao kama siyo wote wameingia kwenye ubunge kwa nia ya kujichotea "vijisenti" sasa hata kuwabana kudai ukweli na uwazi wa yote uliyoyaainisha hapo juu, itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Wengi wapo humo kwa maslahi binafsi na siyo ya taifa.
Mimi nadhani ufumbuzi utapatikana na ukweli wote kujulikana yakifanyika mapinduzi na mafisadi wabanwe waseme ukweli wote halafu wahukumiwe kama ni kufungwa maisha wafungwe, kama ni kunyongwa mpaka kufa, wanyongwe; halafu tuanze upya, vinginevyo tutakuwa tunaendelea na unafiki kila kukicha.
 
Hili la kusubiri viongozi wafanye ndio limetufikisha hapa. Tumewasubiri wee hawafanyi, sasa kuna haja ya wananchi kuanza kuchukua hatua. Tukimhisi kiongozi fulani ni fisadi basi tunamwandama kwa maandishi, miluzi, kelele hadi atakapokosa raha kukaa kwenye kiti chake na hatimaye kukimbia.
 
Hili la kusubiri viongozi wafanye ndio limetufikisha hapa. Tumewasubiri wee hawafanyi, sasa kuna haja ya wananchi kuanza kuchukua hatua. Tukimhisi kiongozi fulani ni fisadi basi tunamwandama kwa maandishi, miluzi, kelele hadi atakapokosa raha kukaa kwenye kiti chake na hatimaye kukimbia.
Hatua iliyo bora ni kwa kutumia sanduku la kura,na hapa ndipo kuna tatizo kubwa,Je wananchi wako tayari??

Kazi bado ni ngumu mpaka pale watu watakapotambua ni kwanini wao ni masikini,hawajajua bado..

Mie napenda mabadiliko ,sababu mvinyo huu umeshanichosha ila baod naupenda,lakini sijapata Mvinyo wenye ladha ambayo itanifanya niuache huu niupendao.
 
Hatua iliyo bora ni kwa kutumia sanduku la kura,na hapa ndipo kuna tatizo kubwa,Je wananchi wako tayari??

Kazi bado ni ngumu mpaka pale watu watakapotambua ni kwanini wao ni masikini,hawajajua bado..

Mie napenda mabadiliko ,sababu mvinyo huu umeshanichosha ila baod naupenda,lakini sijapata Mvinyo wenye ladha ambayo itanifanya niuache huu niupendao.

Ukiwa fisadi au mtetezi wa ufisadi ni vigumu sana kuacha mvinyo ili mwenzako apate hata dawa ya kutibia malaria
 
Haya mambo ya kujiuzuru viongozi wa juu yanaumhimu mkubwa ktk kuielimisha jamii kuwa watu tulio nao ktk madaraka ni wa aina gani. Wananchi wataanza kukonect btn the dots manyanyaso wanayopata vijijini na umaskini uliokithiri na utajiri wa waliowapa kura. Hii sasa ni elimu ya bure kwa mamilioni ya Watanzania na inasambaa kwa kasi. Leo hii ukienda vijiji vya ndani ukauliza jamani mbona tuko maskini hivi? Wanasema si hao viongozi wanakula pesa zetu. Ndani ya miezi mitatu hii kunabadiliko kubwa sana kifikra miongoni mwa wananchi. Ukitaka uprove haya panda daradara usikie ubishi na fact zinazotolewa na wananchi wakawaida, pia tembelea sehemu za mikusanyiko vijijini kama kilioni. You will hear facts are coming from wananchi kuhusu ufisadi wa viongozi wetu. The only problem ni kwamba viongozi wetu wa vyama vya upinzani bado wana alama za utapeli vijijini. Nimefanya uchunguzi maeneo ya vijijini kwetu nimegundua viongozi wa upinzani ktk maeneo hayo ni wale waliokataliwa na jamii kwa misingi mbalimbali kama wizi, uhuni, ulevi, n.k Hii inaangusha sana inapofika wakati wa uchaguzi. Yafaa vyama vya upinzani viliangalie hili na kufuatilia ktk matawi ni watu wa namna gani wanaongoza ktk matawi hayo.
 
pandora box haiajfunguka vya kutosha, na ili pandora box ifunguke basi apatikane kiongozi ndani ya serikali mwenye nia wa kufanya kitu hicho.
mtoto wa mkulima alikuwa afanye kazi hii lakini wapi!! maskini kenda kuwakumbatia mafisadi
 
Back
Top Bottom