Uchaguzi 2020 Itilima! Itilima! this is too much! badilikeni haraka la sivyo muda utawabadilisha!!!

Mnyerede

JF-Expert Member
Dec 29, 2016
210
226
Wanabodi hakuna jambo lolote linalohusu masuala ya kifedha linalofanyika wilayani Itilima bila kuwa na harufu ya upigaji, tangu watu wamalize uandikishaji hawajapewa fedha yao, ukiwauliza wanakuambia wanasubiri mwongozo toka tamisemi. Aisee oneni aibu basi mbona wilaya nyingine wamepewa?

UPDATE :
mpaka Muda huu wilaya ya Itilima haijalipa waandikishaji wake wa wapiga kura tangu zoezi liishe tar. 17/10/2019 wakiulizwa wanasema mfumo wa malipo unasumbua, yaani kweli huo mfumo wa malipo unasumbua wilayani Itilima tu??? Mamlaka zinazohusika tunaomba wachukue hatua katika hili kabla watu hawajaandamana jumatatu tar 28/10/2019 kuelekea ofisi za halmashauri ya wilaya kudai chao, hii itakuwa ni aibu kubwa!!
 
Screenshot_20191021-164513.png
Angalia hao ni wabunge wa Mkoa wa Simiyu. Huyo Njalu Silanga ni Chadema sio eehh? Tatizo lako wewe Elitwege una matege ya ubongo. Au ndo kila baya linasababishwa na Chadema?
 
Ipo mkoa gani? Sijawahi kuisikia hiyo wilaya
Wala sio Wilaya. Ni jimbo la Uchaguzi ambalo liko Wilaya ya Bariadi. Limepakana na jimbo La Kisesa la Luhaga Mpina ambalo liko Wilaya ya Meatu. Hata hajui anachopost
 
Wala sio Wilaya. Ni jimbo la Uchaguzi ambalo liko Wilaya ya Bariadi. Limepakana na jimbo La Kisesa la Luhaga Mpina ambalo liko Wilaya ya Meatu. Hata hajui anachopost
Mkuu Itilima ni Wilaya kama zilivyo wilaya zingine kama Ilala au Monduli. Hata hivyo hapo kabla ilikuwa ni jimbo lililokuwa ndani ya wilaya ya Bariadi likiitwa Bariadi Mashariki. Baadaye ilibadilishwa kuwa Wilaya ya Itilima na jimbo lake la uchaguzi kuitwa Itilima. Zama zile likiwa ni himaya ya UDP chini ya mzee Momose.
 
Back
Top Bottom