Itikadi ya CCM ni ipi kwa sasa?

Mzalendo wa ukweli

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
559
149
Ukitazama kwa umakini alama zilizopo katika bendera ya CCM utagundua kuna alama ya jembe na nyundo; jembe likiwakilisha wananchi wakulima na nyundo ikiwakilisha wafanyakazi. Hii ilikuwa na maana kuwa CCM kilikuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi wakati kinaanzishwa. Kilijikita katikk kutetea haki za wafanyakazi na wakulima kwa ujumla. Na kwa kipindi hiki itikadi/ideology kuu ya chama ilikwa ni siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Swali langu kwa sasa ni kuwa kwa sasa itikadi ya chama hiki kwa uwazi kabisa ni ipi? Je ni chama cha wafanyakazi na wakulima bado au ni cha kibepari zaidi?
 
Kwa ufupi CCM ni chama dola, lakini katika utawala CCM ni chama cha upinzani kwani kinatawala kwa kutekeleza mipango ya Chadema. Hivyo kutokana na utawala wa aina hiyo CCM haiwezi kuwa na itikadi maalumu.
 
Kwa ufupi CCM ni chama dola, lakini katika utawala CCM ni chama cha upinzani kwani kinatawala kwa kutekeleza mipango ya Chadema. Hivyo kutokana na utawala wa aina hiyo CCM haiwezi kuwa na itikadi maalumu.

Okay,Thanks kwa idea yako mkuu
 
Itikadi ya CCM ni Ufisadi baada ya azimo la Zanzibari. Ingekuwa ni ubepari hali ya uchumi ingebadilika.
 
Mkuu unauliza itikadi ya CCM hata wana CCM wenyewe hawaijui; wako kwenye confusion!

Labda tusibiri wenyewe wamo humu jf kama kina Le Mutuz, Ritz, Chama na wengine nadhani wao watakujibu kwa ufasaha ingawa kinadharia.

Lakini tunavyojua watu wengi sasa hivi hata wao wana CCM ni kwamba CCM si chama tena cha wakulima na wafanyakazi. Wakulima na wafanyakazi walikwishatupwa zamani!

Sasa hivi ni chama cha mafisadi na wala rushwa na ndio itikadi yao. Kwa ajili hiyo hata wakikuambia maneno mengi utajua tu ukweli ni upi.
 
Mkuu unauliza itikadi ya CCM hata wana CCM wenyewe hawaijui; wako kwenye confusion!

Labda tusibiri wenyewe wamo humu jf kama kina Le Mutuz, Ritz, Chama na wengine nadhani wao watakujibu kwa ufasaha ingawa kinadharia.

Lakini tunavyojua watu wengi sasa hivi hata wao wana CCM ni kwamba CCM si chama tena cha wakulima na wafanyakazi. Wakulima na wafanyakazi walikwishatupwa zamani!

Sasa hivi ni chama cha mafisadi na wala rushwa na ndio itikadi yao. Kwa ajili hiyo hata wakikuambia maneno mengi utajua tu ukweli ni upi.

ujamaa na kujitegemea : ujamaa= chama cha udugu:-Vita Kawawa, Zainabu Kawawa,Zamaradi Kawawa, Dr.Husein Mwinyi, Balozi Karume, Amani Abeid Karume, ongezea orodha,
Kujitegemea: = Ufisadi,ni hulka ya ulafi, na ubinafisi = (wafanyabiashara wote walioingia CCM kwa ulafi wao wa kujitegemea)
 
Sera kubwa ya CCM kwa sasa ni kuendelea kutawala no matter what and by all means. Hawajali kuwakwamua Watanzania katika dimbwi la umasikini. Kumbuka umasikini wa Watanzania ndo mtaji mkubwa wa CCM. Watanzania kuendelea kuwa masikini ina maana CCM itaendelea kuwa madarakani. Hiyo ndo sera ya CCM.
 
Kwa taarifa alama ya Nyundo na Jembe kwenye bendera ya CCM imebadilika na kuwa "Kisu na Umma". Itikadi yake Kubwa ni wizi wa kura ili kupata dola na baada ya hapo kuchukua Chako Mapema.
 
kutarajia ccm online kujibu ni ndoto,hata katibu mwenezi wao Nape a.k.a. Mzee wa kujivua gamba hawezi jibu kama alivyoshindwa kuwavua magamba.
hao online ukiwasikia hapa jua wanamtukana Slaa mbaya wao.Mapaka ya kijani
 
Hata mwenyekiti wa CCM hajui itikadi ya chama chake vinginevyo tungemsikia akiinadi! Toka ameingia madarakani sijawahi kumsikia akisema "ujamaa na kujitegemea" ambayo ndiyo itikadi inayoelezwa kwenye katiba. Tatizo waliua Azimio la Arusha bila kuondoa baadhi ya maneno ya azimio hilo kwenye katiba sasa wamechanganyikiwa. Na sio mwenyekiti tu hata viongozi wote wa CCM hawana jibu la itikadi ya chama chao. Ukiwauliza sana sana watakwambia "ushindi daima" au "ari zaidi, Kasi zaidi nguvu zaidi" zaidi ya hapo hawana kitu!
 
ujamaa na kujitegemea : Ujamaa= chama cha udugu:-vita kawawa, zainabu kawawa,zamaradi kawawa, dr.husein mwinyi, balozi karume, amani abeid karume, ongezea orodha,
kujitegemea: = ufisadi,ni hulka ya ulafi, na ubinafisi = (wafanyabiashara wote walioingia ccm kwa ulafi wao wa kujitegemea)

mkuu umetishaaa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom