Itifaki ya Urais na piga Simu redioni.

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Kwanza natoa angalizo ya kwamba mada hii si ya kisiasa, Nimeiweka jukwaa la kisiasa Kwa Sababu Rais ni mwanasiasa hata Kama hataki siasa.
Rais wa nchi ni mtu mkubwa Sana kiitifaki, ni mfalme, hata Mungu akitaka Kulibariki taifa lolote lile huanzia kwanza Kwa kumtazama Rais, kiongozi, mfalme wa taifa hilo ana mahusiano gani na yeye?
Mungu akiona kuwa mfalme, Rais, kiongozi hana mahusiano mazuri na yeye hugeukia Kwa raia wa kawaida wanaomcha yeye na kuzitii amri zake na kisha anamua ama alibariki taifa hilo au aache ili kumfanya mfalme, kiongozi, Rais atambue kwamba Mungu anachukizwa na matendo yake ndo maana analiadhibu taifa husika.
Rais ndo mwamuzi wa mwisho ktk mustakabali wowote ule wa taifa.
Ndo maana anapewa ulinzi mkubwa na kuheshimika na watu wote na mataifa yote.
Rais wa nchi si mtu wa kuzoewa zoewa na watu.
Inapotokea Rais akawa anapiga simu redioni personally (Mara nyingi Viongozi wakubwa Kama Rais hutumia wasaidizi wao) ujue hapo kuna Tatizo kubwa sehemu.
Kiitifaki Rais hatakiwi kupiga simu redioni, tena radio yenyewe inaegemea upande mmoja wa siasa na rais ni kiongozi wa watu wote bila kujali itikadi zao za vyama.
Redio yenyewe ina historia mbaya kabisa ya kuchonganisha wananchi na wanamuziki, redio iliyojaa umbea mtupu na haina uwezo wa kusambaa nchi nzima, inasikika mijini tu.
Na Kwa Sababu Rais ni binadamu ndo maana huwa ana washauri wengi sana ambao wengine humshauri hadi aina ya mavazi.
Sasa sijui washauri wa Rais wetu ni wa aina gani kiasi kwamba hawawezi kumshauri kuwa hatakiwi kupiga simu redioni Kwa hadhi yake.
 
Umeanza vizuri sana mkuu! Ila umenza kuharibu hapo uliposema Redio yenye umbea mtupu,mara inafika mijini tuu ! Je kama mijini ndo uwezo wao tuu?

Nadhani ungesimama katika kiini cha mada kuhusu rahisi tuu...!
 
Back
Top Bottom