Itifaki inaruhusu mtu mwingine yoyote kuongea baada ya Rais kumaliza hotuba yake?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,550
46,090
Jana ulizuka mjadala kuhusu katazo la Spika kwa wabunge kutokuvaa tai nyekundu wakati Rais akiwa bungeni leo. Watetezi wa katazo hilo walisema ni suala la Itifaki.

Jambo jingine ambalo niliwahi kuambiwa ni Itifaki ni kwamba mtu mwingine hatakiwi kuongea na hadhira baada ya Rais kumaliza kuongea na hadhira hiyo na yeye akiwepo bado katika hadhira hiyo.

Muda wote niliamini inaweza kuwa kweli ni Itifaki mpaka leo nilipoona kuna mazungumzo mengine marefu kutoka kwa mbunge na Spika baada ya Rais kumaliza hotuba yake.

Je ni sahihi kiitifaki kwa jambo hilo lilofanyika leo bungeni?
 
Uko sahihi mkuu. Nataka nifahamu kama ni mara ya kwanza leo au imewahi kutokea hivyo
Yaani issue siyo hiyo... huko kote tumeelewa ila swali ni kwamba mbona kama ni mara ya kwanza hii kitu au labda iliwahi kutokea/kufanyika kabla kwa maraisi wengine tupeane uzoefu
 
Yaani issue siyo hiyo... huko kote tumeelewa ila swali ni kwamba mbona kama ni mara ya kwanza hii kitu au labda iliwahi kutokea/kufanyika kabla kwa maraisi wengine tupeane uzoefu
Mbona siku ile askof gwajima alishukuru kwa niaba ya wabunge baada ya mh magufuri kuhutubia bunge hukuwepo
 
Naomba nikusaidie mkuu,

Mle ndani mkuu kiitifaki ni spika wa bunge. Hivyo rais alikua kama mgeni na sehemu ya bunge ambapo Bunge lilikua kwenye session yake.


Nje ya bunge ndilo eneo hasa rais huwa top of all.
Baelezee Baelewe
 
Uko sahihi mkuu lakini mbona alikitaza wabunge kuvaa tai nyekundu na yeye mwenyewe hakuvaa tai nyekundu??
Naomba nikusaidie mkuu,

Mle ndani mkuu kiitifaki ni spika wa bunge. Hivyo rais alikua kama mgeni na sehemu ya bunge ambapo Bunge lilikua kwenye session yake.


Nje ya bunge ndilo eneo hasa rais huwa top of all.
 
Back
Top Bottom