Domo Kaya
JF-Expert Member
- May 29, 2007
- 531
- 59
Ndugu watanzania, mimi kama muathirika wa hii hali ngumu ya maisha bora kwa kila Mtanzania naona bora JESHI LA WANACHI TANZANIA wachukue nchi hata kwa Miaka mitatu (3) tu, na baada ya hapo nadhani tutatia adabu na sheria zote zitafuatwa.
Hapo itakuwa hakuna rais mstaafu wala rais mwenyewe amri ni moja tu, siku jeshi likiamua foleni imezidi watu watembee kwa miguu basi ni wote tunapiga kwato tu, wakisema kulala saa kumi na mbili hivyo hivyo.Kila kitu kijeshi jeshi tu.
Nadhani baada ya hapo nchi ikirudishwa kwa Marais adabu itakuwepo, maana kwa sasa nchi inaongozwa na wenye fedha tu, Kikwete yupo pale ikulu kama ushahidi tu kwamba Tanzania tuna Rais, lakini nini kifanyike wenye fedha ndio wanaamua. HIVI KWA MPANGO HUU TUTAFIKA KWELI? AU NDIO ULE USEMI TAJIRI ATAENDELEA KUWA TAJIRI NA MASIKINI ATAENDELEA KUWA MASIKINI MILELE.?
TUJADILI.
Hapo itakuwa hakuna rais mstaafu wala rais mwenyewe amri ni moja tu, siku jeshi likiamua foleni imezidi watu watembee kwa miguu basi ni wote tunapiga kwato tu, wakisema kulala saa kumi na mbili hivyo hivyo.Kila kitu kijeshi jeshi tu.
Nadhani baada ya hapo nchi ikirudishwa kwa Marais adabu itakuwepo, maana kwa sasa nchi inaongozwa na wenye fedha tu, Kikwete yupo pale ikulu kama ushahidi tu kwamba Tanzania tuna Rais, lakini nini kifanyike wenye fedha ndio wanaamua. HIVI KWA MPANGO HUU TUTAFIKA KWELI? AU NDIO ULE USEMI TAJIRI ATAENDELEA KUWA TAJIRI NA MASIKINI ATAENDELEA KUWA MASIKINI MILELE.?
TUJADILI.