Ndugu zangu wanaJF ninataka mnifahamishe. Hivi iwapo mgombea binafsi ataruhusiwa kugombea uenyekiti wa serikali ya mtaa, udiwani, ubunge na urais iteleta hasara au faida zipi? Je ni kweli kama serikali inavyojitetea kuwa wamekata rufaa kwa sababu katiba hairuhusu mgombea binafsi? Naomba wale mlio wasomi wa Political science and constituional law nielimisheni. Binafsi naiona kama iko harmless. Kwa sababu serikali kwa maana ya public service itaendelea kuwepo hata kama akishinda mgombea binafsi. Japo itabidi pia siyo lazima mawaziri watokane na wabunge. Hili ndiyo litaondoa medicority among ministers.