Naomba ushauri kuhusu gari aina ya Isuzu Big Horn

Wakuu nimebabatiza pesa sehemu nataka ninunue gari kubwa kiasi nayo ISUZU BIG HORN mwenye kuijua vizuri
1. Ulaji wa MAFUTA;
2. Spea zake;
3. Mafundi wetu wa Kibongo je wanaziwezea?
Mkuu hata siku moja usibugi ukanunua Bighorn ya diesel, utajuta.

Lkn sasa huu Uzi ni wa tarehe 12 Sept na Leo ni tarehe 6 Nov. Sijui ushaingia cha kike tayari.
 
Ni ushauri tu.

nunua hizi gari kama hela yako inaruhusu kununua.

CADILLAC ESCALADE - dollar $73. sawa na million 160 za kitanzania.

CHEVROLET TAHOE - dollar $47. sawa na million 102 za kitanzania.

BUICK ENVISION - dollar $34. sawa na million 74 za kitanzania.......

ni gari nzuri zenye ubora wa hali ya juu haili mafuta sana.
Ila Nyingi ni left hand. Yaani usukani upo kushoto.

Kama hela ina kuruhusu nunua mkuu. Utaifurahia.
 
Hongera,wenye Bighorn tunazidi kuongezeka,weka kapicha basi, halafu AC zake unaweza kuganda barafu, teh teh unajua watu wamezoea Toyota kumbe kuna gari zingine hatari!
 
ISUZU BIGHORN inanipa faraja, haina mawazo kabisa, haijanisumbua zaid ya service za kawaida kwa mafundi wetu chini ya mwembe pale Mwenge nyuma ya Tamal Hotel.
 
Back
Top Bottom