ISS - Satelaiti Angavu Leo = Extremely Bright Satellite visible today

njiwaji

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
279
202
Leo jioni kuanzia saa mbili kasoro ishirini, yaani saa moja na dakika arobaini (1:40 or 7:40pm) satelaiti angavu sana iitwayo International Space Station (ISS) intaonekana angani, ikitokea upeo wa kaskazini-magharibi.

Ramani hizi zinaonesha njia yake angani kwa miji mbali mbali na maeneo ya jirani yao.

Cha kushangaza ni kwamba mwanga mkali wake utakatika ghafla baada ya kutembea nusu to ya anga kwa dakika mbili hivi kwa sababu ya kuingia katika kivuli cha Dunia.

Kila ramani inaonesha njia, muelekeo pamoja na muda kamili wa kuchomoza na kupotea angani kwa kila mji na jirani zake

Kwa Dar es Salaam: inapanda juu kiasi kwa dakika mbili halafu inapotea ghafla.
IMG_6352.PNG



Kwa Morogoro: inapanda juu karibu na utosini halafu ina potea
IMG_6347.PNG



Kwa Mbeya: haipandi juu sana na itakuwa jirani na upeo wa kaskazini mashariki
IMG_6349.PNG


Kwa Mwanza: inapita anga lote kuanzia kaskazi magharibi hadi karibu na kusini.
IMG_6349.PNG


Kwa Arusha: Inapanda juu angani hadi utosini na inapita jirani sayari ya Mushtarii(Jupiter) kabla ya kupotea ghafla
IMG_6350.PNG



Kwa Mtwara: - haipandi juu sana
IMG_6351.PNG
 

Attachments

  • IMG_6347.PNG
    IMG_6347.PNG
    49.5 KB · Views: 33
Kuna ma maamuma na madarweshi wanaisubiri ili wakiiona wapate kuomba mahitaji yao.
Kuna mfanyakazi mwenzangu aliniomba atumikie zamu yangu majuzi ili leo nisimame katika zamu yake ili apate kuiona hii LAILAT LKADRI(Nyota ya jaa).
Kweli mzungu ni rafiki wa Mungu,anajua dunia na mifumo yake kiundani.
 
Kwanini njia/mistari mingine ni mirefu na mingine ni mifupi zaidi
 
Mbona inajulikana kila inavyo ongezewa nyama ndio inavyozidi kuwa kubwa 2025 itakuwa inaoneka hata mchana
 
Kweli mzungu ni rafiki wa Mungu,anajua dunia na mifumo yake kiundani.
Acha kukashifu imani za wenzio! Huwezi kuifananisha lailatulqadri na "modules with solar pannels" man made junk ambayo ni useless na ni waste of international money"uifananishe na lailatulqadri khairul min alfi shahr, na kwa taarifa yako mzungu huwezi mfananisha na mungu,mungu haibi makinikia.
 
Acha kukashifu imani za wenzio! Huwezi kuifananisha lailatulqadri na "modules with solar pannels" man made junk ambayo ni useless na ni waste of international money"uifananishe na lailatulqadri khairul min alfi shahr, na kwa taarifa yako mzungu huwezi mfananisha na mungu,mungu haibi makinikia.
punguza jazba!
 
international-space-station-iss-with-shuttle-endeavour-2011-05-23.jpg
You can't compare this junk of rusting metal with "laylatu qadri"khairul min alfi shashr
 
Kwanini njia/mistari mingine ni mirefu na mingine ni mifupi zaidi
Mistari lilionesha njia ambamo satelaiti ya ISS itapita.

Kwa hiyo kama mstari ni mfupi satelaiti inapotea mapema baada ya kutembea kuwa muda mfupi,

na ikiwa ndefu inaendelea kuonekana angani kwa muda mrefu.
 
Mistari lilionesha njia ambamo satelaiti ya ISS itapita.

Kwa hiyo kama mstari ni mfupi satelaiti inapotea mapema baada ya kutembea kuwa muda mfupi,

na ikiwa ndefu inaendelea kuonekana angani kwa muda mrefu.


Kwanini inatofautiana kati ya mkoa na mkoa/mji
 
Kwanini inatofautiana kati ya mkoa na mkoa/mji
Swali zuri. Tunaiona ISS kutoka sehemu mbali mbali. Na kwa vile chomboanga hiki kinapita katika mzingo wake maalum. Kwa vile kila sehemu inaiona ISS kwa umbali tofauti tofauti kutokana walipo, kiasi watakachoona hicho chombo pia kitatofautiana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom