Israel yalazimika kukiri nguvu kubwa za kijeshi za Iran

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,839
17,437
Israel yalazimika kukiri nguvu kubwa za kijeshi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Sep 13, 2021 02:27 UTC

[https://media]

Waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa droni yaani ndege zisizo na rubani za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zina uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kwa mujibu wa mujibu wa tovuti ya habari ya "Arab24," waziri wa vita wa Israel, Benny Gantz alikiri jana (Jumapili) kwamba moja ya zana muhimu za kijeshi za Iran ni ndege zake zisizo na rubani ambazo ni kama makombora ya balestiki na ndege za kivita, zinaweza kuruka umbali wa maelfu ya kilomita na kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kabla ya hapo pia, Uzi Rubin aliyepewa lakabu ya baba wa makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel alikuwa naye amekiri nguvu na uwezo mkubwa wa kijeshi wa Iran akisisitiza kuwa, maenendeleo ya haraka iliyopita Iran katika miradi yake ya anga za mbali isiyo ya kijeshi na ya kijeshi, ni jambo linalotia wasiwasi mkubwa.

[https://media]Benny Gantz, waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel



Kamanda mwingine wa ngazi za juu wa jeshi la utawala wa Kizayuni naye pia amekiri kwamba, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina uwezo wa kufanya mashambulizi makali na hatari kwa Israel na kuisababishia Tel Avavi hasara kubwa.

Meja Jenerali Aharon Haliva ameendelea kusema, ishara zote zinaonesha kuwa, kutaka na kukataa, mwaka 2020 si mwaka wa mafanikio ya kiusalama kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.

4bmz2f42298b74t5gs_800C450.jpg
 
Israel yalazimika kukiri nguvu kubwa za kijeshi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Sep 13, 2021 02:27 UTC

[https://media]

Waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa droni yaani ndege zisizo na rubani za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zina uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kwa mujibu wa mujibu wa tovuti ya habari ya "Arab24," waziri wa vita wa Israel, Benny Gantz alikiri jana (Jumapili) kwamba moja ya zana muhimu za kijeshi za Iran ni ndege zake zisizo na rubani ambazo ni kama makombora ya balestiki na ndege za kivita, zinaweza kuruka umbali wa maelfu ya kilomita na kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kabla ya hapo pia, Uzi Rubin aliyepewa lakabu ya baba wa makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel alikuwa naye amekiri nguvu na uwezo mkubwa wa kijeshi wa Iran akisisitiza kuwa, maenendeleo ya haraka iliyopita Iran katika miradi yake ya anga za mbali isiyo ya kijeshi na ya kijeshi, ni jambo linalotia wasiwasi mkubwa.

[https://media]Benny Gantz, waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel



Kamanda mwingine wa ngazi za juu wa jeshi la utawala wa Kizayuni naye pia amekiri kwamba, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina uwezo wa kufanya mashambulizi makali na hatari kwa Israel na kuisababishia Tel Avavi hasara kubwa.

Meja Jenerali Aharon Haliva ameendelea kusema, ishara zote zinaonesha kuwa, kutaka na kukataa, mwaka 2020 si mwaka wa mafanikio ya kiusalama kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.

View attachment 1937873


Sio jambo la kawaida hata kidogo kwa Waisraeli kutamka hadharani "Mambo Mazuri" ya adui yake, hiyo inaitwa "Pyschological warfare".---- Iran anatakiwa ajiangalie na aendelee na mikakati yake ya kijeshi kujilinda.na hao Waisrael akifanya kosa la kubweteka baada ya kusifiwa kinafiki basi sio muda mrefu atakwishilia mbali kwani Waisreal ni watu wajanja, Wenye hila na AKILI NYINGI katika mambo yao.

Iran awe muangalifu sana na hizo sifa za kimkakati za Israeli.

"Jews cunning".
 
Sio jambo la kawaida hata kidogo kwa Waisraeli kutamka hadharani "Mambo Mazuri" ya adui yake, hiyo inaitwa "Pyschological warfare".---- Iran anatakiwa ajiangalie na aendelee na mikakati yake ya kijeshi kujilinda.na hao Waisrael akifanya kosa la kubweteka baada ya kusifiwa kinafiki basi sio muda mrefu atakwishilia mbali kwani Waisreal ni watu wajanja, Wenye hila na AKILI NYINGI katika mambo yao.

Iran awe muangalifu sana na hizo sifa za kimkakati za Israeli.

"Jews cunning".
Muirani toka mchambawima umesikika na Wairan waliopo ng'ambo.
 
Muirani toka mchambawima umesikika na Wairan waliopo ng'ambo.


Nawe Muisiraeli kutoka Mchambanyuma kawaambie hao nduguzo Waiziraeli waliomtungika Yesu msalabani kwamba sifa zao kwa Irani ni za kinafiki na waende kuwasifia Russia.

Iran arms technology hails from Russia scientists who are paid handsomely by Iran goverment for the purpose.
 
Nawe Muisiraeli kutoka Mchambanyuma kawaambie hao nduguzo Waiziraeli waliomtungika Yesu msalabani kwamba sifa zao kwa Irani ni za kinafiki na waende kuwasifia Russia.

Iran arms technology hails from Russia scientists who are paid handsomely by Iran goverment for the purpose.
"Waliomtungika"

Kweli zaidi ya miaka 60 ya uhuru TZ tumefika hapa tokana na hivi vituko
 
Alafu ma ayatola yataamka yanashangilia Kama Mazuzu kwamba Iran ina uwezo yaan ukiona Adui amekushangilia jua kuna sehemu ume bugi
wameeleza ukweli, kama wangekuwa dhaifu wangekuwa wameshavamiwa tayari kama majirani zao. Sio Israel tu bali hata Marekani hawezi ishambulia Iran sababu hakuna nchi itakubali kutumika kama uwanja wa vita kati ya Marekani na Iran. Ingawa Marekani atawashinda Iran kama ikitokea ila kwa gharama ipi? Iran wameendelea kisayansi kuliko nchi zote ambazo Marekani na Israel imewahi kuvamia plus wana serikali ambayo ina nguvu ya umma.
 
Hawajashangilia wameeleza ukweli, kama wangekuwa dhaifu wangekuwa wameshavamiwa tayari kama majirani zao. Sio Israel tu bali hata Marekani hawezi ishambulia Iran sababu hakuna nchi itakubali kutumika kama uwanja wa vita kati ya Marekani na Iran. Ingawa Marekani atawashinda Iran kama ikitokea ila kwa gharama ipi? Iran wameendelea kisayansi kuliko nchi zote ambazo Marekani na Israel imewahi kuvamia plus wana serikali ambayo ina nguvu ya umma.
We , Iran ina Sayansi gani ya kumshinda Mmarekani na Muisrael . Unajua kuna kitu kinaitwa Artificial Intelligence
 
We , Iran ina Sayansi gani ya kumshinda Mmarekani na Muisrael . Unajua kuna kitu kinaitwa Artificial Intelligence
Ndomaana nikasema Marekani itashinda kwa sababu wameendelea kiteknolojia na kiuchumi ila watashinda baada ya muda gani na kwa gharama ipi? Iran sio Afaghanstan, Iraq au Libya hawa wana silaha zao ambazo wao wenyewe wamarekani wanaziogopa na kuhusu teknolojia sio wanyonge sababu ni mwaka huu tu wameishusha drone ya kisasa ya Marekani bila kuilipua. Mfano Mwingine North Korea ana nuclear weapons na ni nchi masikini lakini hadi leo hajavamiwa ( North Korea hamfikii Iran kwa chochote)
 
Ndomaana nikasema Marekani itashinda kwa sababu wameendelea kisayansi na kiuchumi ila watashinda baada ya muda gani na kwa gharama ipi? Iran sio Afaghanstan, Iraq au Libya hawa wana silaha zao ambazo wao wenyewe wamarekani wanaziogopa na kuhusu teknolojia sio wanyonge sababu ni mwaka huu tu wameishusha drone ya kisasa ya Marekani bila kuilipua sasa hadi hapo jiulize wewe Marekani anaweza kwenda kuivamia kirahisi kama alivyofanya Libya na Iraq? Mfano Mwingine North Korea ana nuclear weapons na ni nchi masikini lakini hadi leo hajavamiwa ( North Korea hamfikii Iran kwa chochote)
Kiufupi Mwarabu kumtishia Marekani ni uongo , China na Urusi hili wanalijua.
 
Ndomaana nikasema Marekani itashinda kwa sababu wameendelea kisayansi na kiuchumi ila watashinda baada ya muda gani na kwa gharama ipi? Iran sio Afaghanstan, Iraq au Libya hawa wana silaha zao ambazo wao wenyewe wamarekani wanaziogopa na kuhusu teknolojia sio wanyonge sababu ni mwaka huu tu wameishusha drone ya kisasa ya Marekani bila kuilipua sasa hadi hapo jiulize wewe Marekani anaweza kwenda kuivamia kirahisi kama alivyofanya Libya na Iraq? Mfano Mwingine North Korea ana nuclear weapons na ni nchi masikini lakini hadi leo hajavamiwa ( North Korea hamfikii Iran kwa chochote)
Uliza Kampuni ya Huawei imefikia wapi asa hivi , Kama China ipo vizuri kwenye teknolojia
 
Israel yalazimika kukiri nguvu kubwa za kijeshi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Sep 13, 2021 02:27 UTC

[https://media]

Waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa droni yaani ndege zisizo na rubani za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zina uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kwa mujibu wa mujibu wa tovuti ya habari ya "Arab24," waziri wa vita wa Israel, Benny Gantz alikiri jana (Jumapili) kwamba moja ya zana muhimu za kijeshi za Iran ni ndege zake zisizo na rubani ambazo ni kama makombora ya balestiki na ndege za kivita, zinaweza kuruka umbali wa maelfu ya kilomita na kufanya mashambulizi makini na angamizi.

Kabla ya hapo pia, Uzi Rubin aliyepewa lakabu ya baba wa makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel alikuwa naye amekiri nguvu na uwezo mkubwa wa kijeshi wa Iran akisisitiza kuwa, maenendeleo ya haraka iliyopita Iran katika miradi yake ya anga za mbali isiyo ya kijeshi na ya kijeshi, ni jambo linalotia wasiwasi mkubwa.

[https://media]Benny Gantz, waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel



Kamanda mwingine wa ngazi za juu wa jeshi la utawala wa Kizayuni naye pia amekiri kwamba, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina uwezo wa kufanya mashambulizi makali na hatari kwa Israel na kuisababishia Tel Avavi hasara kubwa.

Meja Jenerali Aharon Haliva ameendelea kusema, ishara zote zinaonesha kuwa, kutaka na kukataa, mwaka 2020 si mwaka wa mafanikio ya kiusalama kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.

View attachment 1937873
Uliwahi kumsikia Moshe Dayan akizungumzia uweza wa jehi la Misri kabla hajaliangamiza? Msikilize hapa
kuanzia dakika ya 50 ujue kuwa wao kusifia uwezo wa wapinzni wao huwa haina maana ya kuwaogopa.

 
Fatilia zaidi masuala ya kimataifa na ujibu nilichoandika.
Mwarabu ajavumbua chochote, silaha zote anazotumia uvumbuzi wake umefanyikia nchi za magharibi kisha wanatengeneza kupitia formular za nchi ya magharibi. Hii ni tofauti na vitu vya kiteknolojia vinavyotoka Israel - formular huwa tofauti na huwezi aribu mifumo haya. Iran ina Drone zilizotengenezwa kwa formular ya Mmarekani - ni rahisi sana kuzi shut-down bila ya kufanya tukio kwa sababu wamarekani wanajua mapungufu yapo wapi.

Iran ana nguvu ya kiuchumi , lakini akili hana. Israel na Mmarekani wana-uchumi na pia wanatumia akili
 
Mwarabu ajavumbua chochote, silaha zote anazotumia uvumbuzi wake umefanyikia nchi za magharibi kisha wanatengeneza kupitia formular za nchi ya magharibi. Hii ni tofauti na vitu vya kiteknolojia vinavyotoka Israel - formular huwa tofauti na huwezi aribu mifumo haya. Iran ina Drone zilizotengenezwa kwa formular ya Mmarekani - ni rahisi sana kuzi shut-down bila ya kufanya tukio kwa sababu wamarekani wanajua mapungufu yapo wapi.

Iran ana nguvu ya kiuchumi , lakini akili hana. Israel na Mmarekani wana-uchumi na pia wanatumia akili
ingekuwa Iran ni mwepesi kama unavyofikilia weweee..
ingekuwa kitambo imeshavurugwaa, unataka Iran wafanye nini ndo ukubali uwezo wao??
wameziteka na kuzitungua drones kibao za US na mwishowe anaishia vitisho tuu bila kushambuliaa
kazitwanga kambi za US na mwishowe anaishia vitisho tuu
kateka meli ya uingereza na mwisho wameishia kuomba poo
kama alivyosema jamaa hapo juu
US atashinda ilaa cha Moto atakionaaa
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom