Israel kuipatia Tanzania techolojia ya Drones kwa ajili ya kupambana na Ujangili

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
Serikali ya Tanzania imesema kwa sasa iko kwenye mazungumzo na serikali ya Israel kuona ni namna gani Israel itaipatia Tanzania teknolojia mpya ya ndege zisizo na rubani "drones" ili kupambana na ujangili katika hifadhi za taifa za wanyama.

Waziri wa Maliasili na Utalii Professor Jumanne Maghembe amesema mazungumzo yanakwenda vizuri na kwa sasa wanaangalia ni namna gani teknolojia hio itaweza kutumika katika mazingira ya kwetu.

Teknolojia hio itaweza kuwagundua majangili mara tu wanapoingia hifadhini kabla hata hawajaanza kuwaua wanyama hususani tembo kwa kutumia ndege ndogo ambazo hazina rubani.

Haya yamekuja baada ya Israel kukubali kufungua Ubalozi wake Dar es Salaam na hapo jana kuzindua kituo cha kushughulikia VISA ya kwenda Israel jijini Dar es Salaam.

Source: The Guardian.
 
Walianza wamarekani hatuoni impact badala yake Geospatial det imefanywa me siikubali
 
Wafanye Research kwanza kabla ya kukurupuka, tutaliwa tena. Kumbuka NCHI Hii ni shamba la marehemu babu
 
Naomba pia operator pia wawe hao hao waislaeli maana akipewa Muha lazima azichokonoe Kama walivyofanya scanners za uwanja wa ndege wa Mwl JK.
 
Kwa utawala huu wa Rais Magufuli naamini kila kitu kitawezekana
 
Drones..? huu utani sasa..! Tatizo la Ujangili sio hakuna ULINZI MZURI.. TATIZO MAJANGILI WAKUU KABISA WAKO KTK SYSTEM.. na katikati ya Chama chetu CCM..!!
 
Kwa hali iyo bado tunapita vichakan badala yakupita njia kuu maana matatizo ya ujangil yanajulikana ila hayawekwi wazz.
 
Back
Top Bottom