Israel imezungukwa pande zote na waarabu lakini hawawezi kufanywa lolote? Kwa nini?

Cosovo

JF-Expert Member
Jul 8, 2018
667
1,795
Mimi huwa ni mhanga wa swali hili,Wayahudi wamezungukwa pande zote na jamii ya kiarabu,lakini huwa nashangaa namna wanavyo wananyanyasa warabu wenzao (Wapalestina)lakini nchi za kiarabu kimya

Hivi warabu wanawawaogopa waisrael kias gani?

Miaka na miaka wapalestina wananyanyaswa na Israel lakini waarabu hawachukui hatua

Nikasoma sehemu huenda vita Juni 1968 ndo iliwafanya kuogopa mpaka leo

Je ni kweli? Ni kweli nchi za kiarabu zaidi ya 20 wameshindwa kupambana na Israel?
 
Unanunua kiwanja halafu unamaliza kujenga unaanza kukutana na vimbwanga vya najirani kuhama huwezi unaishi maisha ya taabu milele hata kuku akienda kwa jirani ni kesi
 
Unanunua kiwanja halafu unamaliza kujenga unaanza kukutana na vimbwanga vya najirani kuhama huwezi unaishi maisha ya taabu milele hata kuku akienda kwa jirani ni kesi
Israel imekuwa jeuri hatari
 
We hujui Israel viongozi wa kiarabu ni vibaraka wa US wao ndio wanailinda Israel.

Siku viongozi wa kiarabu akitokea kama Sadam watamvamia kama alivyo vamiwa Iraq.

Mipaka ya Israel inalindwa na vibaraka wa US viongozi wa kiarabu.
 
We hujui Israel viongozi wa kiarabu ni vibaraka wa US wao ndio wanailinda Israel.

Siku viongozi wa kiarabu akitokea kama Sadam watamvamia kama alivyo vamiwa Iraq.

Mipaka ya Israel inalindwa na vibaraka wa US viongozi wa kiarabu.
Sema walishajaribu na walishindwa vibaya, wengine kutokana na walichokutana nacho, walisaini mikataba ya kutopigana tena na Israel.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Huwezi kupigana na Israeli na ukaishinda!
Israel inalindwa na Mungu mwenyewe wala sio mwanadamu!
 
Walishajaribu wakashindwa. Walishapata hasara vya kutosha kwa kujaribu kupambana na Israel, huko nyuma, huenda ndio sababu wanasita kuingia kichwa kichwa kwenye vita ambavyo wanajua hawawezi kushinda.
Wamwulize Syria, mpaka sasa milima ya Golan ilibebwa tangu walivyojaribu kukabiliana na Israel. Misri nusura mlima Sinai uchukuliwe pamoja na mfereji wa Suez. Kuepuka hilo ilibidi misri iingie makubaliano na israel kule camp David ili mambo yatulie. Ndugu zao Jordan ndo hata hawasikiki tena!
 
Watu mnashindwa kuelewa kua Israeli ni Taifa la Mungu..
Mwanzo wote wa sayansi na teknologia ya Dunia chanzo ni Israeli
Marekani mwenyewe ubora wake na sifa zake zinatokana na watu wa Israeli ama wazaliwa ama mchanganyiko. Sasa atasema nini juu ya Israeli hakohoi wala nini?

Kila kitu kikubwa juu ya uso wa Dunia chimbuko na mwanzilishi mara nyingi Ana historia ya Israeli ama kwa kuzaliwa huko ama kwa kuzaliwa na wazazi mchanganyiko mmoja wapo toka Israeli.

Ndugu zangu tusome vitabu tupate maarifa. Tunaposema Israeli ni Taifa la Mungu na ndilo linaendesha Dunia muelewe.

Marekani ni robot tu ila remote iko Israeli
 
Warabu walipewa kichapo na kwa dharau maeneo ya nchi yao yakatekwa wajeshi kibao wakafa walipata aibu ya maisha yao awawezi kurudia ujinga tena kwasababu wanajua kitachowapata ndio maana wamenyamaza kama awaoni
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom