Fredwash
JF-Expert Member
- Oct 27, 2009
- 1,041
- 1,375
Hahaha!! Hivi unaikumbuka Ile vita ya mataifa 11 ya kiarabu kushambulia Israel mkuu,
Ndege Mia moja ziliyeyushwa ndani ya dk 3 tu na misiri akaapa kutofanya vita na Israeli maisha yake yote, unakumbuka?
Kama ndo hivyo, hamasi ndo Nani??
yaan ile vita inanishangaza.... yaan Israel alipowashinda waarabu akaingia misri akateka
mji wa Sinai.. akaukalia kwa mabavu.. akarudisha mpaka wao sinai ikawa eneo la israel.. akajenga makazi akajenga base za kijeshi akachukua control ya visima vya mafuta
Israel kapigana vita na waraaabu zaid ya mara tano
1948 - 49, 1967, 1973, 1982, and 2006.
1948–49: Israel’s War of Independence and the Palestinian Nakbah. First israel and arab war- ndo rasmi israel ikatangazwa kuwa taifa
1956 Suez War - second war hapa Misri alichangiwa na Israel na Uk kimtindo maana rais mpya wa misri ndugu Gamal Nasser baada ya tofauti za kisiasa kati yake na wazungu akanationalise mfereji wa suez na kupiga marufuku meli kupita bila Misri kuruhusu..
Wazungu kuona hivyo wakaona isiwe shida wakamchochea Israel ambaye nae Misri alipiga ban meli zake na kublock port elizabeth akianzishe kwa Misri halafu wao wataingia kama walinda aman
kwa maana hiyo mfereji wa Suez utakuwa hauna mwenyewe uko chini ya mamlaka ya kimataifa then bussness as usual meli zitaendelea kupita .
israel akakianzisha ndani ya siku tano wakateka miji kama gaza, rafah, na pennisula ya sauez canal, na miji mingine na baada ya mda mfupi wazungu wakaingia eti kama wasuluhishi kumuomba israel aondoe majeshi israel baada ya mwaka akaondoa majeshi 1957 mfereji wa suez ukawa no-man's land kwa muda na wazungu na israel wakaendelea kuutumia kwan ulikuwa chini ya UN
1967- Six days War.. hapa napo syria ambapo wakat huo alikuwa super power upande wa waarabu na ndo original ya palestina ilipo waliashuha mvua ya mabomu vijiji israel kwenye milima inajulikana kama Golan Heights...katika kujaribu kuwafuta Israel.
israel akajibu kwa kutungua ndege za Syria .. kuona hivyo Misri chini ya Nasser mwenye machungu ya kuporwa Suez canal akapata upenyo akawapiga mkwara UN pale suez canal akaingiza majeshi wakakubaliana na Jordan waunganishe nguvu waingie israel.
kwa hiyo Israel akawa anapigwa pande zote huku jordan huku misri kule Syria... ardhini na Angani
Misri na Jordan wakaoanga shambulio
la anganla kumaliza vita. kabla ndege hazijaruka Israel akapiga mabomu kwenye airforce zao hasa za Misri kabla hata ndege kuruka ..shughuli ya anga ikaisha.. wakarudi ardhin. israel akawapush zote upande wa syria akawapiga hadi kwao..
upande wa misri akawapiga akaingia had Gaza, Sinai akachukua na suez canal.. kule
jordan akaingia akachukua had jerusalem yote
ndan ya siku sita shughuli imeisha na israel katanua mipaka zaid. Misri kanyangwanya mji, jordan kanyangwanya mji.
utaona Wataab wanachangia Israel kujitanua. wakianzisha vita jamaa anajitanua.
1973: Yom Kippur War
hii vita ya mda mfupi, Misri na syria waliwakuta Israel offgurs Israel kwenye Sikuku yao ambayo inaitwa Yom Kippur.. israel wakapigika..
kuona hivyo Israel waka focus kuwapiga Syria.. kupitia Syria wakawazunguka wa Misri kuwagawa then nao wakafanya ambush shughuli ikaisha ingawa Misri alifanikiwa kukomboa sehem ya ardhi iliokuwa chini ya Israel
na vita hii ilipigwa kwenye mfungo wa wote ramadhan.. baada ya vita mwaka uliofuatia 1974 pande zote Tatu ( Misri, Syria na Israel) wakawekeana mkataba wa Amani wa kuacha vita...UN wakarud tena pae Sinai na suez canal kupafanya No- Man's Land ingawa sehem kubwa ya sinai Israel alikuwa anaikalia.. akajenga na makazi na base za jeshi akachimba na mafuta.
Kumbuka Misri na mataifa mengi ya waarabu walikuwa hawaitambui Israel kama taifa. mwaka 1977 Misri akaona isiwe shida rais wake wakati huo Saadat akatembelea Israel na kulihutubia Bunge la Israel
1979 Misri wakaomba eneo lake la Sinai kwa njia ya kidiplomasia kupitia UN. Israel akatoa sharti kuwa atarudisha mji wa Sinai na suez canal na kuondoa makaz yake ikiwa Misri ataitambua Israel kama taifa na Israel afungue ubaloz Misri. na marufuku Misri kuivamia israel au kuingilia ugomvi wowote ule wa Misri na mataifa mengine ya kiarabu Misri akakubali
1982 - Lebanon War
Israel walichukua miaka minne kutoka Sinai na rasmi mwaka 1982 Sinai ikarudi Misri.
wiki sita baadae Israel akakianzisha upande wa lebanon.. baada ya tension kati ya israel na palestina kuwa kubwa. Israel akapiga mabomu Beirut Lebanon kulipokuwa na strong hold za Palestina liberation Organization PLO.
Israel akavamia Lebanon na ndani ya wiki moja akauzunguka mji wa Beirut wote. ila baada ya maombi ya umoja wa mataifa na Israel kuipiga mabomu usiku na mchana lebanon akakubali kuacha kuikalia kimabavu lebanon ikiwa tu PLO na waondoke Lebanon.. israel hakutaka palestina organization yotote iwe lebanon.
PLO wakagoma walijua wakitoka shuguli wanayo so baada ya majadiliano ikabidi majeshi ya Umoja wa mataifa yaende lebanon kuwa escort wanajeshi na viongoz wa PLO kutoka lebanon.. na baada ya hapo Israel aliendelea kuikalia lebanon had alipojiridhisha PLO hawa operate lebanon tena akaiachia mwaka 1985
2006 - Second Lebanon war
Hizbola walikuwa wanaoparate lebanon ... na wakawateka wa israel ili kushinikiza israel wawaachie wafungwa wa kilebanon .. badala yake israel akaivamia lebanon akaipiga kwa mda wa siku 34.. akauwa maelfu ya walebanon na kuwakosesha makaz mamilion ya watu.. yaani kama anachofanya sasa Gaza
baadhi ya mataifa ya kiarabu walikishutumu kikundi cha Hizbola kwa kuanzisha vita .. ila kuna mengine walipongeza wa kuonyesha ujasiri wa kupambama na Israel
so utaona waarabu na waisrael hawajaanza kupigana leo. Israel Vita iko kwenye dam yao.. na hawa waarabu pia. ila jordan na Misri walishajiweka pembeni na myahudi