Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 13,992
- 20,283
1. Wapo tayari kuungana katika kutetea kazi za usanii wanaoufanya ndani ya majengo ya makanisa. Lakini hakuna hata mmoja kati yao anayeweza kutawalika kwa mwingine! Kila mmoja anataka amtawale mwenzake.
2. Huwa wanafanya kazi zao kwa muundoo wa ku-copy & paste. Mfano wakiona kuna Nabii mwenzao ametoa Mapepo kwa kupuliza Upepo Mic na wengine watafanya hayo hayo!
3. Hawafanyi kazi ya Unabii bila Pesa Mkononi. Mhitaji akienda Awe na Pesa ya kumuona Nabii, Awe na Pesa ya kwenda Kusafishiwa Nyota, Pesa ya kutabiria! Unabii wao ni kwa ajili Maisha ya watu tu. Hawana Unabii kwa Taifa wala Ulimwengu kwa ujumla.
4. Ni waoga wa kufa kuliko raia (watu) wanaowahudumia. Imefikia wakati hata Ulinzi wa Nguvu za Mungu hawauamini! Wamekuwa na Walinzi wa Kimwili zaidi. Huwa wana VITISHO sana kwa watu wanaowakosoa kiutendani! Wapo tayari Kushambulia kwa maneno au kushambulia kwa Vitendo, Kupiga mtu, Kutishia watu maisha na hata kutoa kauli za kumuua mtu!
5. Wananena kwa Lugha kwa staili ya maneno yale yale ya KUKARIRI yasiyozidi Kumi (10), yaani Lugha yetu wanayonena haipanuki kimaneno, maneno ni yale yale yaliyopo Dsm, Mwanza, Dodona na Morogoro, hayazidi zaid ya hapo! Na hawajui maana ya yale maneno wanayotamka!
6. Wanaongoza KUSENGENYANA wao kwa wao, lakini wakikutana pamoja ni kama wana Umoja wa Kazi ya Mungu na kumbe ndani yao ipo shida kubwa! Wanapenda Sifa sana, Kusifiwa, Kunyenyekewa na Kuabudiwa kuliko hata Mungu mwenyeqe. Hupenda kila wanalolifanya waonekane na watu! Hata akimsaidia mtu msaada wa nauli ya daladala ya Tshs 1,000/= wanataka Wamchukue picha (Selfee). Wakienda huko Maporini (Mlimani) kwa ajili ya kile wanachokiita Maombi ya Mlimani ndiyo usiseme! Hakuna maombi huko ni Vurudu za picha na Clip za shot Video. Hakuna Mungu huko zaidi ya maingizo ya maombi!
7. Wanapenda kunyang'anyana Waumini ndani ya majengo ya Ibada na hasa pale wanapoalikana Kihuduma. Wanapotoka hapo walipoalikwa kuhudumu huchukua namba za simu za Waumini wa eneo husika ili kuwahamisha na hasa wale wenye kuonekana wana Kipato kifedha! Hupenda sifa zaidi hata Waandishi na Mafarisayo kuwawafikii Mitume na Manabii wa zama hizi kwa sifa. Hupenda mashindano ya kuvaa Masuti ya gharama, Hushindana kula vyakula ya bei mbaya na bila kujua hapo mtaani kwake anapohudumu kuna watu ni Maskini wa kutubwa na wanalala na njaa. Hupenda zaidi kujionyesha kwa watu na hasa pale wanaponunua Magari ya kutembelea.
8. Wengi wao wana vinywa Vilivyojaa matusi na maneno Makali ambayo huwezi kumdhania. Wapo tayari kurusha picha za NGONO au mtu anayekata mauno! Halafu utamsikia mrushaji akisema "JAMANI ANGALIENI HAPA NDIPO DUNIA ILIPOFIKIA" na kumbe yeye ndiye anayependa mambo hayo na yamejaa kwa simu yake! Ukiwa nao na kuwaangalia ni Dakika 10 wanaweza kujifanya wapo Kiroho, lakini dakika chache wanakuwa watu wa Kimwili. Na wapo tayari kwenda kwa WAGANGA WA KIENYEJI ili kukuza Kundi la Watu.
9. Mahubiri yao Mitume na Manabii yameegemea zaidi kwenye AGANO LA KALE na hasa Vitabu vya MALAKI (Fungu la Kumi), ZABURI (Misingi ikiharibika), Urejesho wa nyota, Mafanikio wakimnukuu Ibrahimu Baba wa Imani. Bila kujua kwamba Ibrahimu yeye alishakuwa na mali nyingi kwa sababu ya Juhudi zake. Bali Mungu alichokifanya pale ni kumuongezea tu. Zaidi ya hapo hakuna mahubiri zaidi! Labda hapo yatafuata mahubiri ya Kichwani ya Kufoka (Kukoroma) pasipo na maandiko!
10. Wengi wao hawajui nini maana ya Utume Ki-Biblia wala hawajui maana ya Unabii Ki-Biblia. Hata ukimuuliza juu ya Yesu anaweza hata kukujibu kwamba Yesu siyo Mungu! Ndiyo maana kwa hapa Tanzania Mitume wengi na Manabii ndiyo wamekuwa ni Wachungaji wa Kanisa.
2. Huwa wanafanya kazi zao kwa muundoo wa ku-copy & paste. Mfano wakiona kuna Nabii mwenzao ametoa Mapepo kwa kupuliza Upepo Mic na wengine watafanya hayo hayo!
3. Hawafanyi kazi ya Unabii bila Pesa Mkononi. Mhitaji akienda Awe na Pesa ya kumuona Nabii, Awe na Pesa ya kwenda Kusafishiwa Nyota, Pesa ya kutabiria! Unabii wao ni kwa ajili Maisha ya watu tu. Hawana Unabii kwa Taifa wala Ulimwengu kwa ujumla.
4. Ni waoga wa kufa kuliko raia (watu) wanaowahudumia. Imefikia wakati hata Ulinzi wa Nguvu za Mungu hawauamini! Wamekuwa na Walinzi wa Kimwili zaidi. Huwa wana VITISHO sana kwa watu wanaowakosoa kiutendani! Wapo tayari Kushambulia kwa maneno au kushambulia kwa Vitendo, Kupiga mtu, Kutishia watu maisha na hata kutoa kauli za kumuua mtu!
5. Wananena kwa Lugha kwa staili ya maneno yale yale ya KUKARIRI yasiyozidi Kumi (10), yaani Lugha yetu wanayonena haipanuki kimaneno, maneno ni yale yale yaliyopo Dsm, Mwanza, Dodona na Morogoro, hayazidi zaid ya hapo! Na hawajui maana ya yale maneno wanayotamka!
6. Wanaongoza KUSENGENYANA wao kwa wao, lakini wakikutana pamoja ni kama wana Umoja wa Kazi ya Mungu na kumbe ndani yao ipo shida kubwa! Wanapenda Sifa sana, Kusifiwa, Kunyenyekewa na Kuabudiwa kuliko hata Mungu mwenyeqe. Hupenda kila wanalolifanya waonekane na watu! Hata akimsaidia mtu msaada wa nauli ya daladala ya Tshs 1,000/= wanataka Wamchukue picha (Selfee). Wakienda huko Maporini (Mlimani) kwa ajili ya kile wanachokiita Maombi ya Mlimani ndiyo usiseme! Hakuna maombi huko ni Vurudu za picha na Clip za shot Video. Hakuna Mungu huko zaidi ya maingizo ya maombi!
7. Wanapenda kunyang'anyana Waumini ndani ya majengo ya Ibada na hasa pale wanapoalikana Kihuduma. Wanapotoka hapo walipoalikwa kuhudumu huchukua namba za simu za Waumini wa eneo husika ili kuwahamisha na hasa wale wenye kuonekana wana Kipato kifedha! Hupenda sifa zaidi hata Waandishi na Mafarisayo kuwawafikii Mitume na Manabii wa zama hizi kwa sifa. Hupenda mashindano ya kuvaa Masuti ya gharama, Hushindana kula vyakula ya bei mbaya na bila kujua hapo mtaani kwake anapohudumu kuna watu ni Maskini wa kutubwa na wanalala na njaa. Hupenda zaidi kujionyesha kwa watu na hasa pale wanaponunua Magari ya kutembelea.
8. Wengi wao wana vinywa Vilivyojaa matusi na maneno Makali ambayo huwezi kumdhania. Wapo tayari kurusha picha za NGONO au mtu anayekata mauno! Halafu utamsikia mrushaji akisema "JAMANI ANGALIENI HAPA NDIPO DUNIA ILIPOFIKIA" na kumbe yeye ndiye anayependa mambo hayo na yamejaa kwa simu yake! Ukiwa nao na kuwaangalia ni Dakika 10 wanaweza kujifanya wapo Kiroho, lakini dakika chache wanakuwa watu wa Kimwili. Na wapo tayari kwenda kwa WAGANGA WA KIENYEJI ili kukuza Kundi la Watu.
9. Mahubiri yao Mitume na Manabii yameegemea zaidi kwenye AGANO LA KALE na hasa Vitabu vya MALAKI (Fungu la Kumi), ZABURI (Misingi ikiharibika), Urejesho wa nyota, Mafanikio wakimnukuu Ibrahimu Baba wa Imani. Bila kujua kwamba Ibrahimu yeye alishakuwa na mali nyingi kwa sababu ya Juhudi zake. Bali Mungu alichokifanya pale ni kumuongezea tu. Zaidi ya hapo hakuna mahubiri zaidi! Labda hapo yatafuata mahubiri ya Kichwani ya Kufoka (Kukoroma) pasipo na maandiko!
10. Wengi wao hawajui nini maana ya Utume Ki-Biblia wala hawajui maana ya Unabii Ki-Biblia. Hata ukimuuliza juu ya Yesu anaweza hata kukujibu kwamba Yesu siyo Mungu! Ndiyo maana kwa hapa Tanzania Mitume wengi na Manabii ndiyo wamekuwa ni Wachungaji wa Kanisa.